Nape Nnauye CCM ina rasilimali zenye thamani zaidi ya sh. bil 50 yajipanga kutotegemea ruzuku

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Na Irene Mark

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema chama hicho kimejipanga kutumia rasilimali zake zenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 50 kujiimarisha kiuchumi ili kupunguza utegemezi wa ruzuku.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi ndogo za chama hicho jijini Dar es Salaam jana, Nape alisema wamewaalika wafanyabiashara 30 wa Chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini, ili kujifunza namna ya kutumia vema rasilimali za CCM.

Alisema ujio wa wafanyabiashara hao wa ANC ni sehemu ya mageuzi ndani ya chama chao na kwamba wataingia nchini leo kwa ziara ya siku tano ambapo watashiriki kongamano la kibiashara lililoandaliwa na Tanzania Chamber of Commerce, Industries and Agriculture (TCCIA).


"Itakumbukwa kuwa katika maamuzi ya kufanya mageuzi ndani ya chama yanayoendelea, Chama Cha Mapinduzi kiliamua kuongeza juhudi katika kukifanya chama kipunguze au kumaliza kabisa utegemezi wa ruzuku katika kuendesha mambo yake.


"Hivyo basi, ziara hii ni sehemu ya utekelezaji wa maamuzi hayo… lengo ni kujipanua kiuchumi na kujifunza namna bora ya kuwekeza hasa tukizingatia kuwa ANC ni chama kikongwe kwenye siasa barani Afrika hivyo wenzetu wana uzoefu zaidi.


"Wakati wenzetu wanachangishana kuendesha vyama vyao sisi tutawekeza," alisisitiza Nape na kuongeza kwamba watatumia vema makampuni yanayomilikiwa na CCM.


Alibainisha kuwa malengo ya ziara hiyo ni kutafuta fursa mbalimbali za uwekezaji zitakazodumisha na kuendeleza uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya ANC na CCM ikiwemo kubadilishana uzoefu wa makampuni ya vyama hivyo.


Alisema wafanyabiashara hao watatembelea kambi za Mazimbu mkoani Morogoro zilizotumika kuandaa wapigania uhuru wa ANC wakati wa harakati za ukombozi wa nchi yao.


Alisema wataalamu mbalimbali wa CCM na jumuiya zake watashiriki kwenye ziara hiyo ili kujifunza na kupata uzoefu katika uanzishaji, usimamizi na uendeshaji wa vitega uchumi vya chama.


 
Wezi tu hao ccm ipo siku tuzirudisha mikononi mwa umma hizo wanazodai kuwa ni rasilimali zao. Wanadai wana rasilimali bila hata aibu. Haya majizi haya...
 
Baba unamwita jirani aje kukufundisha namna ya kupanga bajeti ya familia yako.
Nape kakosa cha kuongea, Cha msingi ni hii issue ya M4C inawanyima raha wezi wa rasilimali za Tanzania.
 
"Wakati wenzetu wanachangishana kuendesha vyama vyao sisi tutawekeza,"

Wenzenu ndio akina nani?mbona wenzenu hasa kwa maana ya neno hilo ni CUF?Au unamaanisha CHADEMA?Kama ndivyo,kwani na nyinyi mnayo haja kweli ya kuchangiwa na wananchi?Kama hatufanani itikadi,kwa nini basi iwe lazima kuwa na mikakati inayofanana?
kwani si mmekuwa mnasifika kwa kugawa pesa,pilau,chumvi...au mnadhani kile ambacho mmekuwa mnagawa hakiwaridhishi wapokeaji?
Iweje mmekuwa mnadai kuna umuhimu wa kutenganisha siasa na biashara, halafu leo chama cha siasa, CCM ,kinatarajia kujihusisha na masuala ya biashara (kuwekeza)?Halafu inawezekanaje ufanye biashara bila kumnyonya mtu?
Mpango huu ni kinyume kabisa na nadharia za Karl Max ambazo Kambarage alizitumia kuijenga TANU na baadaye CCM!!Alimradi mkanganyiko mtupu!!!
 
CCM warudishe viwanja vyote kwa wananchi kwanza..ikifutiwa na ofisi zilizojengwa kwa pesa za umma

Hata baada ya nyie kuolewa na CCM hapo Zenji bado tu hamjanufaika na rasilimali hizi????
Au ndo mke hajui password ya ATM card ya mumewe???
 
Rasilimali za CCM? Walizopora au walizokwiba? Kuna kitu kwenye chama hiki kinawafanya wanachama wake wakose umakini kwa yale wanayoyatamka na wanayoyatenda, sijui ni laana gani hii! Ni kama nyang'au kusimamia rasilimali za mfugaji wa kondoo na mbuzi!



Nape: Kikao kijacho CCM kuja na maamuzi mazito.​

Nape Nnauye said:
(Akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari katika ziara yake aliyoifanya jijini Mwanza mapema mwaka jana)

Ni suala la maadili na ujumla wake, maadili yanapimwa na nini? Maadili yanapimwa na imani ya Chama Cha mapinduzi, ukiapa kule nyuma unasema 'Rushwa ni adui wa haki sitapokea wala kutoa rushwa, Cheo ni dhamana sito tumia cheo changu wala cha mwingine..'

Kwa hiyo siyo suala la Nape wala la nani, hili ni suala la Chama, Nape atakufa yatabaki haya. Yamekuwepo mimi sijazaliwa, nimezaliwa nimeyakuta, nitayasimamia nitaondoka nitayaacha...!

Swala la lini? Chacha unajua kikao hakipangi Nape, kikao kinapangwa na mamlaka iliyopo... lakini ni kikao kijacho. Mimi naamini kikao kijacho tunamalizana na habari hii (kuvuana magamba?)

Ni baada ya tambo hizi, RA akampiga marufuku Nape kukanyaga Igunga na leo hii EL hataki hata kuona sura yake Arumeru na Sioi aliyesemekana alipitishwa kwa rushwa ndiye anaipeperusha bendera ya CCM Arumeru. Wakati walafi kama Ole Sendeka wanalamba matapishi yao, masikini mnafiki Nape eti bado anasubiri kikao kijacho cha CCM kichukue maamuzi magumu!
 
Last edited by a moderator:
50 billions is not news! gaddafi alikuwa na pipes za mafuta na gdp za billions, lakini wapi alipo....CCM assets my foot! hayo majengo anayosema ni assets afikirie upya. it took few tnt to bring down na assets will be less than 50m. tutaifanya nchi mpya safari yetu ya nchi ya ahadi bado inaendelea. this is not the country we promised we will get there.
 
Hata mngekuwa na over 100bl kwa mtaji huu wa kugawa fedha ovyo ovyo haitoshi kabisa.

Lingine CCM haina la kujivunia kwa sababu imenufaika sana na mfumo wa chama kimoja.
 
50 billions is not news! gaddafi alikuwa na pipes za mafuta na gdp za billions, lakini wapi alipo....CCM assets my foot! hayo majengo anayosema ni assets afikirie upya. it took few tnt to bring down na assets will be less than 50m. tutaifanya nchi mpya safari yetu ya nchi ya ahadi bado inaendelea. this is not the country we promised we will get there.

Hatutaharibu majengo yetu mkuu,hizo ni rasilimali za wananchi,zilipatikana kwa nguvu ya wananchi,c.c.m wasivyo na a**** wakajimilikisha wakiamini watatawala milele,rasilimali za zitarudi kwa wananchi mkuu,hii si nchi ya c.c.m bali ni Watanzania
 
Na Irene Mark

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema chama hicho kimejipanga kutumia rasilimali zake zenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 50 kujiimarisha kiuchumi ili kupunguza utegemezi wa ruzuku.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi ndogo za chama hicho jijini Dar es Salaam jana, Nape alisema wamewaalika wafanyabiashara 30 wa Chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini, ili kujifunza namna ya kutumia vema rasilimali za CCM.

Alisema ujio wa wafanyabiashara hao wa ANC ni sehemu ya mageuzi ndani ya chama chao na kwamba wataingia nchini leo kwa ziara ya siku tano ambapo watashiriki kongamano la kibiashara lililoandaliwa na Tanzania Chamber of Commerce, Industries and Agriculture (TCCIA).


“Itakumbukwa kuwa katika maamuzi ya kufanya mageuzi ndani ya chama yanayoendelea, Chama Cha Mapinduzi kiliamua kuongeza juhudi katika kukifanya chama kipunguze au kumaliza kabisa utegemezi wa ruzuku katika kuendesha mambo yake.


“Hivyo basi, ziara hii ni sehemu ya utekelezaji wa maamuzi hayo… lengo ni kujipanua kiuchumi na kujifunza namna bora ya kuwekeza hasa tukizingatia kuwa ANC ni chama kikongwe kwenye siasa barani Afrika hivyo wenzetu wana uzoefu zaidi.


“Wakati wenzetu wanachangishana kuendesha vyama vyao sisi tutawekeza,” alisisitiza Nape na kuongeza kwamba watatumia vema makampuni yanayomilikiwa na CCM.


Alibainisha kuwa malengo ya ziara hiyo ni kutafuta fursa mbalimbali za uwekezaji zitakazodumisha na kuendeleza uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya ANC na CCM ikiwemo kubadilishana uzoefu wa makampuni ya vyama hivyo.


Alisema wafanyabiashara hao watatembelea kambi za Mazimbu mkoani Morogoro zilizotumika kuandaa wapigania uhuru wa ANC wakati wa harakati za ukombozi wa nchi yao.


Alisema wataalamu mbalimbali wa CCM na jumuiya zake watashiriki kwenye ziara hiyo ili kujifunza na kupata uzoefu katika uanzishaji, usimamizi na uendeshaji wa vitega uchumi vya chama.



Nape wanaokuja ni wafanyabiashara na siyo wanasiasa sasa nyie ccm mnafanyabiashara?huo ujio unaweza usiwe mtaji mzuri sana kama unavyotarajia.usizungumzie ruzuku tu zungumzia pia na pesa mnazochukuwa kwa wahindi na wafanyabiashara wakubwa na kuwapa vyeti.
Tofautisheni ujio wa kisiasa na kibiashara
 
Kabla hawaja piga mahesabu ya mali zao ni bora wangerudisha mali zote walizozipora kwa watanzania kama viwanja, majengo na viwanja vya wazi na stendi ili hesabu zao zikae sawa kwani zitakapo rudishwa na utawala mwingine watajiona ni chama ambacho hakina assets nyingi kama wanavyofikiria.
 
Huyu anazungumzia rasilimali za Taifa ambazo CCM walijimilikisha wakati wa Chama Kimoja?
Viwanja vya mpira, Jengo la Umoja wa vijana wa TANU, Baadhi ya majengo ya Serikali, Magari ya Serikali n.k
Hata Ikulu ni mali ya CCM manake vikao vya Chama hufanyikia Ikulu siku hizi..

Damn!!
 
Na Irene Mark

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema chama hicho kimejipanga kutumia rasilimali zake zenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 50 kujiimarisha kiuchumi ili kupunguza utegemezi wa ruzuku.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi ndogo za chama hicho jijini Dar es Salaam jana, Nape alisema wamewaalika wafanyabiashara 30 wa Chama cha African National Congress (ANC) cha Afrika Kusini, ili kujifunza namna ya kutumia vema rasilimali za CCM.

Alisema ujio wa wafanyabiashara hao wa ANC ni sehemu ya mageuzi ndani ya chama chao na kwamba wataingia nchini leo kwa ziara ya siku tano ambapo watashiriki kongamano la kibiashara lililoandaliwa na Tanzania Chamber of Commerce, Industries and Agriculture (TCCIA).


"Itakumbukwa kuwa katika maamuzi ya kufanya mageuzi ndani ya chama yanayoendelea, Chama Cha Mapinduzi kiliamua kuongeza juhudi katika kukifanya chama kipunguze au kumaliza kabisa utegemezi wa ruzuku katika kuendesha mambo yake.


"Hivyo basi, ziara hii ni sehemu ya utekelezaji wa maamuzi hayo… lengo ni kujipanua kiuchumi na kujifunza namna bora ya kuwekeza hasa tukizingatia kuwa ANC ni chama kikongwe kwenye siasa barani Afrika hivyo wenzetu wana uzoefu zaidi.


"Wakati wenzetu wanachangishana kuendesha vyama vyao sisi tutawekeza," alisisitiza Nape na kuongeza kwamba watatumia vema makampuni yanayomilikiwa na CCM.


Alibainisha kuwa malengo ya ziara hiyo ni kutafuta fursa mbalimbali za uwekezaji zitakazodumisha na kuendeleza uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya ANC na CCM ikiwemo kubadilishana uzoefu wa makampuni ya vyama hivyo.


Alisema wafanyabiashara hao watatembelea kambi za Mazimbu mkoani Morogoro zilizotumika kuandaa wapigania uhuru wa ANC wakati wa harakati za ukombozi wa nchi yao.


Alisema wataalamu mbalimbali wa CCM na jumuiya zake watashiriki kwenye ziara hiyo ili kujifunza na kupata uzoefu katika uanzishaji, usimamizi na uendeshaji wa vitega uchumi vya chama.



Hizo zote ni mali za wananchi. Mfano CCM Kirumba ni mchango wa wananchi, nakumbuka mimi nilichangia ujenzi wa Ali Hassan Mwinyi Tabora. Wakati nalazimishwa kuchangia sikuwa na chama, sasa kama mimi nimejiunga na chama cha siasa naomba nirudishiwe mchango huo ili niupeleke kwenye chamma changu pinzani. na njia nzuri ni kuzirudisha mali zote za CCM serikalini na kuendelea kutoa ruzuku kwa ajili ya kuendesha vyama vya siasa!!
 
“Wakati wenzetu wanachangishana kuendesha vyama vyao sisi tutawekeza,”

Wenzenu ndio akina nani?mbona wenzenu hasa kwa maana ya neno hilo ni CUF?Au unamaanisha CHADEMA?Kama ndivyo,kwani na nyinyi mnayo haja kweli ya kuchangiwa na wananchi?Kama hatufanani itikadi,kwa nini basi iwe lazima kuwa na mikakati inayofanana?
kwani si mmekuwa mnasifika kwa kugawa pesa,pilau,chumvi...au mnadhani kile ambacho mmekuwa mnagawa hakiwaridhishi wapokeaji?
Iweje mmekuwa mnadai kuna umuhimu wa kutenganisha siasa na biashara, halafu leo chama cha siasa, CCM ,kinatarajia kujihusisha na masuala ya biashara (kuwekeza)?Halafu inawezekanaje ufanye biashara bila kumnyonya mtu?
Mpango huu ni kinyume kabisa na nadharia za Karl Max ambazo Kambarage alizitumia kuijenga TANU na baadaye CCM!!Alimradi mkanganyiko mtupu!!!

Inashangaza kwa kweli yaani chama cha kijamaa lakini kinafanya biashara za kuwanyonya wananchi? Ni bora watangaze tu kwamba ujamaa umekufa.
 
MOvement for Changes imewaogopesha CCM hadi Nape kaamua kutangaza kuwa CCM sio chama cha kijamaa bali ni chama cha kibepari.
Serikali ya CCM imeshindwa kuendeleza viwanda na kuviua kwa kutumia sera ya ubinafsishaji, ni CCM hii tena inasema inaendeleza viwanda kwa manufaa ya chama???
CCM is running away like headless chicken.
 
Back
Top Bottom