Msema hovyo
Senior Member
- Jul 3, 2011
- 195
- 86
Katika kuchunguza kwangu uhalisia wa mambo nimegundua kwamba Lowassa anasakamwa kutokana na kuonekana kuwa ni mtendaji mzuri kumshinda Kikwete, jambo ambalo lilikuwa linahatarisha reputation ya Kikwete kama Rais.
Nape naye kwa kutokuelewa akakakurupuka tu na kuanza kumtaja Lowassa kama fisadi. Lakini mimi leo nataka mwenye data za ufisadi wa Lowassa na aseme hapa. Lowassa amefisadi nini? Watu mnapayuka tu Richmond, richmond, lakini hakuna anayesema Lowassa alipata bei gani kutoka kwenye ile Kampuni. Wote tunajua kwamba Rostam alipata bilioni 40 za kagoda kupitia kagoda, pia tunajua ndiye aliyekuwa mmiliki wa Richmond ambayo baadaye ilibadilishwa na kuwa dowans. Pia tunajua kwamba Chenge alituibia hela ya rada.
Sasa Lowassa ameiba nini kilicho dhahiri? Ninachoamini mimi Lowassa aliponzwa na utendaji wake, wa kutaka kupush mambo yaende. Hakuwa legelege kama Pinda ambaye anang'aa tu macho huku watanzania wakiteseka kutokana na ukosefu wa umeme. Lakini katika harakati za kuhakikisha watanzania wanapata umeme ontime Lowassa alijikuta analazimika kumpush Msabaha aharakishe utoaji wa tenda kwenye kampuni iliyopitishwa na kamati, bahati mbaya kampuni iliyopitishwa ikawa fake.
Lowassa hakuwa kwenye kamati ya kupitisha mzabuni wa kuleta mitambo ya umeme, na wala hakuna mahali panapoonyesha kwamba Lowassa alimwambia Msabaha lazima apitishe richmond badala ya makampuni mengine. Tuna ushahidi wa kimazingira juu ya ufisadi wa Chenge (vijisent), na ule wa Rostam ambaye alijitambulisha kuwa msimamizi wa Dowans. Sasa Lowassa ufisadi wake upo wapi?
Ninaamini kwamba Lowassa anaandamwa kutokana na utendaji wake, ati ni tishio kwa uongozi wa Kikwete, pia na fitina za Nape dhidi yake.
Nape naye kwa kutokuelewa akakakurupuka tu na kuanza kumtaja Lowassa kama fisadi. Lakini mimi leo nataka mwenye data za ufisadi wa Lowassa na aseme hapa. Lowassa amefisadi nini? Watu mnapayuka tu Richmond, richmond, lakini hakuna anayesema Lowassa alipata bei gani kutoka kwenye ile Kampuni. Wote tunajua kwamba Rostam alipata bilioni 40 za kagoda kupitia kagoda, pia tunajua ndiye aliyekuwa mmiliki wa Richmond ambayo baadaye ilibadilishwa na kuwa dowans. Pia tunajua kwamba Chenge alituibia hela ya rada.
Sasa Lowassa ameiba nini kilicho dhahiri? Ninachoamini mimi Lowassa aliponzwa na utendaji wake, wa kutaka kupush mambo yaende. Hakuwa legelege kama Pinda ambaye anang'aa tu macho huku watanzania wakiteseka kutokana na ukosefu wa umeme. Lakini katika harakati za kuhakikisha watanzania wanapata umeme ontime Lowassa alijikuta analazimika kumpush Msabaha aharakishe utoaji wa tenda kwenye kampuni iliyopitishwa na kamati, bahati mbaya kampuni iliyopitishwa ikawa fake.
Lowassa hakuwa kwenye kamati ya kupitisha mzabuni wa kuleta mitambo ya umeme, na wala hakuna mahali panapoonyesha kwamba Lowassa alimwambia Msabaha lazima apitishe richmond badala ya makampuni mengine. Tuna ushahidi wa kimazingira juu ya ufisadi wa Chenge (vijisent), na ule wa Rostam ambaye alijitambulisha kuwa msimamizi wa Dowans. Sasa Lowassa ufisadi wake upo wapi?
Ninaamini kwamba Lowassa anaandamwa kutokana na utendaji wake, ati ni tishio kwa uongozi wa Kikwete, pia na fitina za Nape dhidi yake.