Nape mpinga Rushwa.Je atafanikiwa?Ona hii

Mwanajamii

JF-Expert Member
Mar 5, 2008
7,063
68







  • [h=6]Nape Moses Nnauye
    [/h] [h=6]IMANI YA CCM; Rushwa ni adui wa haki.,sitapokea wala kupokea rushwa...! ni imani yetu na muongozo tunaoufuata yeyote aliye nje ya iman hii si mwanaCCM bali ni muasi katika CCM.[/h]






My take;hii kitu inahitaji meno kweli kweli.
 
Si kweli kuwa viongozi wote ccm wanachukua ama kutoa rushwa, lakini pia si kweli kuwa hakuna hatua za kinidhamu ambazo chama kinawachukulia wale waliothibitika katika sheria kuwa wamekula rushwa, lakini pia hili la kupinga rushwa si kweli kuwa lipo theoretically bali ni practically kwani rushwa CCM imepingwa tangu katika misingi na imani ya Tanu-1954, kisha azimio la arusha-1967 kisha kwenye katiba ya CCM ya mwaka 1977. Lakini tangu hapo wapo viongozi kadhaa ambao walijihusisha na rushwa walichukuliwa hatua na kuwajibishwa kwa namna mbalimbali. Katika CCM si tu kuwa maandiko na kanuni zetu zinatuelekeza kulipinga hili bali tunalidhihirisha hili katika maneno yetu na matendo yetu kama chama.@abdullah, adam george,easther na december...!....Nape
 
Anahitaji ushirikiano wa hali ya juu...lakini kama mambo yenyewe ndiyo kama yalivyotokea Arumeru kazi ipo.
 
Hebu tushirikiane sote ktk hili,lisiwe la viongozi tu mpaka kwa wanachama wote hasa ktk mashina.
 
Sasa mbona NAPE, SIOI mnamn'gang'ania ili hali inasemekana kahonga!
 
Si kweli kuwa viongozi wote ccm wanachukua ama kutoa rushwa, lakini pia si kweli kuwa hakuna hatua za kinidhamu ambazo chama kinawachukulia wale waliothibitika katika sheria kuwa wamekula rushwa, lakini pia hili la kupinga rushwa si kweli kuwa lipo theoretically bali ni practically kwani rushwa CCM imepingwa tangu katika misingi na imani ya Tanu-1954, kisha azimio la arusha-1967 kisha kwenye katiba ya CCM ya mwaka 1977. Lakini tangu hapo wapo viongozi kadhaa ambao walijihusisha na rushwa walichukuliwa hatua na kuwajibishwa kwa namna mbalimbali. Katika CCM si tu kuwa maandiko na kanuni zetu zinatuelekeza kulipinga hili bali tunalidhihirisha hili katika maneno yetu na matendo yetu kama chama.@abdullah, adam george,easther na december...!....Nape

hakuna lolote humo ndani ya ccm (chukua chako mapema) wote ni mafisadi hata huyo.
 
hakuna lolote humo ndani ya ccm (chukua chako mapema) wote ni mafisadi hata huyo.

Pendael hiyo siyo kweli, bado kuna watu wazuri wengi tu ndani ya chama...kinachohitajika ni wao kujitambua na kama gamba basi walivue kama walivyo dhamilia awali.
 
jf bila nape kusema kwl cjui ccm ingekuwa wapi,anajitahdi sama na wala tusimbeze jamani zaidi tumtumie moyo na tzdi kumuombea,ccm itashnda arumeru
 
Kulingana na hali halisi ya mwelekeo wa nchi na maisha ya wananchi(individually) ni wazi kuwa maisha ya watu walio wengi na kundi kubwa yamebadilika, mabadiliko ambayo yanatokana na kuachwa kwa misingi bora iliyoachwa na waasisi wa taifa hili na wapigania uhuru, misingi hiyo ni uzalendo na utaifa.,katika kipindi cha miaka ya nyuma mtu ambaye alionekana kuwa na tabia ya udokozi, wizi na rushwa alikuwa akipingwa na kudharaulika na kuonekana ni mtu mbaya na mwenye kutia doa familia, kaya na jamii husika, tofauti na hali ya sasa ambapo mtu ambaye ni mdokozi, mwizi na fisadi anaonekana ni mwokozi na kimbilio la wenye shida, Anatukuzwa na kupewa "heko" kwa wizi wake, leo hali ilivyo ni kuwa yule anayeiba kiasi kikubwa zaidi cha pesa ndiye anayepewa sifa zaidi na heshima katika jamii yake.,vijana wa sasa wanaita "respect"

katika hali kama hii ambaye mwizi anahesabika ni mtu shujaa na hodari.,kupingana na wizi ama rushwa ni kazi kubwa, ngumu na inayohitaji kujitoa muhanga kwa kiasi kikubwa, na ninaamini kuwa kama jamii yenyewe haitakuwa tayari kubadilika basi nape pekee hatoweza kubadilisha hali hii katika jamii, ni lazima watu wawe tayari kuona maisha tofauti katika jamii yao katika kulishughulikia na kukabiliana na "balaa" hili la ufisadi katika jamii yetu.
 
Nape aweza kuwa mpinga rushwa lakini yuko katika kundi la walarushwa hataweza kuishinda rushwa angalia Arumeru waliohonga zaidi ndiyo hawajakamatwa na PCCB huo ndio mfumo wa chama cha Nape
 
sasa atakuaje mpinga rushwa na wakati yupo katika kundi la watoa rushwa??maana anagekuwa mpinga rushwa angekuwa ameshajiuzuru hapo CCM
 
Back
Top Bottom