VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Mnauye ameonekana kuwa na urafiki wa karibu na kundi la Lowassa na Chenge ambalo wanachama wa CCM wamelibatiza jina la 'LO-CHE UNITY' hapa Dodoma.
Nape amekaririwa akisema kuwa hakuna ajenda ya kuwafukuza wanachama wowote wale wa CCM kwani ajenda hiyo haipo mbele ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Rais Jakaya Mrisho Halfan Kikwete.
Nape alikanusha vikali habari zilizoanzishwa jana humu kwenye JamiiForums baada ya mimi kumtupia swali juu ya ukweli wa habari hizo. Katika kuonyesha uswahiba wake na LO-CHE UNIT, Nape amekuwa akiambatana na wafuasi wakubwa wa kundi la Lowassa ambao ni Hussein Bashe na Ole Millya.
Wachambuzi wa mambo wanadai kuwa Nape amelazimishwa kusalimu amri na Wakubwa zake ndani ya Chama. Nape amenywea na kuamua kulinda kitumbua chake.
Nikiripoti kutoka Vikao vya CC na NEC ya CCM Dodoma,mimi ni Vuta-Nkuvute wa JamiiForums.
Nape amekaririwa akisema kuwa hakuna ajenda ya kuwafukuza wanachama wowote wale wa CCM kwani ajenda hiyo haipo mbele ya Mwenyekiti wa Chama Taifa, Rais Jakaya Mrisho Halfan Kikwete.
Nape alikanusha vikali habari zilizoanzishwa jana humu kwenye JamiiForums baada ya mimi kumtupia swali juu ya ukweli wa habari hizo. Katika kuonyesha uswahiba wake na LO-CHE UNIT, Nape amekuwa akiambatana na wafuasi wakubwa wa kundi la Lowassa ambao ni Hussein Bashe na Ole Millya.
Wachambuzi wa mambo wanadai kuwa Nape amelazimishwa kusalimu amri na Wakubwa zake ndani ya Chama. Nape amenywea na kuamua kulinda kitumbua chake.
Nikiripoti kutoka Vikao vya CC na NEC ya CCM Dodoma,mimi ni Vuta-Nkuvute wa JamiiForums.