Nape haifahamu katiba ya CCM?

(Lakini inajulikana wazi kuwa CC ilijiuzulu ili kumpisha mwenyekiti aiunde upya, baada ya lawama kwamba haikuwajibika vema kuleta ushindi wa kishindo mwaka 2010. Ilitokana pia na lawama za wanachama na baadhi ya viongozi dhidi ya katibu mkuu aliyekuwapo, Yusuph Makamba na sekretarieti yake.)


Inajulikana na nani???????
 
(Lakini inajulikana wazi kuwa CC ilijiuzulu ili kumpisha mwenyekiti aiunde upya, baada ya lawama kwamba haikuwajibika vema kuleta ushindi wa kishindo mwaka 2010. Ilitokana pia na lawama za wanachama na baadhi ya viongozi dhidi ya katibu mkuu aliyekuwapo, Yusuph Makamba na sekretarieti yake.)


Inajulikana na nani???????
Mkuu Nape heshima Mbele! Kwanza ningependa vijana wenzangu tuwe na staha tunapojadiliana na viongozi wa kitaifa humu.kama huna hoja usiandike chochote tu tena yasiyo na staha.pili hiyo makala mwandishi amebeba kila kitu kutoka humu kwenye thread aliyoanzisha Mchambuzi ambaye hata yeye amekiri takwimu za asilimia 40 na 60 alikisia tu.nategemea Mchambuzi atakuja kusimamia hoja zake kwakuwa umejitokeza.mwisho nakuunga mkono vita ya ufisadi na umejaribu
 
(Lakini yote hiyo imetokana na kuelemewa kwa hoja kutoka kwa vijana wenzake. Alitumia asilimia karibu 60 za muda wote kujitetea, na nyingine 40 kushambulia wenzake, badala ya kujenga hoja.)

Kipimo chako ni kipi katika hili?... Kulikuwa na shule a msingi ilikuwa na vijana wawili wa darasa la saba wakafaulu wote wawili ikawa asilimia mia moja, na shule ikawa ya kwanza kwa kufaulisha. Wakati kuna shule zimekuwa na vijana zaidi ya mia moja na wamefaulu zaidi ya tisini lakini hazikuwa za kwanza..
NINI BASE YA ASILIMIA ZAKO?
 
Pia mkuu kwenye vita ya ufisadi tuweke itikadi pembeni ungana na Chadema kama hatua ya kizalendo kuikomboa nchi yetu.CCM imeoza na inaweza kukugharimu kwa kujaribu kwako.kubali mkuu hali ni mbaya na makundi yamejaa
 
(Na wakati akifanya hivyo, wenzake walikuwa wakijenga hoja kwa kutumia matukio ya kweli yanayofahamika. Alishindwa hata kukubaliana na wenzake juu ya ubovu wa katiba iliyopo katika vipengele kadhaa, ili apate pa kuanzia kujenga hoja yake.)..

Unaweza kutoa mifano hata miwili ya hizo hoja ambazo wenzangu walijenga kwa mifano inayofahamika nami nikashindwa?? Nina mashaka kama uliangalia mazunguzmo yale au ulisimuliwa tu, eti nilishindwa kukubaliana na wenzangu juu ya ubovu wa katiba iliyopo! Hivi nini maana ya kwenda kuzungumza??? Kuna hoja tumekubaliana wote, kuna hoja mwenzetu mmoja alipinga, na mwingine na mpaka mjadala umeisha, then hata watazamaji waliusifu mjadala ulikuwa mzuri na wamanufaa kwao! Pengine ukitoa mifano ntakujibu mmoja baada ya mwingine
 
Pia mkuu kwenye vita ya ufisadi tuweke itikadi pembeni ungana na Chadema kama hatua ya kizalendo kuikomboa nchi yetu.CCM imeoza na inaweza kukugharimu kwa kujaribu kwako.kubali mkuu hali ni mbaya na makundi yamejaa

Nakubaliana na wewe kuweka itikadi pembeni kwani ufisadi hauna itikadi, lakini unaposema hivyo na wakati huohuo unaniamnia niahamie cdm maana yake umetolea itikadi kwa mkono mmoja na kuurudisha kwa mkono wa pili.h
 
''nina abudu sehemu fulani kwasababu niliwakuta wazazi wangu wana abudu hapo,lakini ningeweza kupewa nafasi ya kuchagua pa kuabudu ningechagua pale napopataka na kupaelewa mimi'' . tusimlaumu sana mi nafikiri tatizo ni hilo
 
yaani haya majibu ndio unayoyatoa sijaridhika na jibu hata moja hapa ni bora ungenyama kimya...
 
CCM imekosa mvuto kwa kushinswa kufanya maamuzi magumu ya kunusuru taswira ya chama kwa wapiga kura.
 
(Kwanza, alikiri kwamba vita ya ufisadi nchini illibuliwa na CHADEMA. Kwa mantiki hiyo, CCM haiwezi kujidai kwa kupiga vita ufisadi, kwa sababu jukumu kubwa ililo nalo ni kujitetea dhidi ya tuhuma za ufisadi ndani yake.)

..... Pengine tumepotoshwa sana katika vita hii ya ufisadi. Tukiwa wa kweli vita hii ilianza rasimi nchini wakati wa Azimio la Arusha na kusimamiwa sana na Marehemu Sokoine, ambao wote Sokoine na Azimio la Arusha ni kazi nzuri ya TANU na baadae CCM. KWA HOJA hii pekeake ukiacha zingine nyingi si kweli kwamba vita hii ya ufiasdi ilianzishwa na Chadema nchini, ilianza toka enzi za WAHUJUMU UCHUMI. kwa kuyajua haya SIWEZI KUSEMA KAMA MTOA HOJA ANAVYODAI, ETI NIMEKIRI KWAMBA VITA HII ILIANZISHWA NA CDM.

kwa hiyo wizi mmeanza zamani? Na bado mnadumisha
 
Sasa nimeelewa maana ya kupoteza dira. Hivi Sokoine alikufa? Alikufaje? Na kolimba je? Mbona wanaopinga wahujumu wanatoweka haraka? Masikini CCM.
 
Nakubaliana na wewe kuweka itikadi pembeni kwani ufisadi hauna itikadi, lakini unaposema hivyo na wakati huohuo unaniamnia niahamie cdm maana yake umetolea itikadi kwa mkono mmoja na kuurudisha kwa mkono wa pili.h
Hapana mkuu sijamaanisha uje Chadema bali ufisadi usipiganwe kiccm au kichadema bali kwa sura ya maslahi ya taifa.mfano tunaposema Chenge ashtakiwe kwaajili ya issue ya radar hata wewe unapaswa kusema wazi kuwa kweli wafikishwe mahakamani(hayo ya kuvuana uanachama si sehemu ya uwajibikaji kisheria!).nakusifu kwa kujaribu kusema waliyoshindwa hata wazee wa chama lakini wanapaswa kuona hutanii kwa jinsi utavyojenga hoja na kushauri serikali ichukue hatua kali na haraka! Ushahidi uph unahitajika ktk issue za Richmond,EPA? Kuwa wazi kwa dhati kuwa sheria ichukue mkondo otherwise waachie chama njoo mtaani una masters wewe!
 
(Kwanza, alikiri kwamba vita ya ufisadi nchini illibuliwa na CHADEMA. Kwa mantiki hiyo, CCM haiwezi kujidai kwa kupiga vita ufisadi, kwa sababu jukumu kubwa ililo nalo ni kujitetea dhidi ya tuhuma za ufisadi ndani yake.)

..... Pengine tumepotoshwa sana katika vita hii ya ufisadi. Tukiwa wa kweli vita hii ilianza rasimi nchini wakati wa Azimio la Arusha na kusimamiwa sana na Marehemu Sokoine, ambao wote Sokoine na Azimio la Arusha ni kazi nzuri ya TANU na baadae CCM. KWA HOJA hii pekeake ukiacha zingine nyingi si kweli kwamba vita hii ya ufiasdi ilianzishwa na Chadema nchini, ilianza toka enzi za WAHUJUMU UCHUMI. kwa kuyajua haya SIWEZI KUSEMA KAMA MTOA HOJA ANAVYODAI, ETI NIMEKIRI KWAMBA VITA HII ILIANZISHWA NA CDM.

Baba wa taifa alisema "chama kinanuka......"
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom