maghambo619
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 1,538
- 1,360
Baada ya kauli ya Nape ya kua CHADEMA wamekua wakipokea fedha chafu na kuzisafisha kwa kupita michango ya wananchi ya kua pesa hizo zitaiweka CHADEMA madarakani na watowaji wa pesa hizo wanawinda rasilimali zetu ,gesi na mafuta ambayo kuna dalili ya kugunduliwa.Kitu amabacho kimeonekana kwa kauli yake,mbali ya kutokua na mantiki ni kichekesho.Kwa sababu ni CCM ambayo iko madarakani imekua ikitumia pesa chafu katika kampeni zake,kuwalazimisha wafanyabiashara na walalahoi kuichangia bila ridhaa yao,kuuza rasilimali zetu dhahabu,almasi na ufisadi mwingine mwingi.
Kwa kauli ya Nape inaonyesha ya kua CCM imeisha kata tamaa ya kurudi madarakani kwa hiyo kwa mawazo yake nikwamba CHADEMA ikichukua madaraka itaendeleza mfumu uliokua ukitumiwa na CCM,kuuza rasilimali zetu ili kupata pesa chafu kiiendesha.Hivyo sivyo,wakati CHADEMA kinakusanya pesa na michango toka kwa wananchi pamoja na ruzuku wanayoipata ,wanaitumia kuwaelimisha walalahoi kuhusu haki zao na uozo wa CCM na utawala kwa ujumla.Wakati CCM ruzuku,pesa chafu,michango ya kuwalazimisha wafanyabiashara na pesa inayoptikana kiufisadi,kwanza wanajinufaisha wao watawala na kiasi kidogo kinachobaki wanakitumia kuwarubuni kwa kuwanunua fulana na,khanga,kofia pilau n.k.
kwa hali ilivyo hivi sasa pesa hazitoshi na wanaionea Wivu CHADEMA kwa walivyojipanga na kuanzisha uzushi usio na kichwa wala miguu.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
naam, inauma sana uhai unapoitoka ccm. Afu wale wanaoitwa machizi na waropokaji wanaposhika hatamu! Haleluyah!!