CHADEMA/UKAWA mna nia ya dhati ya kupambana na CCM?

2kimo

JF-Expert Member
Jan 23, 2014
2,029
2,071
Wana chadema/UKAWA hivi ni kweli mna nia ya dhati ya mapambano dhidi ya ccm?
Ni wakina nani wanaunda chadema? Lengo lao la dhati ni lipi hasa? Kuna kipindi nawaona chadema kama mamluki wa ccm au kama wanajitegemea basi ni kama genge la watu Fulani ambao labda hata ndoto zao hazifanani na za watanzania wengi wanaoaminishwa wapo pamoja! Ni ngumu kujua malengo ya magenge mengi na kwa bahati mbaya wapo watu wanaoweza kujituma ktk makundi ya jamii kuwa wapo naive na wanataka mabadiliko ya kweli, lkn hao ni kwa ajili ya decoy tu, Ila wapo kweli ambao ni mbumbumbu kama Mimi ambao hawajui hila za hawa mabwana wakubwa!
Hebu tujaribu kuona nia njema za chadema!
  1. Chama hakina ofisi yenye ulinganifu na ukubwa wake, yaani hakuna wa kujitolea kukijenga kwa michango yao kama ilivyofanywa na TANU ingawa kuna watu wanaonasibiwa kwa kuwa ni matajiri sana kama Lowasa au Mbowe na Ndesamburo/Mtei au basi hata kwa matumizi ya ruzuku!
  2. Kwa kadri muda unavyoenda chama kinakomaa lkn sio nafasi yake ya uongozi wa juu. Imekuwa kama ufalme ni ukoo mmoja tu wenye privilege ya kutawala na kama huna affiliation nao basi uñakuwa threat. Zitto, Slaa, Chacha, Kitila na Kaborou wanaweza kuwa mifano! Lkn pia tabia ya kukumbatia weak politicians nayo inashangaza zaidi! Mtu wa propaganda kuwa Salim Mwalimu ambaye nadhani wakati wa kampeni zilizopita alikuwa anapambana na kina kinana na Nape!
  3. Chadema ilipaswa kujenga misingi ambayo ndio ingakitambulisha kwa wananchi, kama TANU ilivyokuwa ndani ya mioyo ya watanzania mafukara waliojichangisha kwa kila hali kwa kuwa walikuwa wanawekeza katika chama chao! Lakini hapana, kimantiki ni ngumu kuitofautisha ccm na chadema kwa aina ya watu waliopo pande zote 2, mipango ya vyama vyote kutumia wizi wa kura, kudanganya watu na kutumia mbinu nyingine chafu!
Natamani kufahamishwa juu tofauti za kimkakati, dhamira, usafi na jambo lolote la kisiasa au kimaendeleo ambalo chadema wamekuja nalo kama ndio chachu na dira ya mabadiliko kwa watanzania!
Otherwise napata shida kuona kwanini mtu aiache ccm na kuchagua chadema hasa ukitazama uwekezaji wa vyama hivi kama vifuatavyo:-
Lumumba/Chamwino vs Ufipa
Magufuli vs Lowasa
kinana vs kivuli****
Nape vs Salim Mwalimu??
Mbowe vs Kikwete

Wazee
Mwinyi, Warioba, Salim, Mkapa, etc vs Mtei, Kingunge, Ndesamburo, Makani etc
Chadema think bigger, mnaweza msitegemee sana aina ya watu mlionao kutokana na umaarufu, wekezeni katika character!
Jengeni chama chenye muelekeo lkn msiwe wababaishaji! Or else wekeni dhamira yenu ya dhati hadharani ili watu wajue kwanini wawachague!
Vipo vyama vyenye malengo tofauti duniani na watu bado wanavichagua kutokana na msimamo yao! Trump anapewa support US leo kwa misimamo yake, just kuweni bayana tutawachagua kwa hiyari yetu!
 
rubbish belongs to the pit..this is an original stinky rubbish!!!
Agreed!
Lkn pia unaweza kuwa ni miongoni mwa wachache wanaofaidika na hivi vyama vya ujanja ujanja vinavyozuka kila msimu kusindikiza ccm!
Upinzani legelege unatujengea taifa legelege!
Mlichojiandaa ni kutukana, kukatisha tamaa wanaojaribu kufikiri kwa kuandika na kuropoka! Hiyo sio njia sahihi, ktk siasa wajinga huwa tunafahamishwa!
 
The amount of Stupidity in this Post is of high Degree
Nimekuona ulivyokuwa bright maana hata signature ktk profile yako umenukuu maneno ya mwanafalsafa mkubwa unayemuamini na kujivunia, Godbless Lema!
 
Nimekuona ulivyokuwa bright maana hata signature ktk profile yako umenukuu maneno ya mwanafalsafa mkubwa unayemuamini na kujivunia, Godbless Lema!

Mmawia
Pita huku Kaka uone Wehu wale JK anasema wakumbukwe na Magu kwa kazi zao Mtandaoni
 
Huyu KIWAVi..
Bosi wao kawambia wabane matumizi ya pesa, wao wamabana matumizi ya kutumia akili..
Ngoja muone wakurupukaji wenzie wakija..
Matusi na kashfa ndio mtaji wenu Mkuu!
Unless wewe ni mnufaika na mfumo chadema lkn hatuwezi kuwa na taasisi holela zinazojiita vyama vya ukombozi!
TANU haikuwa subjected ktk auditing lkn nadhani kila senti ilitumika vema, leo mkombozi mpya kaja na anaafeli ktk auditing akiwa bado an infant!
Mkombozi hapaswi kufanana na shetani, vinginevyo mtu haiitaji kukombolewa!
 
Sawa nimekuona lakini huna uliloliandika lenye kufikirisha. Au umekuja kihivi ili ufikiriwe Kama alivyoomba mwenyekiti wako jk? Hebu eaambie basi juu ya hatma ya zanzibar. In kwanini mnaivunja katiba waziwazi hivi? Au MNA imani kuwa wananchi si waelewa wa sheria na katiba? Kafikirie namna nyingine ya kupewa hisani Lumumba st.
 
Siku hizi humu badala ya hoja kujibiwa ni matusi kwa mtoa hoja ....sijawahi kushuhudia humu mtu yeyote aliyesifiwa kwa kutoa ushauri mzuri Chadema .....nafikiri Chadema wamejipanga kuwa chama cha kudumu cha upinzani ....
 
Mmawia
Pita huku Kaka uone Wehu wale JK anasema wakumbukwe na Magu kwa kazi zao Mtandaoni
We unaona tofauti gani kati ya JK na EL!
Mngeshinda na ile team yenu iliyokamatwa mngepewa tu zawadi!
Ndio maana nasema hakuna tofauti kati yenu na ccm, so how comes watu wawachague wakati hamna new package!
 
We unaona tofauti gani kati ya JK na EL!
Mngeshinda na ile team yenu iliyokamatwa mngepewa tu zawadi!
Ndio maana nasema hakuna tofauti kati yenu na ccm, so how comes watu wawachague wakati hamna new package!
Hueleweki hata unataka nini
Yaani kama bint anayevunja Ungo
Samahani lakini
 
Hueleweki hata unataka nini
Yaani kama bint anayevunja Ungo
Samahani lakini
Kamwe sitorudishia matusi yako! Mimi nataka kujifunza toka kwa watu werevu, naomba nisitukane!
Thread hii inajieleza!
Nataka kujua political agenda ya chadema!
Pia nataka kujua ni kwa jinsi gani agenda za chadema zipo tofauti na zile za ccm!
 
Kamwe sitorudishia matusi yako! Mimi nataka kujifunza toka kwa watu werevu, naomba nisitukane!
Thread hii inajieleza!
Nataka kujua political agenda ya chadema!
Pia nataka kujua ni kwa jinsi gani agenda za chadema zipo tofauti na zile za ccm!
Heading na content haviendani
 
Siku hizi humu badala ya hoja kujibiwa ni matusi kwa mtoa hoja ....sijawahi kushuhudia humu mtu yeyote aliyesifiwa kwa kutoa ushauri mzuri Chadema .....nafikiri Chadema wamejipanga kuwa chama cha kudumu cha upinzani ....
Nadhani JF inapaswa kuchange policy!
Watu wapoteze status zao kama contributions zao ni matusi! Unawezaje kuwa na xpert member anayetukana tu mwanzo mwisho!
 
2kimo, moja ya point uliyoorodhesha ni kuhusu muundo wa kiungozi wa Chadema. Ni lini Chadema tutaona ipo haja ya kujenga uongozi wenye taswira ya kitaifa kuliko hii yenye taswira ya kikabila na kikanda??
Ifikie kipindi sasa Chadema tuelewe na tujiamini kuwa sisi ndio chama kikuu cha upinzani TANZANIA sio chama kikuu cha upinzani ARUSHA na KILIMANJARO. Tukiibadilisha hii taswira ya kiuongozi itakuwa rahisi kuiua hii sumu inayoenea taratibu kwa wananchi kuwa chadema ni chama cha ukoo na kabila fulani vinginevyo tutaendelea kuwa chama cha upinzani.
 
umeandika ndeeeefu lakini ni matakataka matupu ? aliyekudanganya kwamba ccm waliwekeza ni nani ? kupora na kuhodhi mali ya umma ni uwekezaji ? halafu nakuonya kwa mara ya mwisho , ni marufuku kumlinganisha kiongozi mkubwa sana Salum Mwalimu ( kaimu katibu mkuu ) na mtu mdogo sana anayetumwa na kinana kama nape , dharau haitakusaidia kitu .
 
Toka Jk kasema mkumbukwe mmeanza kupost utumbo wenu. Magufuli usiwalipe hawa vilaza wala kuwakumbuka
kuna taarifa kwamba wameishaanza kurogana , kisa ukuu wa wilaya ! kiongozi wao VUTA NKUVUTE amerogwa vibaya sana , ndio maana haonekani siku hizi .
 
Back
Top Bottom