WANAJAMVI,poleni kwa majukumu ya kila siku ya kujikwamua kimaisha na kulijenga taifa letu ,kumekuwa na mijadala ya mipana ya kisiasa hapa nchini na baadhi ya mijadala mingine imekuwa ikinikera sana haswa kwa baadhi ya wanasiasa uchwara (gutter politicians) kwa kuwaona wachaga wote wapo chadema na hivyo unapozungumzia chadema humtengi mchaga napata shida kwasababu mimi ni mwanaccm damu damu tangu nikiwa mtoto nimeingia ccm nikiwa mwanaskauti sasa ni mtu mzima nipo ccm bado,sasa jinsi watu wanavyolisema hili kabila langu vibaya kwa wale waliopo vyama vingine kama kina mbowe,lema,john mrema,komu n.k napata shida kwamba sisi wachaga tuliopo huku ccm tupo kimakosa tumekuja kwenye kabila gani,je ccm ni chama cha kabila gani naomba mnisaidie
CCM ni chama cha wote bila ya kujali kabila,dini au rangi. Dhana ya Chadema na uchagga inatokana na ukweli kwamba mwasisi licha ya kuwa mchagga, inawafuasi wengi kutoka kabila hilo ukilinganisha na makabila mengine na mngmt team ina wachagga wengi kuliko makabila mengine. Pia wafia chama wengi au wanachama watiifu ni kutoka kabila hilo. Hata CUF na upemba msingi wake ni huohuo.