Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Jamvi hili mara kwa mara limekuwa likitoa ushari wa dhati kabisa kwa Nape pamoja na kuwa yeye pia ni mdau humu nimeshindwa kuelewa ni kwamba haelewi au amekuwa sikio la kufa......... Nimechukua baadhi ya maneno au majibu ya Wilson Mukama (Katibu Mkuu wa CCM) dhidi ya Nape ili hoja hii ikae sawa (Source Mwanahalisi)
1. Taarifa zinamnukuu Mukama akimueleza Nape " ............nimeambiwa umekwenda Igunga, wakati Kamati Kuu ya Chama imekuzuia kwenda huko. Unataka nini? Mbona unataka kutuharibia uchaguzi? alifoka Mukama
2. Mukama kwa hasira alihoji, "Nape kwa nini umekwenda Igunga? Alipojaribu kujitetea kwamba alikwenda huko kuhani, Mukama alisema, "Nani amekutuma? Nani amekuruhusu? Kijana tafadhali usituharibie uchaguzi"
3. Mukama akamuuliza Nape, "Nimeambiwa unajiandaa kwenda Igunga, mbona wewe kijana husikii?
Nyongeza ya Hayo; Baada ya ufunguzi wa Kampeni Mukama akiwa mwenye furaha, aliwaambia baadhi ya viongozi na wanachama wa chama hicho, "Tumefanikiwa sana katika mkutano wetu huu, kuna watu wengine bwana hawana Discipline (nidhamu), hawana adabu wanajiona wanaweza kuvuta watu kwenye mkutano. Mwiguru Nchemba anafanya kazi nzuri sana. Ameratibu mkutano huu vizuri Kampeni zimekwenda vema. Ni kijana mwenye busara sana yule"
Kwa kauli hii ya Mukama kuna maswali ya kujiuliza; Mosi ni watu gani hao wasio na nidhamu na adabu? Pili ni nani anayefanya kazi mbaya? Tatu ni kijana yupi asiye na busara kama za Nchemba?
Mwandishi (Alfred Lucas) anasema, alipowasiliana na Nape ili kuthibitsha haya au kukanusha majibu ya Nape yakawa haya "Alfred, mimi sina la kusema juu ya hilo, Nape akauliza, Jamani mimi kijana mwenzenu nimewakosea nini? Niambieni basi"
Binafsi sina shaka hata kidogo juu ya maneno ya Wilson Mukama kwa Nape hayo yanathibitika si tu kwa Alfred Lucas bali wenye uwezo wa kufahamu tunafahamu haya kuwa ni ya kweli labda mazungumzo ya Nape na Alfred ndiyo ninayoweza kusema kuwa siwezi kuyanenea ila vile vile Alfred hana sababu yeyote ya kudanganya juu ya majibu aliyoyatoa Nape.
Swali langu wanajamvi; is this not embarassement? Hivi ni mpaka Malaika ashuke ndo Nape atapata uelewa au? What else do he want........ Ni kweli kwamba anahitaji vijana wamwambie alichowakosea au? (Mtu kama Mwita si lazma ajibu hili)
1. Taarifa zinamnukuu Mukama akimueleza Nape " ............nimeambiwa umekwenda Igunga, wakati Kamati Kuu ya Chama imekuzuia kwenda huko. Unataka nini? Mbona unataka kutuharibia uchaguzi? alifoka Mukama
2. Mukama kwa hasira alihoji, "Nape kwa nini umekwenda Igunga? Alipojaribu kujitetea kwamba alikwenda huko kuhani, Mukama alisema, "Nani amekutuma? Nani amekuruhusu? Kijana tafadhali usituharibie uchaguzi"
3. Mukama akamuuliza Nape, "Nimeambiwa unajiandaa kwenda Igunga, mbona wewe kijana husikii?
Nyongeza ya Hayo; Baada ya ufunguzi wa Kampeni Mukama akiwa mwenye furaha, aliwaambia baadhi ya viongozi na wanachama wa chama hicho, "Tumefanikiwa sana katika mkutano wetu huu, kuna watu wengine bwana hawana Discipline (nidhamu), hawana adabu wanajiona wanaweza kuvuta watu kwenye mkutano. Mwiguru Nchemba anafanya kazi nzuri sana. Ameratibu mkutano huu vizuri Kampeni zimekwenda vema. Ni kijana mwenye busara sana yule"
Kwa kauli hii ya Mukama kuna maswali ya kujiuliza; Mosi ni watu gani hao wasio na nidhamu na adabu? Pili ni nani anayefanya kazi mbaya? Tatu ni kijana yupi asiye na busara kama za Nchemba?
Mwandishi (Alfred Lucas) anasema, alipowasiliana na Nape ili kuthibitsha haya au kukanusha majibu ya Nape yakawa haya "Alfred, mimi sina la kusema juu ya hilo, Nape akauliza, Jamani mimi kijana mwenzenu nimewakosea nini? Niambieni basi"
Binafsi sina shaka hata kidogo juu ya maneno ya Wilson Mukama kwa Nape hayo yanathibitika si tu kwa Alfred Lucas bali wenye uwezo wa kufahamu tunafahamu haya kuwa ni ya kweli labda mazungumzo ya Nape na Alfred ndiyo ninayoweza kusema kuwa siwezi kuyanenea ila vile vile Alfred hana sababu yeyote ya kudanganya juu ya majibu aliyoyatoa Nape.
Swali langu wanajamvi; is this not embarassement? Hivi ni mpaka Malaika ashuke ndo Nape atapata uelewa au? What else do he want........ Ni kweli kwamba anahitaji vijana wamwambie alichowakosea au? (Mtu kama Mwita si lazma ajibu hili)