Nape: Jisahihishe, Unapoteza Vijana Wengi CCM

Ndugu mchambuzi,kwa kuzingatia mfululizo wa mabandiko yako hapa jamvini umeonyesha dhahiri unaamini kuwa CCM kama taasisi ya kisiasa imekamilika.Kukamilika huko kunatokana na kuwa hazina ya nyenzo muhimu kama vile Katiba,Miongozo , Kanuni na Taratibu za Chama.Sote tunaelewa kuwa ,CCM, imerithi nyenzo hizo kutoka kutoka kwa mtangulizi wake,TANU.Katiaka maandishi yako, unaamini vile vile, kuwa, taasisi hiyo ina tatizo watu wenye matatizo ya kimaadili katika nafasi na ngazi tofauti .Sasa nini kimetokea kiasi kwamba mienendo ya wanachama imeshindikana kudhibitiwa licha ya uwepo wa katiba,miongozo na kanuni za chama?Je,hii si ashirio la wazi kuwa wanachama wake wa sasa wameshindwa kurithi tabia,silka na hulka za wana TANU wa wakati huo.Katika taaluma za oganaizesheni, tunafahamu kuwa taasisi ama oganaizesheni yoyote hulazimika kupitia hatua tano (5) muhimu katika makuzi yake :huzaliwa ,huanza ukuaji ,kisha hukua kwa kasi (exponential growth),halafu hubaki katika mkuo sawa kwa muda (constant growth)  kabla haijalazimika ''kuchagua'' ama kufa kama itakosa nyenzo za kujiokoa, ama kujiumba upya ikipata nyenzo hizo ili kuepuka kutoweka.Kwa sasa,baadhi yetu tunaamini CCM ipo katika hatua za mwisho wa kifo maama haikui tena kiidadi na kimaadili.Baada ya CCM kufa,halafu sasa nyie mnaoamini katika misingi ya TANU mje mpate nafasi ya kukifufua chama chenu huku mkichukua hadhari ya kutenda makosa ya waandamizi wa sasa.Kwa sasa ,hakuna namna CCM inaweza kujiepusha katika kuuendea mwisho wake.Haiyumkini kuamini vinginevyo.
 
FortJeasus,

Nashukuru sana kwa mchango wako mzuri, hasa swali lako na maoni yako kuhusu masuala ya msingi "sana sana. Naomba univumilie kidogo iwapo majibu yangu yatakuwa marefu. Ningependa kuanza na sehemu ya kwanza ya hoja yako kwamba:

Ndugu mchambuzi,kwa kuzingatia mfululizo wa mabandiko yako hapa jamvini umeonyesha dhahiri unaamini kuwa CCM kama taasisi ya kisiasa imekamilika.Kukamilika huko kunatokana na kuwa hazina ya nyenzo muhimu kama vile Katiba,Miongozo , Kanuni na Taratibu za Chama.Sote tunaelewa kuwa ,CCM, imerithi nyenzo hizo kutoka kutoka kwa mtangulizi wake,TANU.Katiaka maandishi yako, unaamini vile vile, kuwa, taasisi hiyo ina tatizo watu wenye matatizo ya kimaadili katika nafasi na ngazi tofauti .Sasa nini kimetokea kiasi kwamba mienendo ya wanachama imeshindikana kudhibitiwa licha ya uwepo wa katiba,miongozo na kanuni za chama?Je,hii si ashirio la wazi kuwa wanachama wake wa sasa wameshindwa kurithi tabia,silka na hulka za wana TANU wa wakati huo.

Tatizo la mienendo ya viongozi ndani ya CCM sio jambo geni, kwani ni suala ambalo hata Mwalimu Nyerere aliliona ndani ya mwaka mmoja baada ya uhuru. Mwalimu alipata wakati mgumu sana kujaribu kudhibiti tatizo hili, kwa mfano, kwenye TANU na RAIA (1962), mwalimu anasema:
------------
"Wakoloni walipokuwa hapa walipanga mishahara bila ya kujali uwezo wetu kuilipa mishahara hiyo, na bila kuilinganisha mishahara hiyo na mapat ya watu wetu. Lakini wao ilikuwa ni ada yao kufanya hivyo. Serikali ya wageni haiwezi kujali maisha ya raia. Serikali ya ilikuwa ni serikali ya ubwana na ufahari; na walijitimizia ubwana wao na fahari yao, bila ya kujali uwezo wa watu wetu wa kugharamia ubwana huo na fahari hiyo.

Lakini baadhi yetu tulikuwa hatutambui jambo hilo. Waafrika wengi tulikuwa tumekwisha kusahau kwamba mzigo ule wa ubwana na ufahari ni mzito mno na watu wetu hawawezi kuubeba. Kilichokuwa kikituuma ni kwamba ubwana ule na fahari ile wazungu waligawana wenyewe tu, bila kutugawia na sisi pia; baadhi yetu hatukuwa tunadai uhuru ili uwapunguzie watu wetu mzigo huu wa ubwana na ufahari, bali tama yetu ilikuwa ni kukalia viti vile vya ubwana na ufahari. Tamaa yetu haikuwa kushika vyeo tu, vilivyokuwa vimeshikwa na wazungu hapo zamani, tulitaka na mishahara pia iliyokuwa ikifuatana na vyeo bila kujali kama watu wetu wanaweza kulipa mishahara hiyo, na bila kujali maisha ya watu."
--------------

Pamoja na jitihasa hiza, bado viongozi waliendelea kumshinikiza Mwalimu juu ya hili, kwa mfano, makala moja ya Irene and Roland Brown titled "Approach to Rural Mass Poverty" inaelezea kauli za viongozi wa TANU wakimwambia Mwalimu:

-------------
"A Politician", they said, "has no security. Today he is a Minister, Tomorrow he is not, today he is an MP, after five years he is not, (or may be not), today he is a regional or area commissioner, tomorrow he is unemployed, today he is chairman of the region, district, or Town and tomorrow someone else may be elected in his or her place. Why does the Arusha Declaration prevent such leaders from providing by other means, for their future?"

------------
Nyerere Responded:

"In its entirely (Azimio la Arusha), "leaders ask this question more than any other and it is the most serious and dangerous question of all. Personal difficulties of the leaders are interest to the people only to the extent that they might be of such a degree that the leader cannot do his work properly. It is this consideration which causes some leaders to be paid while they carry responsibility. Leaders often forget this, and especially do they tend to forget the purposes of leadership in a socialist Tanzania: it is a good thing if the Arusha Declaration and its leadership requirements act as a constant reminder."
--------

Nyerere went on to Ask:

["Which is the politician who sent to the people at election time and asked them to elect him so that he could provide for his future? Which Area or Regional Commissioner or other TANU worker got his job by saying he wanted to improve his personal position and get security for his future? Whenever a person seeks political work, whether it is through election or by appointment, he says he wants the opportunity to serve the people, to guard their interest and further their aspirations. What right has such a person, once he has the appointment he sought on this basis, use his responsibility for his own betterment? This question is absolutely central to the Arusha Declaration and to the whole purpose of TANU and the independent Tanzania."]
-------

Katika kipindi chote cha utawala wake, Mwalimu alijitahidi sana kuhakikisha viongozi wa TANU wanaongoza kwa kufuata maadili, na TANU ilikuwa na imani nyingi sana kwa mfano "rushwa ni adui wa haki, sitatoa wala kupokea rushwa"; vile vile miaka ya mwisho ya utawala wake alipoona anaelemewa na nguvu, sheria ya uhujumu uchumi ikaletwa na sote tunajua jinsi gani Marehemu Sokoine alivyopambana na tatizo hili hadi kufikiwa na umauti wake. Lengo la juhudu zote hizi ilikuwa kujenga uongozi wenye maadili na wenye commitment kwa wananchi.

Je, hapa tunajifunza nini?
Tunajifunza kwamba itikadi ya Ujamaa chini ya TANU ‘denounced' kwa nguvu zote ukoloni mamboleo, imperialism, capitalism & class exploitation. Lengo kuu la Azimio la Arusha ilikuwa ni kufutilia mbali vitu hivi (kupitia sera ya Ujamaa na kujitegemea) kwani Mwalimu aliona yote haya yalikuwa adui wa Maendeleo.

Sote tunaelewa jinsi wimbi la mabadiliko became inevitable na kuanza kushuhudia Liberalization, Marketization & Privatization, vikisindikizwa na Liberal Democracy vikishika kasi ya ajabu. Tukumbuke kwamba hata mwasisi wa Chadema – Mzee wetu Edwin Mtei alikuwa sehemu muhimu sana ya kuunga mabadiliko haya akishirikiana na World Bank na IMF. Baadae kidogo tukasikia Azimio la Arusha linatupwa kimya kimya, which meant – getting rid of anti – capitalist leadership code, pia mwanzo wa kuporomoka kwa commitment kwa wananchi (bali tycoons na matapeli) miongoni mwa viongozi.

Mageuzi ya kiuchumi na kisiasa yalikuja na madhara mengi kwa CCM, muhimu ikiwa ni pamoja kukauka kwa vyanzo vya fedha (toka serikalini). Since then, vyama vyote vya siasa vimekuwa vikishindana in a "highly monetized political game." Tunashuhudia jinsi gani viongozi wanatumia muda wao mwingi to ‘dine' and ‘wine' na tycoons na matapeli kuliko na wananchi waliowapa dhamana ya uongozi, kwani tycoons na matapeli ndio wenye umuhimu zaidi as they sponsor activity nyingi za viongozi na CCM, including kununua kura wakati wa chaguzi mbalimbali. CCM ambayo awali ilikuwa inajivunia kama chama cha wakulima na wafanyakazi, sasa kimegeuka kuwa chama cha tycoons na matapeli!

Mageuzi haya ya kiuchumi na kisiasa hayana madhara kwa CCM peke yake bali the entire political landscape in the country. Tunashuhudia jinsi gani ushindani wa kisiasa unazidi kuwa mgumu bila ya vyama na viongozi wao kuwa na fedha. Matokeo yake ndio mifarakano kama hii baina ya CCM na Chadema kuhusu fedha za harambee. Lakini ukijaribu kuangalia suala hili kwa jicho la tatu, ni rahisi kubaini kwamba tatizo kumbe sio tycoonization ya vyama kwani both, CCM na Chadema kinaendeshwa na nguvu za tycoons. Tatizo ni wivu na woga kwani mwenye nguvu ya pesa ndiye mshindi katika hii "monetized political game". Both, Chadema na CCM hutokwa na udenda wakisikia chama kingine kimepata fedha kwa sababu: FEDHA is the GATEWAY to MAGOGONI, so kila chama kinatamani kiwe ndicho kinapewa fedha (e.g. suala la Mzee Mustapha Sobodo).

Kwa kumalizia kuhusu swali lako, the political game is already polluted na mageuzi. Suala la fedha na siasa (kujilimbikizia mali, kutumia pesa kupata madaraka n.k), halitaweza kutatuliwa na kanuni na miiko ndani ya katiba ya chama chochote cha siasa Tanzania ya leo. Tukubali tu kwamba "Tycoonization Per Se" sio tatizo kwa Chadema wala CCM; Afterall, hii ni logical consequence of Marketization, Privatization & Liberalization, na vitu vyote hivi CCM na Chadema can't stop falling in love with, without any reservation (100%);

Sehemu ya pili ya hoja yako ningependa kujibu kama ifuatavyo i.e:

Katika taaluma za oganaizesheni, tunafahamu kuwa taasisi ama oganaizesheni yoyote hulazimika kupitia hatua tano (5) muhimu katika makuzi yake :huzaliwa ,huanza ukuaji ,kisha hukua kwa kasi (exponential growth),halafu hubaki katika mkuo sawa kwa muda (constant growth)  kabla haijalazimika ''kuchagua'' ama kufa kama itakosa nyenzo za kujiokoa, ama kujiumba upya ikipata nyenzo hizo ili kuepuka kutoweka.Kwa sasa,baadhi yetu tunaamini CCM ipo katika hatua za mwisho wa kifo maama haikui tena kiidadi na kimaadili.Baada ya CCM kufa,halafu sasa nyie mnaoamini katika misingi ya TANU mje mpate nafasi ya kukifufua chama chenu huku mkichukua hadhari ya kutenda makosa ya waandamizi wa sasa.Kwa sasa ,hakuna namna CCM inaweza kujiepusha katika kuuendea mwisho wake.Haiyumkini kuamini vinginevyo.


Hoja yako kuhusu life cycle ya vyama vyetu vya siasa imenifungua zaidi. Nashukuru sana. Ningependa kulizungumza hilo kwa mtazamo kwamba maisha ya vyama vya siasa barani Africa mimi nadhani yamepitia hatua kuu tatu ambazo ni:

1. Nationalistic Parties (vilivyopigania uhuru) e.g. TANU, KANU, UNIP n.k, na kufanikiwa kuleta uhuru wa kisiasa.
2. Post – independence Parties – vikiongozwa na hivi vya kwanza lakini muda mfupi baadae, nchi nyingi zilifuta mfumo wa vyama vingi kwa justifications mbalimbali na kuleta mfumo wa chama kimoja, mfano Tanganyika (TANU) 1965. Kazi kubwa CCM ilikuwa ni kulinda uhuru wa kisiasa huku ikijaribu kuwapatia wananchi uhuru wa kiuchumi. Tofauti na TANU, vyama vingine vingi barani Africa soon viwaka ‘corrupted' na wakoloni wale wale.
3. Post – Cold War Parties – baada ya kumalizika kwa Cold War, wimbi la mageuzi likaingia katika nchini zote za dunia ya tatu, ikiwepo Tanzania ambapo mfumo wa vyama vingi ukajerea tena hivyo CCM kupata washindani kuanzia 1992.

Sababu kuu kwanini CCM ilifanikiwa kuhimili mikiki mikiki ya mfumo wa vyama vingi nimezijadili sehemu nyingine, mfamo: (https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...tujadili-utayari-wa-kutawala-nchi-2015-a.html).

Ingawa kwa mtazamo wa haraka haraka mtu unaweza kuona CCM imeshafikia hatua ya mwisho ambayo wewe umeielezea ni aidha "kifo" au "to rejuvenate", kifo cha CCM kitachelewa kuja kutokana na ukweli kwamba ushindaniwa kisiasa nchini unakabiliwa na tatizo kubwa sana la "ombwe la itikadi", hivyo kuchangia sana CCM kupona, ingali ikichechemea. Katika mazingira ya Marketization, Liberalization & Privatization, masuala ambayo vyama vyote Tanzania (including CCM) wapo hoi taabani kimapendi na masuala haya, unakuta wote CCM na Chadema wanaongea au advocate sera zile zile tu. Tofauti iliyopo ni kwamba tu wakati CCM wao wapo madarakani wakijitahidi kutekeleza Marketization, Liberalization & Privatization ambavyo ndio chanzo cha ufisadi na utekelekezaji (abandonment) ya wanavijiji, Chadema wao pembeni kuikosoa CCM katika janga hili – CCM inapofanya madudu katika mazingira ya sasa ya Liberal Democracy ambayo ipo under pinned na Marketization, Liberalization & Privatization.

Kwahiyo katika mazingira haya mimi sidhani kama ni jambo la mjadala kwamba sio CCM wala Chadema wenye nia ya dhati, mikakati ya dhati na practical solutions kuwakomboa watanzania wa vijijini (over 70% of the population). Since mid 1980s, what Marketization, Liberalization & Privatization have done to ndugu zetu vijijini and urban poor ni kuzidi kuwa ‘marginalize' na kuwaacha wasijue kesho wataamka vipi. Chadema ni chama kilichoinua matumaini ya watanzania kwa kiasi kikubwa sana, lakini tukubaliane tu kwamba hakina mkakati ulio wazi jinsi gani kitasahihisha mapungufu ya CCM huko vijijini. Vinginevyo ningependa sana kufahamu kama Chama Cha Chadema ambacho (kama CCM) kipo hoi bin taabani kimapenzi na Marketization, Liberalization & Privatization, kitafanya nini kuwakomboa 70% of the population (wanavijiji). Once I am convinced, kesho nachukua kadi ya uanachama na kuanza kushirikiana na Chadema aidha mwanachama, lakini wakiniamini, basi katika nafasi ya uongozi wowote watakaonipa nishirikiane na vijana wengine mahiri ndani ya Chadema, lakini wakiniamini zaidi, basi kuomba ridhaa kuwawakilisha wananchi wa sehemu yoyote ya Tanzania ambako Chama kitaona ninatafaa. Vingineyo ugomvi wangu na Chadema ni huo tu – prosperity ya wanavijiji in the context of Marketization, Liberalization & Privatization.

Pamoja na ukweli kwamba kwa CCM ‘mbele kaburi, nyuma gizai', kwa hali ya sasa, hata Chadema wakishinda uchaguzi 2015, bado tutakuwa hatuna chama chenye itikadi inayowahakikishia wanavijijini their survival and prosperity into the future.

Vinginevyo, mimi sio kwamba nasubiria eti CCM siku moja irejee kwenye TANU. Hilo haliwezekani kwani kuna mengi yamepitwa na wakati (ingawa yapo mengi pia bado mazuri). Tatizo langu ni – sioni mbadala wa kweli kwa mwanakijiji kama nilivyokwisha eleza. Ni vigumu sana kwa CCM kujirekebisha ikiwa madarakani, na jinsi siku zinavyokwenda, chama kinazidi kupoteza mwelekeo. The only way forward ni aidha:
· CCM ivunjike ili kipatikane chama kingine kitacho kuja na itikadi inayosimamia matakwa ya wengi – hasa itikadi yenye uwezo na uthubutu wa kukemea Marketization, Liberalization & Privatization ili mambo haya yawe na manufaa kwa wanavijiji; au
· Chadema, CCK n.k waje na orientation ya namna hiyo.

FortJeasus,
Tupende tusipende, Marketization, Liberalization & Privatization, vitu ambavyo "sweet hearts" wa CCM na Chadema, haviwezi kutatua matatizo ya msingi yanayomkabili mwanakijiji, tofauti na CCM na Chadema wanavyotaka tuamini. Kinachohitajika ili kumkomboa mwanakijiji huyu ni some sort of a radical and a national autonomous programme (development agenda devised and owned by us), tofauti na hali ya sasa ya mapenzi ya kutojitambua na Marketization, Liberalization & Privatization, na kutegemea eti mwanakijiji atainuka kimaisha humo humo. Mwanakijiji hajanyanyuka kimaisha kwa miaka 27 (1985-2012), na hatonyanyuka for the next foreseeable future, huku viongozi wengi wa CCM, Chadema wakizidi kuneemeka (sio viongozi wote kwani watu kama Dr. Slaa, Mwandosya wanaonyesha kuwa na uzalendo mkubwa sana na nchi yao). Pia ni muhimu katika mchakato huu wa kujitambua tena kama taifa (kutafuta a radical and a national autonomous programme), tukaacha maneno ya vitisho kwa wananchi kwamba chama fulani kinataka kurudisha nchi kwenye Ujamaa na upuuzi kama huo, kwani suala hapa sio kurudi kwenye Ujamaa bali kuja na itikadi itakayozaa sera zitakazofanikiwa kurekebisha mapungufu ya Marketization, Liberalization & Privatization yaliyomaliza kabisa matumaini ya mwanakijiji kwa miaka 27 sasa, na badala yake vitu hivi vianze kuwa na manufaa kwa walio wengi.
 
Tatizo CCM si Nape! ni chama kutotoa majibu ya matatizo ya wananchi...

Binafsi sidhani kama kuna Chama chenye majibu juu ya hili, sio CCM wala Chadema hadi sasa - naongelea 70% ya watanzania ambao wapo vijijini; Chadema wanaleta matumaini lakini hawana jibu; nilielezea kwanini nafikiria hivi nilipokuwa namjibu 'Fortjeasus' (rejea post no. 42 ya uzi huu); ila suala hapa halikuwa kuhusu Nape kutokuja na majibu ya matatizo ya wananchi bali baadhi ya kauli zake ambazo zinazokatisha vijana ndani ya CCM tamaa;
 
Na hilo hasa la ku entartain UFISADI ndiyo linatuudhi Watanzania wengi, tunaona bora tujaribu CDM, Hata kama CDM haitakuwa na jingine jipya lakini wakiweza kupigana na UFISADI kwa dhamira ya dhati mimi kwangu CDM litakuwa CHAGUO LENYE MAANA.
 
Na hilo hasa la ku entartain UFISADI ndiyo linatuudhi Watanzania wengi, tunaona bora tujaribu CDM, Hata kama CDM haitakuwa na jingine jipya lakini wakiweza kupigana na UFISADI kwa dhamira ya dhati mimi kwangu CDM litakuwa CHAGUO LENYE MAANA.

Upo sahihi lakini Ufisadi ni zao la Liberalization, Marketization and Privatization; litakuwepo tu hata Chadema ikiingia madarakani, hasa kutokana na deni kubwa la taifa ambapo kwa muda mrefu sana tulishapoteza our social, economic and political power, na hii ni a big threat even to our national security;
 
hujachelewa vua gamba vaa gwanda mnaoonekana kama vijana mliopachikwa bila malengo maalum ila wewe umeshang,amua hilo kabla hujaundiwa zengwe soma maandishi ukutani .
 
hujachelewa vua gamba vaa gwanda mnaoonekana kama vijana mliopachikwa bila malengo maalum ila wewe umeshang,amua hilo kabla hujaundiwa zengwe soma maandishi ukutani .

Sijakusoma hapo kwenye nyekundu; vinginevyo ikiwa Nyerere alitamka CCM sio mama yake na anaweza kuachana nayo, mimi ni nani?

Opereshen ya vua gamba vaa gwanda is still too narrow for me, ingawa ni mwanzo mzuri; ukipata muda soma post yangu no.42 ya huu uzi- majibu yangu kwa 'fortjeasus'
 
Tatizo la NCHI yetu ni UBINAFSI. Tumeweka sana mbele maslahi binafsi na kusahau nchi yetu. Kama viongozi tunakazana kuwaandalia WATOTO wetu maisha ya "kufikirika" katika nchi ya watu masikini sana. Tunapaswa kuangalia maslahi ya NCHI kwanza, halafu CHAMA na mwisho ndio maslahi BINAFSI. Viongozi wetu wamemezwa na ubinafsi kiasi kwamba wanasahau wajibu wao wa msingi kwa NCHI. Wanatugawa kwa misingi ya VYAMA, DINI, UKABILA, UKANDA, ELIMU kwa maslahi binafsi. Nakusihi wewe na wengine kuendelea kukisaidia chama chako katika hay a huku ukiweka mbele masilahi ya nchi YETU. Kwa matokeo yeyote ya 2015 na 2020 kama nchi itahitaji kuwa CCM imara ili iweze kutoa mchango wa kuisaidia nchi yetu. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBAR!
 
Wapi Ritz chama Rejao zomba

Mkuu Mchambuzi hao vijana wa CCM nilitegemea wangekuja hapa jamvini kukusaidia kukijenga chama chenu lakini wapi. Ukitaka kuwapata hawa jamaa Anzisha uzi "Dr. Slaa Afumaniwa' lakini kwa uzi kama aaa huwezi kuwaona. Otherwise uko sahihi mkuu
 
Last edited by a moderator:
Nape ni tatizo kubwa ndani ya ccm ni sample ya uwezo wa chama, chama kimefika hapo kwa sababu uwezo wa mtu sio kigezo tena cha kumpa cheo bali mambo mengine mbali na uwezo wa mtu, haingii akilini kuwa na katibu wa itikkadi wa cha kikubwa kama ccm halafu mtu huyo akawa ni Nape , inavyoonyesha chama kimechoka hebu tizama hata uwezo wa viongozi wa juu wa chama halafu vingozi haohao walinganishe na chama cha upinzani, angalia vile wanavyoweza kuwasilisha mada mbalimbali, ndipo utakavyoweza uelewa jinsi chama kilivyochakaa, nafsini mwao wanadhani wana hati miliki ya kutawala nchi hii na kwa hiyo kuwa na hoja katika mawasiliano na umma kwao sio kitu cha maana, eti wameandiiwa kutawala bila kujali uwezo wao,sikiliza wabunge wao sikiliza wengi wa mawaziri, msikilize waziri mkuu utashangaa
kimsingi hauwezi ukamshangaa nape bila kuhoji uwezo wa wale waliomteuwa
 
Wapi Ritz chama Rejao zomba

Mkuu Mchambuzi hao vijana wa CCM nilitegemea wangekuja hapa jamvini kukusaidia kukijenga chama chenu lakini wapi. Ukitaka kuwapata hawa jamaa Anzisha uzi "Dr. Slaa Afumaniwa' lakini kwa uzi kama aaa huwezi kuwaona. Otherwise uko sahihi mkuu

Albedo;
Nipo vacation muda wa kuwa jamvini JF ni mdogo ila nitajitahidi nimeiona article ya mchambuzi ni ndefu sijapata muda wa kuisoma vizuri, nakuahidi nitaisoma na kama kuna hoja ya msingi nitamjibu, kuna ubaya kujadili uzinifu wa Dr. Slaa? Tunataka viongozi waadilifu.

Chama
Gongo la mboto DSM- in vacation Puerto Vallarta
 
Nape ni tatizo kubwa ndani ya ccm ni sample ya uwezo wa chama, chama kimefika hapo kwa sababu uwezo wa mtu sio kigezo tena cha kumpa cheo bali mambo mengine mbali na uwezo wa mtu, haingii akilini kuwa na katibu wa itikkadi wa cha kikubwa kama ccm halafu mtu huyo akawa ni Nape , inavyoonyesha chama kimechoka hebu tizama hata uwezo wa viongozi wa juu wa chama halafu vingozi haohao walinganishe na chama cha upinzani, angalia vile wanavyoweza kuwasilisha mada mbalimbali, ndipo utakavyoweza uelewa jinsi chama kilivyochakaa, nafsini mwao wanadhani wana hati miliki ya kutawala nchi hii na kwa hiyo kuwa na hoja katika mawasiliano na umma kwao sio kitu cha maana, eti wameandiiwa kutawala bila kujali uwezo wao,sikiliza wabunge wao sikiliza wengi wa mawaziri, msikilize waziri mkuu utashangaa
kimsingi hauwezi ukamshangaa nape bila kuhoji uwezo wa wale waliomteuwa

JAPHETtumpa, nini maoni yako kuhusu hoja za wenzetu hawa juu ya suala hili; nikianza na bobuk, baadhi ya hoja zake ni kama ifuatavyo:

...Jamani Nape amekuwa CAUGHT ON A CROSS ROAD!

….baada ya kuona CCM inapoteza VIJANA wengi na sababau kubwa ni UFISADI, JK M'kti wa CCM akaona njia pekee ya kurudisha trust ya VIJANA kwa CCM, kwanza ni kuwaletea KIJANA mwenzao, lakini sio Kijana tu bali kijana anayechukia UFISADI kwa dhati ya moyo wake. Katika kuangaza katika chama chake ndiyo akamuona Nape Nnauye. kweli JK hakuwa amekosea. Nape bila kujua masikini akifikiri JK ana niya ya dhati ya kupambana na UFISADI na kurudisha trust ya vijana kwa CCM. Kumbe JK alikuwa na na lake jambo (read Mazigaombwe/usanii). Nape bila kujua akaingia kichwa kichwa.

…Sasa katika hatua hii ndiyo Nape amefikia na kama kawaida ya watanzania ameshindwa kufanya maamuzi MAGUMU. Hivyo amebaki vuguvugu, that is ana lazimika sasa kuwatetea MAFISADI na CHAMA chake ilihali ni kinyume na dhamira yake.

Vile vile Lawrence luanda anasema hivi:

"...tatizo CCM si Nape! ni chama kutotoa majibu ya matatizo ya wananchi…

…maisha ya waTZ ndio yanafanya watu waichukie CCM na ili linaitaji CCM ( sio Nape ) kubadilika…

Una maoni gani juu ya masuala haya mkuu. Binafsi nakubaliana na sehemu kubwa ya hoja hizi kwamba the problem ni CCM kama taasisi, lakini the over ridding problem ni viongozi kwani watu/viongozi ndio linchpin ya any organization, bila watu (viongozi), hata kuwepo mabilioni ya dollars na millions of excellent strategies on paper, kama hakuna viongozi wenye vision, uthubutu etc, things won't get better; so for me, tatizo ni viongozi kwani chama sio lolote bila ya watu (viongozi).
 
Inawezekana cdm hawana itikadi inayoeleweka kuhusu ku uplift maisha ya watz wa vijijini ambao ni 70% lakini mimi naamini kama watafanikiwa kutwaa madaraka na wakadhibiti hizi rushwa kubwakubwa na wakawa fair kwenye kugawa hicho kitakachopatikana, basi miundombinu vjijini itajengwa, hospitali zitaboreshwa, elimu pia itaboreka, kilimo kitaboreshwa na mwisho wa siku taratibu maisha ya watz wote hata wa vijijini yataboreka. Naamini kwetu sisi itikadi bora na nzuri ni ile itakayowezesha maisha yetu kuwa mazuri na bora kuliko yalivyo leo.
 
Mchambuzi, nafurahi sana kuona kuwa bado CCM in a vijana wenye mawazo kama yako.

Asante mkuu,

Nia yangu ni kumsaidia kijana mwenzetu Nape lakini iwapo atakuwa na muda wa kukutana na mijadala hii yetu huku site, lakini muhimu zaidi iwapo ataona ina umuhimu kwake; vinginevyo mimi nadhani kitendo cha yeye kutulia na kusoma mawazo ya wengi humu kila anapopata nafasi and take notes za hapa na pale, Nape atarudi kuwa yule kiongozi wetu wa UVCCM. Pia atakuwa in a better position kurudisha mvuto wa CCM kwa vijana kwa mbinu beyond confrontation na Chadema. Ni muhimu Nape akaanza kuzungumza na Vijana (sio UVCCM), Vijana wenzake waliotapakaa nchin nzima. Kila statement yake, press conference yake ahakikishe inakuwa na that tonality. Ajue kwamba Chadema wanagundua yafuatayo na wanayafanyia kazi:

Vijana Tanzania wanaishi under all sorts of misfortunes. Wao ndio wengi in terms of idadi ya watu, lakini ni wao pia who also carry most of the social burdens. Inahuzunisha if we further think that this large group of the population is the very same that will form the future of our country.

Historia ya nchi yetu imetufundisha kuhusu nguvu ya vijana hasa the prominent positive role that organized youths can play kwenye jamii. Kwa mfano, enzi za TANU,vijana played a prominent role in the political resistance and the struggle against the colonial rule. Kuna mifano mingine mingi kama Majimaji resistance in the 1920s in Songea (hawa walikuwa wengi ni vijana), to students' uprising at UDSM (Mlimani) in the 1970s, 1980s, 1990s, and more recently katika vyuo vikuu vingi nchini. Matukio yote haya underscore the centrality of the position of youths in the struggle for change. M4C ya chadema lazima tukubali tumepigwa bao; na badala ya kuja na mikakati ya kuwa na kitu kama hiki na sisi, tunakimbilia kukosoa the movement kwa hoja za ovyo kabisa; vyama vya siasa hata katika nchi zilizofanikiwa kimaendeleo na kidemokrasia always vinafanya kazi kama hii ya Chadema ingawa in different ways. Clinton, Obama, Blair, wote walitokana na project kama hii ya M4C. Hata Rais wetu JK, kwenye ngazi ya chama, kulikuwa na movement kama hii 1995, lakini ikaja kuzaa matunda 2005;

Sijui kwanini tunakataa kwamba vijana wengi wa kitanzania leo live in despair and hopelessness na hawana matumaini tena. They face uncertainty in terms educational, employment, and other opportunities (social, economic and political). Kwa wengi ya vijana hawa, maisha wanayoishi wazazi wao are humiliating. Yote hii inatokea in the context of poverty and crime; vijana wengi end up becoming criminals, drug users and prostitutes as a way of drowning their frustrations na pia earning their daily bread. Na yote haya yametokea chini ya CCM.

Ndio maana sio ajabu kuona masses of young people in the country are increasingly aligning themselves with CHADEMA, na kwa wengi, kimegeuka kuwa chombo chao to express their dissidence with the CCM government. Organized by youth leaders ndani ya CHADEMA, who are in turn increasingly getting support hata kutoka kwa wazee, vijana Tanzania are becoming significant agents of social transformation, and they are in the verge of making history as we see it unfolding before our eyes.

Lakini haina maana kwamba CCM haina nafasi tena kwenye mioyo ya vijana wa nchi yetu, nafasi hiyo bado ipo lakini itajitokeza pale tu viongozi wetu wa CCM wakikubaliana na uhalisia huo hapo juu na kuamua kkufanyia kazi kwa dhati;
 
Inawezekana cdm hawana itikadi inayoeleweka kuhusu ku uplift maisha ya watz wa vijijini ambao ni 70% lakini mimi naamini kama watafanikiwa kutwaa madaraka na wakadhibiti hizi rushwa kubwakubwa na wakawa fair kwenye kugawa hicho kitakachopatikana, basi miundombinu vjijini itajengwa, hospitali zitaboreshwa, elimu pia itaboreka, kilimo kitaboreshwa na mwisho wa siku taratibu maisha ya watz wote hata wa vijijini yataboreka. Naamini kwetu sisi itikadi bora na nzuri ni ile itakayowezesha maisha yetu kuwa mazuri na bora kuliko yalivyo leo.

Sawasawa. Na chama kitakachoweza to communicate hii statement yako in red - in ideological terms na kuanza kufanyia kazi hata kama ni kwa asilimia moja kwa mwaka, hicho ndicho chama kitakachofanikiwa kutawala Tanzania kwa muda mrefu sana. Lakini unaposema maisha yetu - tunaongelea watanzania zaidi ya milioni 30 ambao wapo vijijini;
 
Uko sahihi sana mkuu! What i know ni kwamba Nape amesoma Political Science, sasa sijui anachofanya sasa ni siasa ambazo mimi hata simwelewi.

The issue of today sio propaganda ni kuadmit failure then choose the right approach ili kurejesha mvuto wa chama unaotoweka kwa kasi mithiri ya rocket iendayo sayari ya mars! Siku za nyuma ccm ilikuwa imewekeza sana kwa vijana na hivyo kuwa na mtaji wa kudumu na ndio hao watu wazima wachache wanaoishilia.

Kama Nape angesimamia mambo haya 4 angekuwa kijana wa kipekee!
1. Serikali kuwa wazi kwenye mambo ya msingi kwa maendeleo ya taifa, mfano mikataba inayoingia na wawekezaji kama madini n.k.
2. Serikali kutumia kwa umakini mapato ya ndani yanayotokana na kodi za ndani na kuepuka matumizi makubwa ya fedha za kukopa.
3. Viongozi kuishi maisha yatakayo reflect uhalisia wa uchumi wa mtanzania na siyo kukopy na kupaste lifestyle za viongozi wa Bahrain, Brunei au Abu Dhabi.
4. Kuchukua hatua kali kwa viongozi wanao hujumu uchumi wa nchi kwa kuiba na kufuja mali za umma na kujilimbikizia mali

Nape ni reflecting mirror ya uongozi wenu. Hawezi kuleta mabadiliko yoyote kwa sababu anatumiwa na wanaomtumia kama toilet paper.
Dawa ya kunusuru ccm leo ni kuwapiga chini viongozi wote kuanzia mwenyekiti wa taifa kuja chini. Zaidi ya hapo subirini muone anguko lenu wana ccm. Mpende msipende. Mkilazimisha kukaa tutalazimisha muondoke na mnajua nini itakuwa matokeo. Thanks kwa kunielewa.
 
Nape ni reflecting mirror ya uongozi wenu. Hawezi kuleta mabadiliko yoyote kwa sababu anatumiwa na wanaomtumia kama toilet paper.
Dawa ya kunusuru ccm leo ni kuwapiga chini viongozi wote kuanzia mwenyekiti wa taifa kuja chini. Zaidi ya hapo subirini muone anguko lenu wana ccm. Mpende msipende. Mkilazimisha kukaa tutalazimisha muondoke na mnajua nini itakuwa matokeo. Thanks kwa kunielewa.

Kuna vitu ambavyo nadhani ni muhimu niviweke sawa. Nape sio kiongozi peke yake ndani ya CCM ambae ni kijana (bearing in mind kwamba vijana ndio chachu ya mabadiliko), kwani wapo wengine kadhaa, lakini yeye ndiye alikuwa tumaini la wengi kwa sababu zilizo wazi, na bado anaendeleo kuwa tumaini la wengi hata hivi tunapozungumza, ndio maana uzi huu unapata maoni mengi. Huko nyuma niliwahi kuandika makala kwamba hatumtendei haki Nape na nilieleza kwa kirefu sana kwanini yeye mwenyewe hawezi kuleta mabadiliko ndani ya CCM. Katika uzi huu ambao tunaujadili leo, msimamo wangu kwa hili haujabadilika. Katika uzi huu, ninacholenga mimi:

  • Ni vitu ambavyo vipo ndani ya uwezo wake, kwa mfano baadhi ya kauli zake ambazo sina uhakika kama huwa anakaa na washauri wake na kuzijadili kabla ya kuzitoa; ni baadhi ya kauli hizi ndiz zinaleta madhara makubwa sana kwa vijana 'site'. Hilo ni moja.


  • Pili, ni suala la chama kukosa mwelekeo wakati yeye ndiye anayesimamia idara inayojihusisha na suala zima la itikadi, siasa, uenezi, na sera.

Vinginevyo suala la Nape na mapambano ya ufisadi, sijui nyinyi, lakini mimi kwa kweli naona kwa hilo tunamwonea kwani amejitahidi kwa nafasi yake na sioni anaweza kufanya nini zaidi ya aidha kujiuzulu kwa kushindwa kitu alichosimamia au kuendelea na mikakati mingine kichama kukabiliana na hilo, ambayo huku site sisi hatuijui.

Sijui nyinyi, lakini mimi sidhani kama ni sahihi kupima utendaji wa Nape kwa kigezo cha mafanikio ya vita vyake dhidi ya ufisadi; kwanza ni kukubali kwamba je, yeye ni tegemeo letu pekee ndani ya CCM au hapana; kama tunakubali kwamba ni ndio, wengi wameshaelewa msimamo wake dhidi ya ufisadi na tukubali ukweli kwamba ndani ya CCM, hakuna kiongozi mwingine aliyejitoa mhanga hivi kwa hilo, ni kwamba tu wengi wetu tunapenda kuchukulia mambo kirahisi sana; so kazi yake juu ya ufisadi tuiweke pembeni angalau kwa sasa, kwani kwenye hilo, ana marks nyingi kutoka kwa vijana, ni wakuu wake tu wamuunge mkono (Lakini muhimu hapa asisahau uwepo wa azimio la Zanzibar)!; tugeukie vigezo vingine vinavyoendana na idara yake, huku tukiangalia kwa ukaribu kauli zake na matendo yake, je ni za kujenga au kobomoa in the ears of vijana wa Tanzania wanaozidi kukata tamaa na CCM? Kumbuka, haya ni masuala yaliyopo ndani ya uwezo wake, so tumpime kama mkuu wa kitengo ambacho ni roho ya chama (CCM), na tupime jitiada zake za kuvuta au kufukuza roho ya nchi - vijana. Katika hili mimi nadhani ameanza kupwaya.
 
JAPHETtumpa, nini maoni yako kuhusu hoja za wenzetu hawa juu ya suala hili; nikianza na bobuk, baadhi ya hoja zake ni kama ifuatavyo:



Vile vile Lawrence luanda anasema hivi:



Una maoni gani juu ya masuala haya mkuu. Binafsi nakubaliana na sehemu kubwa ya hoja hizi kwamba the problem ni CCM kama taasisi, lakini the over ridding problem ni viongozi kwani watu/viongozi ndio linchpin ya any organization, bila watu (viongozi), hata kuwepo mabilioni ya dollars na millions of excellent strategies on paper, kama hakuna viongozi wenye vision, uthubutu etc, things won't get better; so for me, tatizo ni viongozi kwani chama sio lolote bila ya watu (viongozi).
upo sahihi viongozi ni kila kitu taasisi yeyote hutengenezwa na watu, namna gani vingozi wanapatikana ni kitu muhimu sana. shida ni mmoja ndani ya chama tawala ili uwe kiongozi inabidi ama utumie fedha au uwe ni mtoto wa aliyewahi kuwa kiongozi wa juu ndani ya chama kama sio hivyo uwe umekubali kutumikia matakwa ya watu fulani lakini kamwe sio uwezo wa mtu
hapo ndipo unapowapata kina mukama kina nape na wengine, unaweza kuona ccm haijakosa watu makini wa kuwa viongozi shida ni kwa watu hawa wazuri hawawezi kupenya nguvu za watu wanaolinda maslahi yao kwa nguvu zote, kitu ambacho kinaweza kupambana na watu hawa ni nguvu ya umma peke yake sio wanaccm wenzao
 
upo sahihi viongozi ni kila kitu taasisi yeyote hutengenezwa na watu, namna gani vingozi wanapatikana ni kitu muhimu sana. shida ni mmoja ndani ya chama tawala ili uwe kiongozi inabidi ama utumie fedha au uwe ni mtoto wa aliyewahi kuwa kiongozi wa juu ndani ya chama kama sio hivyo uwe umekubali kutumikia matakwa ya watu fulani lakini kamwe sio uwezo wa mtu
hapo ndipo unapowapata kina mukama kina nape na wengine, unaweza kuona ccm haijakosa watu makini wa kuwa viongozi shida ni kwa watu hawa wazuri hawawezi kupenya nguvu za watu wanaolinda maslahi yao kwa nguvu zote, kitu ambacho kinaweza kupambana na watu hawa ni nguvu ya umma peke yake sio wanaccm wenzao

Kuhusu suala la uongozi, kweli CCM ina tatizo kwani chama kinaegemea zaidi on LEADERSHIP SUCCESSION badala ya RECRUITMENT OF LEADERS. Leadership succession ni hali ya watu kupewa madaraka kwa sababu baba alifanya kazi na mkubwa huyu au yule, au kupata madaraka kwa kujikomba (upambe); in the long run, hii huleta matatizo ya kiuongozi na kiutendaji. Recruitment of leaders ni kitu ambacho mwalimu alijaribu sana kukijenga.

Leadership recruitment inafuata mchakato wa ‘identification', ‘nurturing', ‘education' and ‘training', hasa vijana. Kunakuwepo mazingira ambayo ni enabling na vile vile kunakuwepo taasisi ambazo zinatoa a guidance jinsi gani mchakato huu ufanyike – rules, principles, codes of conduct ambazo zinasaidia system to identify potential leaders, attract them, nurture them, traine them etc. Uwepo wa such an enabling environment inavuta kwa urahisi sana attracts young independent individuals wenye talent, elimu, and well informed, na wenye uwezo wa kuja na vision au ideas mbalimbali zenye kuweza kusogeza taifa mbele kimaendeleo/kwa faida ya wengi. Na sio lazima vijana wa namna hii wawe wanasiasa au wanachama kutoka chama fulani, hawa wanaweza kuwa just ordinary citizens ambao mazingira yaliyopo yanawapa hamasa ya kujihusisha na masuala ya umma kwa ujumla.

CCM ingeendelea kuwekeza katika hili i.e. kuwa na such an enabling environment, ingefanikiwa sana kuvuta talents, skills, enthusiasm na experience kutoka kwa vijana wengi sana. Mazingira haya yangejenga a pool of resources for CCM ambapo vijana mbalimbali wangeweza kutumika kwa ajili ya sasa na baadae. In return, hata vijana wengine kwenye jamii wangehisi kwamba kumbe fursa zipo kwa kijana yoyote mwenye kuweka bidii na mwenye ku sustain tabia ya uadilifu. Kwa bahati mbaya CCM haina muundo wa namna hii, na mbaya zaidi, hakuna mchakato au ushindani wa kupata viongozi haupo fair, open wala transparent. Kinachotokea sasahivi ni kwamba kama baba au mama ana ukaribu na mkubwa, hata ukiangushwa kura za maoni za udiwani au ubunge na ukawa wa tano, utabebwa tu. Ndio maana vijana wengi wanakimbilia chadema, na wengi zaidi wataenda huko uchaguzi wa 2015.
 
Back
Top Bottom