NAPE: Dk. Slaa ameikimbia Mwanza mapema

Chezeni michezo yenu yote wananchi tunasubiri 2015. ndiyo hapo Nape atajua ushindi wa kishindo ni kitu gani, wakichakachua kama kawaida yao tunawachakachua pia
 
Nape ana akili Kama za nyumbu beside that Nape kujichubua ana maanisha nini ?
 
hivi mwanza hakuna TAKUKURU iwachunguze madiwani wa cuf walioipigia kura ccm? Najua lazima magamba
walizunguka mbuyu! mkono mtupu haulambwi
 
CCM hawajui watendalo wakihonga madiwani watatu au wanne leo ikifika uchaguzi ujao maanake wameeongeza hasira kwa wananchi ina maana waongeze madiwani zaidi wa cdm kwani hasira za wananchi kwa ccm ni rushwa na kutotekeleza matakwa ya wananchi ...cdm nna ccm wote ni watz ila tabia ya chama

dawa za vvu wamechakachuwa kura wanachakachuwa.....mfano wamesema wamefukuza wakurugenzi wabadirifu kumbe uwongo wengi wao wamepangiwa kazi kubwa zaidi kwenye mikoa mipya mfano ded katolewa chato kapeleka simiyu kufa afisa mipango mkoa
 
Nape unatupa shida Watanzania kuwa na kiongozi kitaifa wa chama kilichoshika hatamu badala ya kupambana na changamoto mbalimbali zinazosababisha umaskini kwa Mtanzania. Watanzania Tunafahamu kuwa Slaa siyo chanzo cha ufisadi, EPA, kutowajibika kwa viongozi wabadirifu na matatizo lukuki yanawasumbua watanzania. Ikiwa unamlaumu na kumtukana mtu asiye hata na serikali wala hakusanyi kodi ukijua kabisa hahusiki na matatizo yaliyopo tuna wasiwasi kama unafahamu chanzo cha matatizo tuliyonayo. Unamlaumu akiwa haongozi serikali je, siku akiwa anaongoza serikali utafanyaje? Ikiwa vijana wana uwezo mdogo kama wako nafuu tuongozwe na wazee wenye miaka 90.
 
Mimi nilikua nasubiri heading ya thread kama cdm ingeshinda. Mtaalamu Molemo angetuletea ya uhakika.
 
CDM ni maafa kanda ya ziwa, pongezi zipokeeni wana Nyamagana kwa kugundua udhaifu wa chama kilijichokita kwenye misingi ya ukanda na ubabe

Mkuu unawaita hao 11 waliopiga kura wananchi wa Nyamagana! Ni kuwadhalilisha na kutowatendea haki wakazi wa Nyamagana mie nikiwa mmoja wapo. Kumbuka Nyamagana kuna watu waelewa sana kuliko unavyofahamu wewe katika kutafsiri tukio hili, fuatilia utagundua
 
Mimi ninge mshauri nape na wana ccm wenzake,ambao wana shika nyadhifa mbali mbali,waache majungu na fitna,na hivyo ndivyo vitakavyo wamaliza,nape kama kiongo anatakiwa atekeleze ilani ya chama chake,au inawezekana ilani ya chama chake ni majungu na fitna.
 

Friday, September 28, 2012


*Asema Dk. Slaa ameikimbia Mwanza mapema baada ya kunusa Chadema kugaragazwa

*Awapongeza madiwani wa CCM wa Nyamagana kwa kuwezesha ushindi wa Menya na Naibu Meya Nyamagana

NA MWANDISHI WETU, MWANZA

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, amesema dalili za kubwagwa kwa CHADEMA ndizo zilizomkimbiza mapema jijini Mwanza, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willbroard Slaa.

Amesema kushindwa kwa Chadema katika kinyang'anyiro cha Meya na Naibu Meya, ni mavuno ya ubabe wa viongozi wa chama hicho ambao baadhi wanazeeka vibaya.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa, Nape (pichani) alisema kwamba, Slaa alikimbia baada ya kuona maji yamezidi unga.

Nape aliyetumia fursa hiyo pia kuwapongeza Madiwani wa CCM wa wilaya ya Nyamagana na Chama kwa ushindi wa Viti vya Meya na Naibu wake, alisema Dk. Slaa anazeeka viba ndiyo maana naongoza chama hicho kwa ubabe na maandamano ya kila mara.

"Babu (akiwa na maana ya Dk Slaa) alisema CCM Mwanza itaondoka madarakani, imejidhihirisha wazi katika uchaguzi wa leo kuwa CCM bado ina nguvu na ni Chama kikongwe kisiasa, vingine vinaiga."

"Chadema wameona mavuno ya ubabe wao japo kura za CCM ni ndogo…., Babu ajiulize kwa nini ameshindwa kwenye uchaguzi huo wa Meya na Naibu Meya." Alisem Nape na kuongeza kwamba, kutokana na dalili za kushindwa zilizoonekana mapema, ndiyo maana Dk Slaa alikimbia Mwanza mapema.

Akiwapongeza madiwani hao kwa ushindi alisema kwamba wamefanya kazi kubwa na ya ziada kuhakikisha CCM inarejesha Halmashauri ya jiji hilo mikononi mwake baada ya kushikwa na Chadema kwa kipindi kifupi na hivyo kuwataka wana Mwanza wawe na mshikamano na kuwapa ushirikiano viuongozi wao.

"Nawasihi wananchi wa Mwanza wawe na mshikamano na kuacha maandamano yasiyokuwa na msingi, badala yake wafanye maandeleo, waimamini CCM sasa inachokuja kufanya ni cha uhakika." Alieleza Nape.


POSTED BY: BASHIR NKOROMO AT FRIDAY, SEPTEMBER 28,







Ndugu yangu Nape ujiulize ushindi huo una maana gani kwako hasa ukiangalia cahama chako kilivyokuwa na mikashfa ya kukumbatia mafisadi, ningeona unafanya furaha nzuri kaama falsafa yenu ya kuvua gamba ingefanikiwa walau hata kwa asilimia 0.5. Hapo hatuchezi ligi ili bingwa apate kombe bali ni vipi tunaweza kuwahudumia wananchi kwa fursa za kiuongozi tunazopewa.
 
Idadi ya madiwani iko wazi, Hapa pongezi wape wale madiwani waliosaliti chadema na kufukuzwa na kufanya idadi ya ccm na cuf kuongoza.Ila cha msingi ni kwamba cdm ni chama pekee kinachofanya maamuzi magumu, tuko tayari kupoteza hata jimbo zima kuliko kuwa na viongozi mamluki ndani ya chama chetu makini.Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Nbimependa comment yako, I feel the same way
 
Ni mchezo mchafu wa ccm ndo umewapa ushindi.madiwan wa viti maalum wa ilemela wakapiga kura kumchagua meya wa nyamagana.we uliona wapi kama siyo uhuni.cuf nao wameendeleza usaliti kwa upinzani kwa kuwapa ccm kura.ngoja 2one kibaraka wa lowassa atafanya nini!
 
Mkuu wa MKOA wa MWANZA ndie alieyeanza kuwapa hongo MADIWANI WA CHADEMA wa Kuchaguliwa ili

Wabadilishe kura zao kuchagua Mwana CCM as MAYOR... na tatizo walilonalo CHADEMA Mwanza na ILEMELA

Una uhakika na unachokiongea.....Chagulani ndie aliekuwa anakubalika hata kwa madiwani wa cuf....baada ya kupigwa chini cuf wakaona chadema hamna kitu msimamo wao ukawa bora CCM.....!
 
Idadi ya madiwani iko wazi,
Hapa pongezi wape wale madiwani waliosaliti chadema na kufukuzwa na kufanya idadi ya ccm na cuf kuongoza.
Ila cha msingi ni kwamba cdm ni chama pekee kinachofanya maamuzi magumu, tuko tayari kupoteza hata jimbo zima kuliko kuwa na viongozi mamluki ndani ya chama chetu makini.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Hata kama hao madiwani waliofukuzwa wangekuwepo bado ushindi wa chadema ulikuwa unategemea madiwani wa cuf.....chagulani ndio wa nyamagana,mashaka ni wa ilemela....bado ingekuwa chadema 9 ccm 9 na cuf 2!
 
CDM ni maafa kanda ya ziwa, pongezi zipokeeni wana Nyamagana kwa kugundua udhaifu wa chama kilijichokita kwenye misingi ya ukanda na ubabe

Huyu nae matatizo ni yale yale ya ugonjwa wa akili na matatizo ya kusoma sasa maafa unayosema hapa ni maafa gani na hao wana Nyamagana unaowapongeza wamefanya nini?Kumbuka madiwani madiwani narudia rudia ili uelewe na ushindi wenyewe ulikuwa wa umafia iweje Nepi ahamishie madiwani/wabunge wa viti maalumu kutoka Ilemela kuja Nyamagana?Hebu fikiria kwanza acha ushabiki usio wa maana na unaposema ukanda sikulaaumu kwani ndivyo mlivyoaminishwa ndio maana kila leo shida haziwatoki kwa kuaamnini ati ccm itawapa maisha bora kumbuka kama wewe unakijibarua lakini 99.9%ya familia yako wanasafa Lol!!pole kwa kushobokea Magamba
 
porojo zingine sasa kama mlikuwa mnayajua hayo kwa nini dr slaa alienda mwanza.

jiji la mwanza limegawanywa sehemu mbili yaani nyamagana na ilemela lengo ni ccm kupata nyamagana....hivyo dokta alienda kufanya taratibu za kuwapata na kuwashauri wagombea both nyamagana na ilemela ambako cdm lazima wanashinda ila uchaguzi umepigwa tarehe!
 
Mkuu wa MKOA wa MWANZA ndie alieyeanza kuwapa hongo MADIWANI WA CHADEMA wa Kuchaguliwa ili

Wabadilishe kura zao kuchagua Mwana CCM as MAYOR... na tatizo walilonalo CHADEMA Mwanza na ILEMELA

Dah mkuuu unaweza ukatuma more evidence to support your statement
 
cdm isiwavumilie mamluki hata kama, itamaanisha kushindwa 2015, bora tushindwe kuliko kushinda tukiwa na watu wenye akili za ki-ccm ccm

Joely: Ni kweli kabisa wingi siyo hoja. Kuliko CDM irithi tabia za CCM ni vema iendelee kuwaelimisha wananchi misingi ya utawala bora na huo ndio msingi imara wa kuendesha nchi na kuleta maendeleo ya kweli kwa kuwa wananchi watakuwa na uelewa, na kushirikishwa katika kupanga maendeleo endelevu yao na serikali yao.
 


ninazo kumbukumbu kuwa nccr likumbwa na kundi kubwa la mamluki mpaka kikasambaratika;kwamba karibu asilimia kubwa walikuwa wanachama wakutengenezwa na ccm na usalama wa taifa ambao walipandikizwa nccr kupanga na kutekeleza migogoro ili kisilete upinzani wa dhati kuipumulia ccm karibu.hayohayo yamefanyika kwa cuf mpaka sasa haielewiki kule visiwani zanzibar na pemba kama bado chama cha upinzani .haya pia yalitegemewa kwa cdm yatokee,sikweli kabisa kundi kubwa linaloshabikia cdm ni wahafidhina wa upinzani, wengine mamluki na wachumia tumbo.weamekuwpo lutekeleza mipango ya ccm na usalama wa taifa kuidhofisha cdm, ili ccm iendelee kutawala milele.hapa nape hana cha kujivunia, chaguzi kama za meya si kioo cha kuonyesha imara wa ccm, bali mbinu chafu kuionyesha jamii kuwa bado kinapendwa na umma.swali jamii itarudisha imani ya kutumikia wanyonge kwa kushinda umeya huku ukirubuni madiwani wa cuf na baadhi ya mamluki wa chadema?kwa sasa nape angejitahidi kuwatumikia wanyoge waliopoteza imani na serikali yao badala ya kujidaganya na viuchaguzi vya hila kama ngao kwa umma, wakati ukweli hali si nzuri.serikali hiyohiyo ndo imesababisha chama cha ushirika kufirisika kwa kumtumia dalali ambaye alikuwa mbunge wa ccm kuhujumu ushirika huo kwa kuuza mali za ushirika, hivyo kuwafanya wakulima kwa sasa kupata bei duni .huyohuyo mbunge wa ccm magu dr.limbu amekuwa msitari wa mble kuwakejeri wakulima wa zao hilo bila kkuishauri serikali itie mkono kuwasaidia wapate bei nzuri.kwa hiyo nape kujiridhisha kwa uchaguzi wa meya kama msingi wa maisha ya wana mwanza ni kukumbatia utoto.



pumba tupu....kumbe sio kila anaejaza thread kama wewe ana mawazo mtambuka? Bora hata ungeandika "habari zenu great thinkers" halafu usome posts za wenzako mkuu. Ungefanya la maana kuliko utumbo uliouandika.
 
Back
Top Bottom