chinchilla coat
JF-Expert Member
- May 16, 2016
- 5,107
- 10,961
- Thread starter
- #181
Aisee wewe hatari, dhahabu na Almasi hazijaleta kipato ije application ya Wema. Dunia nzima wanamjuwa wema ahhhhhh. Nchi hii inatia huruma kweli.Kuna mtu alietengeneza app yake akawaalika viongozi wakagoma kwenda? Toa mfano. Nijuavyo hii ya wema Ni hatua kubwa sana MBELE KWANI SASA DUNIA NZIMA WANAWEZA KUZINUNUA KAZI ZA WEMA NA TAIFA LITAPATA KODI NA MAISHA KUSONGA MBELE.
Wema aliahidi lowasa hawezi kuwa rais ikatimia.
Ndio maana BAVICHA wanatokwa povu
Waziri anaacha BUNGE sbb ya Wema Sepetu apps... Mungu uko wapi..? Umetuacha pekee yetu bwana, umetusahau duniani, tu yatima, hatuoni, eeh Mungu hadi lini utarudi..? Ungekuwepo haya yote yasingetokea, uuuhh..!!
Ndugu yangu, ni waziri huyu huyu ambaye ana madaraka ya kuweza kuamka asubuhi bila kushauriana na yeyote akakifunga kituo cha redio au gazeti kwa muda anaotaka yeye hata kama kimeajiri watu elfu na kinalipa kodi vizuri!Sikuwa nimeiona hii thread wala kusikia hii app! haya maajabu! mawaziri wetu ndio walivyo hawajui majukumu yao na hawana viapaumbele.
Mkuu; mi Nilidhani application ya "dawasco"au "tanesco",warahisishe huduma zao...kumbe "Wema pepetu" bhanaWaziri wa habari, michezo na sanaa Nape Nnauye amesema msanii wa filamu Wema Sepetu amewapa heshima kubwa kwa ku launch application yake ya Wema Sepetu ambayo itakuwa inatoa taarifa za Wema.
Aliyasema hayo alipokuwa amehudhuria hafla hiyo aliyodai amehairisha kuhudhuria vikao vya bunge ili asiikose, pia amesema serikali itamsaidia na kumtangaza.
WAZIRI NAPE AZINDUA MFUMO WA KISASA WA WEMA SEPETU MOBILE APPLICATION
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akizindua mfumo wa kisasa kabisa wa msanii wa filamu hapa nchini,WEMA SEPETU MOBILE APPLICATION mbele ya waandishi wa habari, katika hotel ya Hyatt Regency jijini Dar.Picha na Geofrey Adroph(Pamoja Blog)
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh,Nape Nnauye akizungumza kabla ya kuzindua mfumo wa kisasa kabisa wa msanii wa filamu hapa nchini,WEMA SEPETU MOBILE APPLICATION mbele ya waandishi wa habari,katika hotel ya Hyatt Regency jijini Dar.
Msanii wa Bongo Movie na aliyewahi kuwa Miss Tanzania Maadam Wema Sepetu akizunguma mbele ya waandishi wa habari katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar kabla ya kuzindua huduma yake WEMA SEPETU MOBILE APPLICATION,ambayo itakuwa ikijumuisa matukio yake yote sambamba na video mbalimbali yatakayowekwa kwenye mfumo wa teknolojia ya kisasa kupitia simu za mikononi.
Mtaalamu wa huduma za mitandao kutoka Push Mobile, Haji Yussuph akifafanua jambo kuhusiana na huduma hiyo ya WEMA SEPETU MOBILE APPLICATION
Meneja wa Biashara wa Hartmann Trader ambao ndio watoa huduma ya Wema Sepetu Mobile Application,Cecil Mhina akifafanua namna huduma hiyo inavyoweza kutumika na pia maelezo kadhaa namna ya kujinga na kupata taarifa mbalimbali na video kupitia huduma hiyo
Munalove(kushoto) akimwelekeza mama mzazi wa Wema Sepetu jinsi ya kujiunga na WEMA SEPETU MOBILE APPLICATION mara bada ya kufanyika kwa uzinduzi huo
Msaniii wa Bongo Movie, Wema Sepetu akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye baada ya uzinduzi wa huduma hiyo kufanyika mbele ya waandishi wa habari, katika hotel ya Hyatt Regency jijini Dar.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa kazini
Msanii wa Bongo Movie na aliyewahi kuwa Miss Tanzania Maadam Wema Sepetu akifanya mahojiano na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi wake wa huduma ya WEMA SEPETU MOBILE APPLICATION
Wema Sepetu akiwa amemkumbatia mama yake mzazi mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi huo.
Picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi