KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,139
Mbona unasomeka! Maana sasa hivi hakuna aibu kubwa kama mtu kujitangaza kwamba ni MwanaCCM, unless uwe kiongozi ndio unajikuta huwezi kujificha, sisi wenye akili zetu tumekuelewa Mkuu hatutamwambia mtu kwamba wewe ni Gamba.
Fikra mpauko!ni sawa sawa na kusema mimi kwa kuwa sio mchagga basi lazima nitakuwa mpare!ok bwana endeleeni kujifungia kwenye hivyo vyama vyenu mdumishe fikra za wenyeviti wenu!lakini mimi kujiunga na chama ng'o!na enjoy kuwa independent zaidi na kutoa mawazo yangu kama tax payer!
Nitaendelea kufanya maamuzi yangu kwa kutizama sera za mgombea husika kwa wakati husika, uchaguzi uliopita mfano mwanzo nilipomsikiliza slaa na jakaya kwa kuwa ndio walikua wanajitangaza zaidi niliona sera za slaa zinafaa kuliko jakaya lakini nilipokija kitazama mdahalo wa lipumba itv live pale moven pick nikachange mind kutokana na jinsi lipumba alivyoelezea jinsi atakavyoutendea uchumi wa tanzani,nikaona sera zake zinatekelezeka kirahisi kuliko za jakaya na slaa!
Lakini nyie watu wa vyama kutokana na kujifungia kwenye hivyo vyama sidhani hata kama mliwahi kumsikiliza Lipumba ama mgombea mwingine yeyote tofauti na hao wenyeviti na makatibu wa vyama vyenu, mimi nawaskiliza wote ndio nafanya maamuzi, hiyo ndio advantage ya kuwa na mfumo wa vyama vingi, lengo ni kuwa na choices nyie acheni ubwege, hivyo vyama ni kama makoti tu, ukilichoka unalivua!