Katika kauli ambazo wanasiasa wanatakiwa kuepuka ni kauli za kichochezi. Nilihuzunika sana nlvomsikia Nape akiwahadaa Watanzania kuwa Tanzania inawenyewe na wenyewe ni CCM. Sijajua kama Katiba inasema nchi hii ni ya chama fulani,kabila,wala dini. Nape Nnauye anatakiwa kuwa makini na kauli zake. Mie sitoshangaa kesho akisema Tanzania ni ya wapagani au Waislamu au basi ya Wakristu au wachaga au wasukuma. CCM wawe makini na watoa kauli kama hizi za Nape.