Wewe acha maneno mengi, mliogopa kwa sababu ya nguvu aliyo nayo RA igunga.Nashukuru Mzee Mwanakijiji kwa comment yako,nahisi umepotoka kwa kiasi fulani kwa kukariri kuwa silaha ya CHADEMA ni issue ya ufisadi tu...Na ndio maana ulipoona kuwa hii silaha haikutumika sana umepata wasiwasi kidogo..well,kwenye vita unapaswa uwe na silaha mbalimbali na mbinu mbalimbali za kuweza kupambana na adui yako,hii ni kwasababu kila silaha au mbinu inafaa kwa mazingira husika tu...Uwezi ukawa unapigana vita kwenye jangwa ukavaa makombati ya kijani na nyeusi hapo utachemsha,uwezi tumia mshale kwenye vita vya silaha za moto mkuu!! Sasa CHADEMA kutotumia silaha ya ufisadi ni mbinu ya kawaida katika vita,na hata hivyo sidhani kama hii silaha haikutumika kama ambavyo wengi mnasema,baadhi ya maeneo niliwasikia Dr Slaa,na M/Kiti Mbowe wakisema jambo hili....Lazima chama kiwe na mbinu mbadala za kupambana katika uchaguzi,sasa Rostam alikuwa ametoka,utasema alikuwa fisadi itasaidia nini kwa wakati ulipo wakati sio mgombea?
Lakini pia Mwl Kashindye aliyekuwa mgombea wa CDM na Leopald Mahona aliyekuwa mgombea wa CUF walisema wazi kuwa kuna baadhi ya mambo aliyoyafanya Dr Kafumu akiwa kamishina wa Madini yameletea taifa hasara kubwa,sasa mlitaka wasemaje ndio mkubali kuwa walisema?
Conclusively;
Lazima chama kiwe na mbinu mbadala za kupambana,sio lazima kila siku msikie ufisadi! ufisadi! ufisadi! wananchi wanahitaji sera pia,TUTAWAFANYIA NINI na TUTAWATOAJE KWENYE UMASKINI HUU..Tusikariri!!!!