kushinda kunapokaribiwa kushindwa wahusika hujitahidi kutumia kila namna kuonekana kuwa wanakaribia kushinda ili hali kiukweli ni kwamba wanashindwa.
Leteni hata wabibi kwenye gwaride ila ukweli utabaki palepale.
Watoto wao wako darasani kwenye shule za Saints Saints, hawa wa walalahoi wanaokaa chini sio tu wanasoma kwenye mazingira magumu lakini bado hawaachwi wakaa darasani - wanawekwa kwenye jua kuwambia wakubwa! Kuna uonevu zaidi ya huu? Mtoto wa maskini hana lake nchi hii.
Hii inanikumbusha enzi za zamani sana za Chipukizi. Kuna mtu anaitwa Cosmas Kasangani, yule alikuwa mmoja wa mashahidi kwenye kesi ya ubunge ya Tundu Lissu. Huyu jamaa kaanza long time alikuwa kinara wa kunoa watoto kucheza magwaride ya CCM. Jamaa alikuwa mwalimu wa shule ya msingi Isike pale Tabora ila alikuwa ni trainer mzuri sana wa chipukizi. Ila baada ya kuanzishwa sheria ya vyama vingi ilikubalika kuwa sasa watoto wa mashuleni waachwe wasome. Sasa sijui hawa watoto Nape kawatoa wapi?, je kila chama kikiwa na vijana wake kama hawa tutajenga taifa la aina gani?. Siasa tuwaachie watu walifikia umri wa kuwa na utashi wa kuamua sasa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.