nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Wednesday, 04 May 2011 08:36
Rachel Balama na Rose Itono, Jijini
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeazimia kuandaa mkakati wa kuangalia ubora wa wanachama wake kuliko kuendelea kuwa na mamluki ndani ya chama hicho. Kauli hiyo imetolewa jana usiku na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Nape Nnauye, katika kipindi maalumu kinachorushwa na televisheni ya ITV kuhusu kujivua gamba kwa wanachama wa CCM.
Amesema chama hicho kina wingi wa wanachama wasio na sifa wala ubora ambao wamekuwa wakisababisha makundi ndani ya chama na kukivuruga chama.
Amesema CCM asilimia 80 ya wananchi ni wanachama wa CCM lakini baadhi yao hawana ubora, jambo ambalo lililosababisha chama kupoteza majimbo mengi katika uchaguzi uliopita.
Wanachama wa CCM ni wengi, lakini ubora wa wanachama ni mdogo ambao umesababisha wananchi kukosa imani na chama, amesema Nnauye.
Nnauye amewataka wana-CCM waliotakiwa kuwajibika wasiwe na chuki kwa kuwa hizo ni taratibu walizojiwekea katika chama.
Kuna watu wanafikiri kuwa kujivua gamba ni kwa ajili ya watu wawili au watatu. La hasha! Hiyo ni kwa ajili ya wanachama wote, amesema Nnauye.
Nnauye amewaomba wana-CCM kushikamana kuhakikisha kuwa chama kinaimarika na kurudisha imani kwa wananchi ambao walikuwa wameonesha kukatishwa tamaa na serikali ya chama hicho.
Nawaomba wananchi waliokuwa wamekata tamaa na chama kurudisha imani yao sasa hivi. Chama kimeshaanza kuimarika na hali ya kukiimarisha zaidi itaendelea hadi ngazi za chini, amesema Nnauye.
Ameongeza kuwa chama hicho kimekubaliana kutoa elimu kwa wanachama kabla ya kupewa kadi ili kuwawezesha wanachama wa chama hicho kukomaa kisiasa.
Amesema awali chama kilikuwa kikotoa kadi kwa wanachama kama njugu hali iliyopelekea chama hicho kupata wanachama wasio na sifa ndani ya chama.
Amewataka Watanzania kutarajia mabadiliko makubwa katika chama kwa maendeleo katika jamii kwa ujumla.
Nnauye ameongeza kuwa ndani ya sekretarieti yao wamekubaliana kuunda tume ya kumtafuta mgombea bora wa kiti cha Urais ambaye anakubalika ndani ya chama na jamii.
Rachel Balama na Rose Itono, Jijini
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeazimia kuandaa mkakati wa kuangalia ubora wa wanachama wake kuliko kuendelea kuwa na mamluki ndani ya chama hicho. Kauli hiyo imetolewa jana usiku na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Nape Nnauye, katika kipindi maalumu kinachorushwa na televisheni ya ITV kuhusu kujivua gamba kwa wanachama wa CCM.
Amesema chama hicho kina wingi wa wanachama wasio na sifa wala ubora ambao wamekuwa wakisababisha makundi ndani ya chama na kukivuruga chama.
Amesema CCM asilimia 80 ya wananchi ni wanachama wa CCM lakini baadhi yao hawana ubora, jambo ambalo lililosababisha chama kupoteza majimbo mengi katika uchaguzi uliopita.
Wanachama wa CCM ni wengi, lakini ubora wa wanachama ni mdogo ambao umesababisha wananchi kukosa imani na chama, amesema Nnauye.
Nnauye amewataka wana-CCM waliotakiwa kuwajibika wasiwe na chuki kwa kuwa hizo ni taratibu walizojiwekea katika chama.
Kuna watu wanafikiri kuwa kujivua gamba ni kwa ajili ya watu wawili au watatu. La hasha! Hiyo ni kwa ajili ya wanachama wote, amesema Nnauye.
Nnauye amewaomba wana-CCM kushikamana kuhakikisha kuwa chama kinaimarika na kurudisha imani kwa wananchi ambao walikuwa wameonesha kukatishwa tamaa na serikali ya chama hicho.
Nawaomba wananchi waliokuwa wamekata tamaa na chama kurudisha imani yao sasa hivi. Chama kimeshaanza kuimarika na hali ya kukiimarisha zaidi itaendelea hadi ngazi za chini, amesema Nnauye.
Ameongeza kuwa chama hicho kimekubaliana kutoa elimu kwa wanachama kabla ya kupewa kadi ili kuwawezesha wanachama wa chama hicho kukomaa kisiasa.
Amesema awali chama kilikuwa kikotoa kadi kwa wanachama kama njugu hali iliyopelekea chama hicho kupata wanachama wasio na sifa ndani ya chama.
Amewataka Watanzania kutarajia mabadiliko makubwa katika chama kwa maendeleo katika jamii kwa ujumla.
Nnauye ameongeza kuwa ndani ya sekretarieti yao wamekubaliana kuunda tume ya kumtafuta mgombea bora wa kiti cha Urais ambaye anakubalika ndani ya chama na jamii.