Nape atumia ziara zake mikoani kumwandama Lowassa

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
KATIBU wa Idara ya Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye anadaiwa kuwatisha wanachama wa chama hicho wanaomuunga mkono Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Chanzo chetu kilicho ndani ya chama hicho, kimesema chini ya mkakati huo, Nape amekuwa akiwatisha wana CCM hao wakiwamo wanaotarajia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.

"Kuna mkakati mbaya unasukwa na Nape na amekuwa akitumia nguvu zote kuhakikisha wana CCM wanaomuunga mkono Lowassa hawapiti katika uchaguzi wa ndani wa chama chetu.

"Katika kutekeleza hili, Nape anawatisha watu hao moja kwa moja kwa kukutana nao ama kwa kuwapigia simu na kuwaeleza madhara ya kuendelea kumuunga mkono Lowassa.

"Katika hili, amekuwa akiwaambia kuwa, hawatakiwi kuwa upande wa Lowassa na kibaya zaidi anawaambia kuwa, kama wataendelea kuwa upande wa Lowassa, hawatashinda katika nafasi zozote watakazogombea au atakata majina yao pindi watakapogombea," kilisema chanzo hicho.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, Nape anatekeleza mpango huo katika ziara zake anazozifanya katika mikoa mbalimbali nchini, kwa kisingizio cha kukijenga Chama cha Mapinduzi.

Chanzo hicho kimeendelea kusema kuwa, hadi sasa Nape ameshawatisha baadhi ya wana CCM walioko katika Mikoa ya Iringa, Mbeya na Ruvuma.

Chanzo hicho, kimeendelea kusema katika utekelezaji wa mkakati huo, Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi, amekuwa akimtumia mmoja wa vijana walioko katika Idara ya Mambo ya Nje, aliyetajwa kwa jina moja la Nyakia. Kijana huyo yuko Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba Dar es Salaam.

"Nape anamtumia Nyakia katika mkakati huu kwa sababu kila anapokwenda, anakuwa naye na huyu kazi yake ni kufuatilia kila mkoa ni nani yuko upande wa Lowassa, kisha anampa taarifa Nape ambaye huwaita na kuwatisha au huzungumza nao kwa njia ya simu, akiwataka wasiwe upande wa Lowassa," kilisema chanzo hicho.

Nyakia alipozungumza na MTANZANIA kwa simu juzi, alihamaki na kutaka aelezwe ni nani aliyetoa taarifa hizo katika vyombo vya habari.

Hata hivyo, mwandishi wetu aliposema hawezi kumtajia aliyetoa taarifa hizo, alisema hana taarifa nazo na kutaka aulizwe Nape kwa kuwa ndiye anayejua jukumu lake ndani ya chama.

Nape alipozungumza na MTANZANIA jana kwa simu alisema jambo hilo halipo kwa sababu katika dunia ya sasa, huwezi kumtisha mtu kwa kuwa hakuna sababu ya kufanya hivyo.

"Kwanza kabisa jana ulizungumza na Nyakia, kisha ukazungumza na Chongolo, sasa nasema hivi, jambo hilo halipo kwa sababu mimi siwezi kuwatisha watu katika dunia ya sasa.

"Nakwambia huo ni upumbavu, najua wanaoandaa mambo haya ni Lowassa na wenzake, tafadhali msijiingize katika mambo haya, kama mtaandika andikeni, lakini mwishowe tutaanza kuwapiga wao kisha tutawapiga nyinyi ambao ni rafiki zetu.

"Mimi kazi yangu mikoani ni kuimarisha chama, yaani tukikaa ndani bila kutoka nje yanakuwa matatizo, tukitoka nje yanakuwa matatizo, nasema hayo mambo hayapo, waambieni welete hata mtu mmoja aliyetishwa na mimi au hata aliyetishwa na ofisa wangu.

"Hili siyo jambo jema mnataka kutugombanisha, sasa kama mtaitumia tumieni lakini ipo siku tutaanza kuwapiga na nyingi," alisema Nape kwa hasira.


CHANZO: Gazeti la Mtanzania
 
CCM dhaifu inamwogopa kweli Lowassa, walimtosa kwa Richmond ya Kikwete, ambae alimkataza Lowassa kuifukuza
 
nape asipoteze mda kushindana na lowassa yule ni kichwa wenzake wengi wamekuja na kuondoka yeye bado yupo
 
Nape hana jipya ameshiba pesa za Membe....lakini wasahau urais 2015 ni LOWASA AU DK.SILAHA tunataka watendaji si wapiga porojo.
 
katibu wa idara ya itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (ccm), nape nnauye anadaiwa kuwatisha wanachama wa chama hicho wanaomuunga mkono waziri mkuu wa zamani, edward lowassa.

Chanzo chetu kilicho ndani ya chama hicho, kimesema chini ya mkakati huo, nape amekuwa akiwatisha wana ccm hao wakiwamo wanaotarajia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.

“kuna mkakati mbaya unasukwa na nape na amekuwa akitumia nguvu zote kuhakikisha wana ccm wanaomuunga mkono lowassa hawapiti katika uchaguzi wa ndani wa chama chetu.

“katika kutekeleza hili, nape anawatisha watu hao moja kwa moja kwa kukutana nao ama kwa kuwapigia simu na kuwaeleza madhara ya kuendelea kumuunga mkono lowassa.

“katika hili, amekuwa akiwaambia kuwa, hawatakiwi kuwa upande wa lowassa na kibaya zaidi anawaambia kuwa, kama wataendelea kuwa upande wa lowassa, hawatashinda katika nafasi zozote watakazogombea au atakata majina yao pindi watakapogombea,” kilisema chanzo hicho.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, nape anatekeleza mpango huo katika ziara zake anazozifanya katika mikoa mbalimbali nchini, kwa kisingizio cha kukijenga chama cha mapinduzi.

Chanzo hicho kimeendelea kusema kuwa, hadi sasa nape ameshawatisha baadhi ya wana ccm walioko katika mikoa ya iringa, mbeya na ruvuma.

Chanzo hicho, kimeendelea kusema katika utekelezaji wa mkakati huo, katibu huyo wa itikadi na uenezi, amekuwa akimtumia mmoja wa vijana walioko katika idara ya mambo ya nje, aliyetajwa kwa jina moja la nyakia. Kijana huyo yuko ofisi ndogo ya ccm, lumumba dar es salaam.

“nape anamtumia nyakia katika mkakati huu kwa sababu kila anapokwenda, anakuwa naye na huyu kazi yake ni kufuatilia kila mkoa ni nani yuko upande wa lowassa, kisha anampa taarifa nape ambaye huwaita na kuwatisha au huzungumza nao kwa njia ya simu, akiwataka wasiwe upande wa lowassa,” kilisema chanzo hicho.

Nyakia alipozungumza na mtanzania kwa simu juzi, alihamaki na kutaka aelezwe ni nani aliyetoa taarifa hizo katika vyombo vya habari.

Hata hivyo, mwandishi wetu aliposema hawezi kumtajia aliyetoa taarifa hizo, alisema hana taarifa nazo na kutaka aulizwe nape kwa kuwa ndiye anayejua jukumu lake ndani ya chama.

Nape alipozungumza na mtanzania jana kwa simu alisema jambo hilo halipo kwa sababu katika dunia ya sasa, huwezi kumtisha mtu kwa kuwa hakuna sababu ya kufanya hivyo.

“kwanza kabisa jana ulizungumza na nyakia, kisha ukazungumza na chongolo, sasa nasema hivi, jambo hilo halipo kwa sababu mimi siwezi kuwatisha watu katika dunia ya sasa.

“nakwambia huo ni upumbavu, najua wanaoandaa mambo haya ni lowassa na wenzake, tafadhali msijiingize katika mambo haya, kama mtaandika andikeni, lakini mwishowe tutaanza kuwapiga wao kisha tutawapiga nyinyi ambao ni rafiki zetu.

“mimi kazi yangu mikoani ni kuimarisha chama, yaani tukikaa ndani bila kutoka nje yanakuwa matatizo, tukitoka nje yanakuwa matatizo, nasema hayo mambo hayapo, waambieni welete hata mtu mmoja aliyetishwa na mimi au hata aliyetishwa na ofisa wangu.

“hili siyo jambo jema mnataka kutugombanisha, sasa kama mtaitumia tumieni lakini ipo siku tutaanza kuwapiga na nyingi,” alisema nape kwa hasira.


chanzo: Gazeti la mtanzania
nape = gamba
 
Nape nadhani anataka kufukuzwa na nyinyiemu!

Kwanza nape hamuwezi lowasa kwa lolote

basi amvue gamba kama anaweza
 
Vita kati ya Nape na Lowassa vimemuimarisha Lowassa na kumpa nape jina la vuvuzela!!!
Nape hamuwezi lowassa,ataishia kufa kifo kibaya kisiasa
 
Hivi siku 90 za kumvua gamba lowassa na chenge hazijaisha?alidakia kauli ya kisanii ya boss wake ambaye pia anamuogopa lowassa
 
Sijampata vizuri anaposema "Tutawapiga"! Hiyo ndio imekuwa njia yao ya kuwanyamazisha watu wanaowapinga! Pole sana Dr. Ulimboka, laiti kama ungelijua hili mapema.
 
Jk yupo nyuma ya kuchafuliwa Lowassa, wanajua akishinda atachapa bakora CCM nzima, Lowassa ni Uzalendo tu aloutoa Jeshini na si chama, ubilionea wake ni asilia na nyerere shahidi
 
Nape anampa shida sana lowassa....too bad hana cha kumfanya zaidi ya kumtungia uzushi
 
Simshangai, na magamba kutisha wanachama wao ni jadi ili kufanikisha jambo wanalolitaka
 
pole sana nape kwa kujua kuwa lowassa ni dume la mbegu na humuwezi kwa lolote 2013 ndio mwisho wako na lowasa na akina chenge wanapeta tu sijiu utafanya kazi gani maana unchokijua ni siasa tu si kingine
 



JUMATATU, JULAI 02, 2012 05:50

NA MWANDISHI WETU - MTANZANIA



KATIBU wa Idara ya Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye anadaiwa kuwatisha wanachama wa chama hicho wanaomuunga mkono Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.Chanzo chetu kilicho ndani ya chama hicho, kimesema chini ya mkakati huo, Nape amekuwa akiwatisha wana CCM hao wakiwamo wanaotarajia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.

"Kuna mkakati mbaya unasukwa na Nape na amekuwa akitumia nguvu zote kuhakikisha wana CCM wanaomuunga mkono Lowassa hawapiti katika uchaguzi wa ndani wa chama chetu.

"Katika kutekeleza hili, Nape anawatisha watu hao moja kwa moja kwa kukutana nao ama kwa kuwapigia simu na kuwaeleza madhara ya kuendelea kumuunga mkono Lowassa.

"Katika hili, amekuwa akiwaambia kuwa, hawatakiwi kuwa upande wa Lowassa na kibaya zaidi anawaambia kuwa, kama wataendelea kuwa upande wa Lowassa, hawatashinda katika nafasi zozote watakazogombea au atakata majina yao pindi watakapogombea," kilisema chanzo hicho.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, Nape anatekeleza mpango huo katika ziara zake anazozifanya katika mikoa mbalimbali nchini, kwa kisingizio cha kukijenga Chama cha Mapinduzi.

Chanzo hicho kimeendelea kusema kuwa, hadi sasa Nape ameshawatisha baadhi ya wana CCM walioko katika Mikoa ya Iringa, Mbeya na Ruvuma.

Chanzo hicho, kimeendelea kusema katika utekelezaji wa mkakati huo, Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi, amekuwa akimtumia mmoja wa vijana walioko katika Idara ya Mambo ya Nje, aliyetajwa kwa jina moja la Nyakia. Kijana huyo yuko Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba Dar es Salaam.

"Nape anamtumia Nyakia katika mkakati huu kwa sababu kila anapokwenda, anakuwa naye na huyu kazi yake ni kufuatilia kila mkoa ni nani yuko upande wa Lowassa, kisha anampa taarifa Nape ambaye huwaita na kuwatisha au huzungumza nao kwa njia ya simu, akiwataka wasiwe upande wa Lowassa," kilisema chanzo hicho.

Nyakia alipozungumza na MTANZANIA kwa simu juzi, alihamaki na kutaka aelezwe ni nani aliyetoa taarifa hizo katika vyombo vya habari.

Hata hivyo, mwandishi wetu aliposema hawezi kumtajia aliyetoa taarifa hizo, alisema hana taarifa nazo na kutaka aulizwe Nape kwa kuwa ndiye anayejua jukumu lake ndani ya chama.

Nape alipozungumza na MTANZANIA jana kwa simu alisema jambo hilo halipo kwa sababu katika dunia ya sasa, huwezi kumtisha mtu kwa kuwa hakuna sababu ya kufanya hivyo.

"Kwanza kabisa jana ulizungumza na Nyakia, kisha ukazungumza na Chongolo, sasa nasema hivi, jambo hilo halipo kwa sababu mimi siwezi kuwatisha watu katika dunia ya sasa.

"Nakwambia huo ni upumbavu, najua wanaoandaa mambo haya ni Lowassa na wenzake, tafadhali msijiingize katika mambo haya, kama mtaandika andikeni, lakini mwishowe tutaanza kuwapiga wao kisha tutawapiga nyinyi ambao ni rafiki zetu.

"Mimi kazi yangu mikoani ni kuimarisha chama, yaani tukikaa ndani bila kutoka nje yanakuwa matatizo, tukitoka nje yanakuwa matatizo, nasema hayo mambo hayapo, waambieni welete hata mtu mmoja aliyetishwa na mimi au hata aliyetishwa na ofisa wangu.

"Hili siyo jambo jema mnataka kutugombanisha, sasa kama mtaitumia tumieni lakini ipo siku tutaanza kuwapiga na nyingi," alisema Nape kwa hasira.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom