commonmwananchi
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 3,377
- 1,952
"KUSHINDWA KWA DHANA YA KUJIVUA GAMBA"
imekuwa ni ndoto na dua ya mafisadi wengi na walafi wa rasilimali za nchi kwa faida ya matumbo yao kuona swala la wao kuwajibishwa kwa usaliti wao linashindwa! Ndo maana wanadhani wanaweza kujidanganya kwa kuimba tu kuwa limekufa.... HUWEZI DHULUMU HAKI ZA WATU NA UKAIMBA TU TENA KWA SHIBE YA KIFISADI KUWA ETI ZOEZI LIMEKUFA... Kama matamanio yote yangekuwa farasi basi kila masikini angepanda ili awe tajiri bahati mbaya sio!
SASA UAMUZI WA NEC ILIYOKETI APRIL MWAKA JANA ILIYORIDHIA MAGEUZI NDANI YA CHAMA( kujivua gamba).. KUHUSU SWALA LA MAADILI ILIAMUA.... VIONGOZI WOTE WANAOTUHUMIWA NA JAMII KWA UFISADI NA RUSHWA, WAPIME NA WACHUKUE HATUA ZA KUWAJIBIKA WENYEWE KWA KUONDOKA KWENYE VIKAO VYA MAAMUZI VYA CHAMA. WASIPOFANYA HIVYO CHAMA KICHUKUE HATUA YA KUWAONDOA BILA KUCHELEWA.
Wakati wa mjadala watu wakatajwa baadhi ya watu wanaotajwa sana na jamii hasa kwenye ngazi za juu kujihusisha na yanayosemwa kuwa ni ufisadi mkubwa ambao leo ukimwamsha Mtanzania yeyote usingizini ukamuuliza hivi matendo gani ya kifisadi unayoyajua makubwa nchini, bila shaka na bila kigugumizi atakwambia, RICHMOND, DOWANS, EPA, RADA nk. Na ukimuuliza kina nani wanahusika atakutajia majina bila kuuma maneno..
Na tukakubaliana KIKAO KINACHOFUATA TUTAFANYA TATHIMINI YA MWITIKIO WA WITO HUO WA WAO WENYEWE KUWAJIBIKA.... WENGINE WAKATAFISIRI SIKU TISINI, TUKAJARIBU KUFAFANUA LAKINI KWASABABU MAFISADI WANAPESA WASIZO NA UCHUNGU NAZO WAKAENDELEA KUPOTOSHA... SI NENO, TUKAKUTANA NOV. TATHIMINI IKASOMWA IKAONEKANA MWITIKIO SIO MZURI, JAPO TULIKIRI WAPO/ YUPO WALIOITIKIA MWITO HUO.
UAMUZI UKAWA SASA TUCHUKUE HATUA YA PILI YA KUWAONDOA KWANI YA KWANZA YA KUWAPA MUDA KUPIMA, NA NILICHUKUA MUDA MREFU KUPIGA KELELE KUTAKA KILA MMOJA ASIKIE ASIJE MTU KUSEMA SIKUSIKIA( nina hakika kwa wanyonge na wachukia ufisadi kelele zangu zilikuwa za kuamsha matumaini, lakini kwa mafisadi, kelele zangu ilikuwa ni kero kubwa ndo maana wanaziita uvuvuzela, am happy for that kwani lengo ilikuwa ni kuwakera pia mafisadi)..
SASA CHAMA KIPO KWENYE MCHAKATO WA HATUA YA PILI, NA JUZI MKITI WA CCM TAIFA, KASEMA " tuliamua jambo hili kwenye kikao na nila manufaa kwa chama, wanaosema ni la hovyo, wao ndio wa hovyo).
Wanaodhani limekufa wanajidanganya... Mafisadi wanajua hawana chao, sasa kama wanawadanganya ni kwasababu wanataka muendelee kuwasindikiza, kama shetani afanyavyo anajua kabisa mwish wake ni motoni lakini anadanganya watu ili aende nao
Nnauye Jr,
Nimefuatilia kwa makini majibu yako kwa leo.Binafsi nakuona mtu usiye na aibu hata kidogo!.na una mapenzi binafsi na chama ccm kuliko wananchi wa nchi hii wanaoumia kutokana na madhara ya ufisadi uliofanywa,na unaoendelea kufanywa na makada waandamizi ndani ya chama chako ccm.(nina uhakika wewe si mmoja wao).
Kama si mapenzi yako kwa ccm,nina imani kwa akili ya kawaida kabisa ungekwisha ondoka na kujiunga na chama kingine na huko ungeendesha mapambano ya dhati kumkomboa mtanzania kutoka katika haya matatizo ya ufisadi,pamoja na kupambana na mafisadi wenyewe
Kwa wigo mpana zaidi.kuliko hivi sasa ambapo saa nyingine tunashuhudia wengine wakikupiga marufuku hata kukanyaga jimboni kwao ili kufanya kazi za chama.(rejea tukio la igunga).
Nasikitika kuona jasho la kijana mzalendo kama wewe unavyojitambulisha likipotea kwa maneno ambayo hata wewe nafikiri saa nyingine unayasema bila kuwa na uhakika nayo.
Kama ndivyo hasa mkuu anachotaka ukiseme,nasema hivyo kwa sababu sijwahi kusikia kauli ya mwenyekiti wako popote pale katika hotuba zake,akitutaka watanzania tukuunge mkono katika vita hii dhidi ya ufisadi katika chama chako na taifa kwa ujumla.
Ebu jaribu kuwa kama yule kijana mwenzako wa ANC,Julius malema kule afrika kusini.maana wote mnapigana vita vya aina moja na tofauti yenu ni kwamba yeye amepata ujasiri wa kuthubutu ambao wewe umeukosa na hakika umeona jinsi umma wa vijana wa ANC walivyo nyuma yake.
Siasa za nchi hii kwa sasa zinahitaji vitendo zaidi kuliko uenezi majukwaani ukiwa umeshikilia kitambaa cha kufutia jasho.mfano halisi unauona kwa vijana wenzio kama kina Mnyika na wengineo wengi wanavyofanya siasa za kisasa kulingana na mahitaji ya wananchi wakiwa na makabrasha yaliyojaa kero za wananchi.bila shaka hata wewe unawakubali katika nafsi yako kama Nape nnauye,na unaweza kuwakataa pale unapokuwa jukwaani kama katibu mwenezi wa ccm
Kwa sasa unachokifanya watanzania tulio wengi tunakukubali,ila pia tunakuhurumia tunapofikiria aina ya watu unaopambana nao,pamoja na idadi yao ndani ya chama chako.kumbuka wengine waliwahi kutamka kwamba "mwenyekiti wako hawakukutana naye barabarani"..wewe hili ualichukuliaje komredi?.nakupa angalizo usije kuwa kama yule katibu mwenezi wa marehemu Saddam hussen wa Iraq (RIP). aliyekuwa akikanusha kipigo cha wamarekani ,walivyokuwa wakizidi kuikaribia Baghdad na hatimae akakoswa kombora la kichwa mbele ya kamera za television, akiendelea kukanusha,na hatimae akakamatwa wa kwanza kabla ya Saddam.
Watu wanakuita vuvuzela kwa sababu pamoja na kero ya ufisadi,ukiwa kama katibu mwenezi wa chama kikubwa kama ccm,mojawapo ya majukumu yako ni pamoja na kuwaeleza watanzania dira ya serikali ya chama chako,katika kutatua kero za wananchi zinazotukabili kwa sasa kama nitakavyoeleza kwa uchache tu.na si kila ukipanda jukwaani,ukihojiwa na press suala linakuwa moja tuuu!
Si wananchi wote hususan vijijini wanaoweza kuyaelewa madhara ya ufisadi moja kwa moja, hii ni nchi kubwa sana ikiwa na wapiga kura wengi sana ambao hata elimu ya uraia bado ni tatizo hivyo wanataka kuelezwa nini hasa dira ya ccm katika kupambana na kero kama rushwa na Wizi wa madawa katika mahospitali ya serikali (baadhi ya hospitali nchini) na kupelekwa maduka binafsi,jambo linalopelekea madaktari walio wengi kugeuka mawakala wa maduka ya binafsi kwa kutuelekeza wagonjwa maduka wanayopendekeza tukanunuwe dawa wanazotuandikia.
Kuna tatizo kubwa la kushuka kwa morali wa utendaji kazi, kwa walimu wetu nchini na ushahidi ni jinsi kiwango cha ufaulu kinavyozidi kuporomoka nchini mwaka hadi mwaka je unafikiri nini kifanyike ili kuokoa nchi na janga hili nyemelezi,
Tunaambiwa kilimo kwanza, na hata bendera ya chama chako ni jembe na nyundo,(ingawa yule kijana pale mwanza katika kipindi asubuhi alitoa hoja kwamba iongezwe na picha ya noti akikueleza maoni yake live star tv)serikali inaanza kununua zana nyingi za kilimo bila kwanza kufanya utafiti na kuleta wataalamu wa kilimo cha umwagiliaji kwanza,kwani tatizo kubwa la mkulima wa tanzania pamoja na uduni wa zana lakini zaidi ni tatizo la uhaba wa mvua.nafikiri na wewe ni shahidi kwa hilo.
Lakini kubwa zaidi nimalizie kwa kukumbusha kuwa ccm na serikali yenu mnatakiwa kudhibityi mfumko wa bei na kushuka thamani ya shilingi,pia mtueleze kwa nini nchi yetu bado inatumia sarafu mbili?
kwa haya machche niliyoyatoa kwako ninaomba walau unijibu ili wananchi wengi tuendelee kukuombea mungu akupe uzima na ufanikiwe katika vita hii kubwauliyonayo mbele yako.
Kila lakheri.