Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Nape amzodoa kwa aibu Mnyika kuhusu wanawake
Mwanasiasa shupavu na mjumbe wa NEC ya chama tawala(CCM) Nape Nnauye amemzodoa kijana wa CHADEMA, John Mnyika kuhusiana na kauli zake kuhusu uwakilishi wa wanawake katika siasa.
Tukio hilo lilitokea katika Mkutano uliondaliwa na Kituo cha Demokrasia(TCD) uliofanyika hivi karibuni.
Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Waziri wa Jinsia, Wanawake na Watoto, Dr Nkya ambae pamoja na mambo mengine aliisifu CCM kwa kuwa mstari wa mbele kwa kuwajali wanawake kwa kupitisha mfumo wa uwakilishi wa 50 kwa 50 baina ya wanawake na wanaume. Waziri Nkya alivitaka vyama vyote kuiga mfano wa CCM.
Baadaye ilifuatiwa na Mada iliyowasilishwa na waziri kiongozi wa zamani wa Zanzibar Dr Ghalib Billal ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Kamati iliyotoa mapendekezo kuhusu namna ya kupanua uwakilishi wa wanawake bungeni. Dr Billal alieleza kuwa kamati yake imeiwezesha CCM kupitisha mfumo ambao utawezesha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 uwakilishi baina ya wanawake na wanaume kuwa 50 kwa 50.
Majadiliano yalipofunguliwa kiongozi Nape Nnauye naye akaeleza kwa kina kuwa CCM iko mstari wa mbele katika kuweka viongozi katika nafasi za uongozi kupitia mfumo wa 50 kwa 50 na kwamba suala hilo limetokana na ilani ya chama hicho.
Alipopewa nafasi ya kuchagia kwa upande wake, kijana Mnyika alitaka kwamba wajumbe wachangie bila kujali vyama vyao wakitanguliza maslahi ya taifa na kueleza ukweli wa hali halisi ilivyo Tanzania ili wadau washirikiane kuleta mabadiliko ya kweli.
Kijana Mnyika alikwenda mbali zaidi kwa kubeza kwamba hakuna chama nchini ambacho kimepitisha mfumo wa 50 kwa 50 katika katiba ya chama chao. Alisema vyama vyote vikubwa, vya CCM, CHADEMA na CUF katika katiba zao hakuna mfumo 50 kwa 50, na kwamba kilichopo katika vyama hivyo ni uwakilishi wa asilimia 30 tu ya wanawake katika marekebisho ya katiba za vyama hivyo.
Kijana Mnyika aliendelea zaidi kuwa hakuna dhamira ya kisiasa toka kwa chama tawala kuweka mfumo wa uwakilishi wa asilimia 50 kwa 50 katika uchaguzi wa mwaka 2010. Alisema kuwa amegusa dhamira ya chama tawala kwa kuwa chama hicho kina uwingi mkubwa bungeni kwa sasa hivyo mabadiliko yoyote ya kimfumo lazima yatokane na dhamira ya kweli kwa upande wa chama hicho.
Alisema kwamba anao ushahidi wa CCM kutokuwa na dhamira hiyo kwa kuwa anayo maazimio ya kikao cha NEC chama cha hicho kilichofanyika tarehe 7 mwezi Machi, mwaka 2009 na maamuzi ambayo chama hicho kimefikia kuhusu mfumo wa 50 kwa 50.
Aliituhumu NEC ya CCM kwamba imepitisha azimio la chama hicho kuielekeza serikali kufanya haraka marekebisho ya katiba yatayofanya bunge liwe na wabunge 360.
Pia NEC imeitaka serikali kuongeza wabunge wa viti maalumu kufikia 109. Na Hatimaye NEC imeitaka serikali imuongezee zaidi Rais mamlaka ya kuteua Wabunge na sasa aweze kuteua Wabunge 14 na kati yao apewe nafasi ya kuteua wabunge wanawake 7. Bwana Mnyika akasema kwamba chini ya maelekezo hayo ya NEC ya CCM kwa serikali uwakilishi wa wanawake wa moja kwa moja utakuwa ni wabunge 109, na wabunge wengine 7 ambayo jumla ni 116 ambayo ni sawa na asilimia 33%. Bwana Mnyika alisema kwamba asilimia hiyo sio 50% ambayo ndiyo inatakiwa katika mfumo wa 50 kwa 50. Hivyo akaituhumu CCM kwa kufanya propaganda za kisiasa za kuwarubuni wanawake kuwa inawajali wakati ambapo tayari imeshapitisha maazimio ya marekebisho ya katiba ambayo hayaendani na kauli za CCM za majukwaani kuwa imepitisha mfumo wa 50 kwa 50. Kijana Mnyika alisema kuwa nusu ya 360 ni wabunge 180, hivyo kama mfumo wa 50 kwa 50 basi uwakilishi wa wanawake ungepaswa kufikia kiwango hiko. Kijana Mnyika alisema kuwa kuna tofauti kati ya maneno ya kwenye ilani ya CCM na matendo yanayofanyika kwenye maamuzi ya utekelezaji. Hivyo, alitaka vyama vyote kwa pamoja kukikiri kwamba kama taifa bado hakuna mfumo wa uwakilishi wa 50 kwa 50 kama hatua ya kwanza katika katika kujadili mwelekeo kuhusu suala hilo. Aliendelea kusema kwamba njia pekee ya kutekeleza ahadi hiyo ni CCM kukubali sauti ya wananchi ya kufanya mabadiliko ya katiba ili kuwa na katiba mpya. Akafafanua kwamba mabadililko hayo lazima yahusishe kuingiza katika katika mfumo wa uchaguzi utakaohusisha uwakilishi wa uwiano, lakini suala lisiwe idadi tu bali pia ajenda zinazogusa wanawake wenyewe na mustakabali wa taifa. Alitaka wajumbe kutazama picha kubwa zaidi ya wanawake.
Kauli hiyo ilimfanya mjumbe wa NEC, kiongozi Nape Nnauye kuingilia kati na kumzodoa mwaka Mnyika kwa kutoa maelezo yasiyokuwa ya kweli. Kiongozi Nape alisema kuwa ni kweli NEC imepitisha maamuzi hayo lakini si kweli kwamba CCM haina dhamira ya kutekeleza mfumo wa 50 kwa 50. Nape alienda mbali zaidi kwa kumweleza wazi Mnyika kuwa CCM haifanyi propaganda katika suala hilo bali ina dhamira ya kweli ya kuweka mstari wa mbele wanawake. Nape alifafanua kuwa tayari asilimia 33 imepangwa kwa ajili ya wanawake pekee, lakini asilimia 17 iliyobaki NEC imeazimia kwamba wapatikane toka majimboni. Kiongozi Nape akataja majina ya wanawake wa CCM ambao wamefanikiwa kushinda uchaguzi katika majimbo mwaka 2005 na akafafanua kwamba katika uchaguzi wa mwaka 2010 asilimia hiyo 17 ya wanawake itafikiwa na hivyo kufanya wanawake kuwa asilimia 50 katika Bunge. Pia Nape akaeleza kwamba pengine kijana Mnyika hajasoma katiba za vyama kwa kuwa CCM tayari ilishafanya mabadiliko ya katiba yake na kuwa katika uongozi wa ndani wa chama hicho kwa sasa uwakilishi ni asilimia 50 wa 50.
Baada ya kuzodolewa kwa kiwango hicho, kijana Mnyika aliingilia kati kutaka kutoa taarifa, lakini Mwenyekiti wa Mkutano huo, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mama Kidawa ambaye alimwakilisha Makamu Pius Msekwa alikataa taarifa hiyo.
Mara baada ya Kiongozi Nape kumaliza kuzungumza kijana Mnyika alianza kuchagia bila kufuata utaratibu kuanza kutoa ufafanuzi. Kijana Mnyika alisema kwamba ana hakika kuwa hakuna katiba ya chama chochote hapa Tanzania yenye uwakilishi wa 50 kwa 50, alisema kuwa anachokisema Nape ni kuhusu wajumbe ambao hata kwenye katiba ya CHADEMA wapo 50 kwa 50. Akatolea kwa mfano Kamati Kuu ya CHADEMA inawajumbe 8 wa kuchaguliwa ambao katiba ya chama hicho inaeleza bayana kwamba lazima 50% wawe wanawake, na 50% wawe wanaume, lakini huo sio mfumo wa 50-50 unaozungumzwa. Akasema mfumo wa 50-50 unahusu muundo na uwakilishi wa kikao kizima cha maamuzi sio wajumbe wateule. Akauliza swali washiriki, je, kwa mujibu wa Katiba ya CCM nusu wa wote wanoshiriki kamati kuu ni wanawake?, nusu ya NEC je ni wanawake? Na Nusu ya Mkutano Mkuu nao ni wanawake? Kama jibu ni hapana basi hakuna mfumo wa 50 kwa 50 hapo. Akaanza kuzungumzia mfumo wa uwakilishi 50 kwa 50 katika bunge lakini Mwenyekiti wa Mkutano akamkatanisha na kuruhusu wachangiaji wengine, na kumfanya anyamaze kwa aibu.
Akichangia Mada hiyo, Afisa wa Uchaguzi(CHADEMA), Mama Suzan Kiwanga alieleza kuwa kama serikali ina dhamira ya kutekeleza mfumo wa 50 kwa 50 badala ya kuanzia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 katika ubunge basi uanzie katika uchaguzi wa mitaa na vijiji unaofanyika mwaka 2009. Hii itawezesha kupata uzoefu kama mfumo huu unatekelezeka. Alisema kwamba ameshangaa katika makubaliano ambayo serikali imesaini na wadau Morogoro mwezi Februari mwaka 2009 kuhusu kanuni za uchaguzi wa 2009, suala la uwakilishi wa 50 kwa 50 wa wanawake halipo. Hivyo, akaitaka CCM na serikali yake kuzingatia suala hilo. Mama Kiwanga akaeleza kuwa kuna ugumu wa wanawake kushinda majimboni kwani yeye mwenyewe aliwahi kuwa mgombea ubunge katika jimbo la Kilombero.
Wanaharakati mbalimbali wamekuwa wakielezea kuwa wanawake wanakosa nafasi ya kugombea na kushinda majimboni. Takwimu zao zinaeleza kuwa katika uchaguzi wa mwaka 2005 takribani wanawake 300 walichukua fomu za ubunge na kuingia katika kura za maoni za CCM pekee lakini kati yao waliopitishwa ni chini ya wagombea 20 kupitia chama hicho. Katika takwimu zao wanaeleza kuwa vyama vidogo vidogo kama NLD ndivyo ambayo vinaongoza kwa kutoa nafasi zaidi kwa wanawake kugombea ubunge kupitia vyama hivyo.
Akitihimisha mada hiyo, Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake hapa nchini(UNIFEM), Mama Salome alisema kwamba amesikia ufafanuzi wa Kiongozi Nape wa jinsi ambavyo CCM imeweka mfumo wa kutekeleza 50 kwa 50. Mkutano huo wa siku mbili, uliohusisha viongozi wakuu wa vyama, wizara, vyombo vya habari na asasi za kiraia ulipitisha maazimio mbalimbali ya jinsi ya kuweka uwiano wa kijinsia katika mifumo ya kisiasa.
ndiyohiyo
Mwanasiasa shupavu na mjumbe wa NEC ya chama tawala(CCM) Nape Nnauye amemzodoa kijana wa CHADEMA, John Mnyika kuhusiana na kauli zake kuhusu uwakilishi wa wanawake katika siasa.
Tukio hilo lilitokea katika Mkutano uliondaliwa na Kituo cha Demokrasia(TCD) uliofanyika hivi karibuni.
Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Waziri wa Jinsia, Wanawake na Watoto, Dr Nkya ambae pamoja na mambo mengine aliisifu CCM kwa kuwa mstari wa mbele kwa kuwajali wanawake kwa kupitisha mfumo wa uwakilishi wa 50 kwa 50 baina ya wanawake na wanaume. Waziri Nkya alivitaka vyama vyote kuiga mfano wa CCM.
Baadaye ilifuatiwa na Mada iliyowasilishwa na waziri kiongozi wa zamani wa Zanzibar Dr Ghalib Billal ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Kamati iliyotoa mapendekezo kuhusu namna ya kupanua uwakilishi wa wanawake bungeni. Dr Billal alieleza kuwa kamati yake imeiwezesha CCM kupitisha mfumo ambao utawezesha katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 uwakilishi baina ya wanawake na wanaume kuwa 50 kwa 50.
Majadiliano yalipofunguliwa kiongozi Nape Nnauye naye akaeleza kwa kina kuwa CCM iko mstari wa mbele katika kuweka viongozi katika nafasi za uongozi kupitia mfumo wa 50 kwa 50 na kwamba suala hilo limetokana na ilani ya chama hicho.
Alipopewa nafasi ya kuchagia kwa upande wake, kijana Mnyika alitaka kwamba wajumbe wachangie bila kujali vyama vyao wakitanguliza maslahi ya taifa na kueleza ukweli wa hali halisi ilivyo Tanzania ili wadau washirikiane kuleta mabadiliko ya kweli.
Kijana Mnyika alikwenda mbali zaidi kwa kubeza kwamba hakuna chama nchini ambacho kimepitisha mfumo wa 50 kwa 50 katika katiba ya chama chao. Alisema vyama vyote vikubwa, vya CCM, CHADEMA na CUF katika katiba zao hakuna mfumo 50 kwa 50, na kwamba kilichopo katika vyama hivyo ni uwakilishi wa asilimia 30 tu ya wanawake katika marekebisho ya katiba za vyama hivyo.
Kijana Mnyika aliendelea zaidi kuwa hakuna dhamira ya kisiasa toka kwa chama tawala kuweka mfumo wa uwakilishi wa asilimia 50 kwa 50 katika uchaguzi wa mwaka 2010. Alisema kuwa amegusa dhamira ya chama tawala kwa kuwa chama hicho kina uwingi mkubwa bungeni kwa sasa hivyo mabadiliko yoyote ya kimfumo lazima yatokane na dhamira ya kweli kwa upande wa chama hicho.
Alisema kwamba anao ushahidi wa CCM kutokuwa na dhamira hiyo kwa kuwa anayo maazimio ya kikao cha NEC chama cha hicho kilichofanyika tarehe 7 mwezi Machi, mwaka 2009 na maamuzi ambayo chama hicho kimefikia kuhusu mfumo wa 50 kwa 50.
Aliituhumu NEC ya CCM kwamba imepitisha azimio la chama hicho kuielekeza serikali kufanya haraka marekebisho ya katiba yatayofanya bunge liwe na wabunge 360.
Pia NEC imeitaka serikali kuongeza wabunge wa viti maalumu kufikia 109. Na Hatimaye NEC imeitaka serikali imuongezee zaidi Rais mamlaka ya kuteua Wabunge na sasa aweze kuteua Wabunge 14 na kati yao apewe nafasi ya kuteua wabunge wanawake 7. Bwana Mnyika akasema kwamba chini ya maelekezo hayo ya NEC ya CCM kwa serikali uwakilishi wa wanawake wa moja kwa moja utakuwa ni wabunge 109, na wabunge wengine 7 ambayo jumla ni 116 ambayo ni sawa na asilimia 33%. Bwana Mnyika alisema kwamba asilimia hiyo sio 50% ambayo ndiyo inatakiwa katika mfumo wa 50 kwa 50. Hivyo akaituhumu CCM kwa kufanya propaganda za kisiasa za kuwarubuni wanawake kuwa inawajali wakati ambapo tayari imeshapitisha maazimio ya marekebisho ya katiba ambayo hayaendani na kauli za CCM za majukwaani kuwa imepitisha mfumo wa 50 kwa 50. Kijana Mnyika alisema kuwa nusu ya 360 ni wabunge 180, hivyo kama mfumo wa 50 kwa 50 basi uwakilishi wa wanawake ungepaswa kufikia kiwango hiko. Kijana Mnyika alisema kuwa kuna tofauti kati ya maneno ya kwenye ilani ya CCM na matendo yanayofanyika kwenye maamuzi ya utekelezaji. Hivyo, alitaka vyama vyote kwa pamoja kukikiri kwamba kama taifa bado hakuna mfumo wa uwakilishi wa 50 kwa 50 kama hatua ya kwanza katika katika kujadili mwelekeo kuhusu suala hilo. Aliendelea kusema kwamba njia pekee ya kutekeleza ahadi hiyo ni CCM kukubali sauti ya wananchi ya kufanya mabadiliko ya katiba ili kuwa na katiba mpya. Akafafanua kwamba mabadililko hayo lazima yahusishe kuingiza katika katika mfumo wa uchaguzi utakaohusisha uwakilishi wa uwiano, lakini suala lisiwe idadi tu bali pia ajenda zinazogusa wanawake wenyewe na mustakabali wa taifa. Alitaka wajumbe kutazama picha kubwa zaidi ya wanawake.
Kauli hiyo ilimfanya mjumbe wa NEC, kiongozi Nape Nnauye kuingilia kati na kumzodoa mwaka Mnyika kwa kutoa maelezo yasiyokuwa ya kweli. Kiongozi Nape alisema kuwa ni kweli NEC imepitisha maamuzi hayo lakini si kweli kwamba CCM haina dhamira ya kutekeleza mfumo wa 50 kwa 50. Nape alienda mbali zaidi kwa kumweleza wazi Mnyika kuwa CCM haifanyi propaganda katika suala hilo bali ina dhamira ya kweli ya kuweka mstari wa mbele wanawake. Nape alifafanua kuwa tayari asilimia 33 imepangwa kwa ajili ya wanawake pekee, lakini asilimia 17 iliyobaki NEC imeazimia kwamba wapatikane toka majimboni. Kiongozi Nape akataja majina ya wanawake wa CCM ambao wamefanikiwa kushinda uchaguzi katika majimbo mwaka 2005 na akafafanua kwamba katika uchaguzi wa mwaka 2010 asilimia hiyo 17 ya wanawake itafikiwa na hivyo kufanya wanawake kuwa asilimia 50 katika Bunge. Pia Nape akaeleza kwamba pengine kijana Mnyika hajasoma katiba za vyama kwa kuwa CCM tayari ilishafanya mabadiliko ya katiba yake na kuwa katika uongozi wa ndani wa chama hicho kwa sasa uwakilishi ni asilimia 50 wa 50.
Baada ya kuzodolewa kwa kiwango hicho, kijana Mnyika aliingilia kati kutaka kutoa taarifa, lakini Mwenyekiti wa Mkutano huo, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mama Kidawa ambaye alimwakilisha Makamu Pius Msekwa alikataa taarifa hiyo.
Mara baada ya Kiongozi Nape kumaliza kuzungumza kijana Mnyika alianza kuchagia bila kufuata utaratibu kuanza kutoa ufafanuzi. Kijana Mnyika alisema kwamba ana hakika kuwa hakuna katiba ya chama chochote hapa Tanzania yenye uwakilishi wa 50 kwa 50, alisema kuwa anachokisema Nape ni kuhusu wajumbe ambao hata kwenye katiba ya CHADEMA wapo 50 kwa 50. Akatolea kwa mfano Kamati Kuu ya CHADEMA inawajumbe 8 wa kuchaguliwa ambao katiba ya chama hicho inaeleza bayana kwamba lazima 50% wawe wanawake, na 50% wawe wanaume, lakini huo sio mfumo wa 50-50 unaozungumzwa. Akasema mfumo wa 50-50 unahusu muundo na uwakilishi wa kikao kizima cha maamuzi sio wajumbe wateule. Akauliza swali washiriki, je, kwa mujibu wa Katiba ya CCM nusu wa wote wanoshiriki kamati kuu ni wanawake?, nusu ya NEC je ni wanawake? Na Nusu ya Mkutano Mkuu nao ni wanawake? Kama jibu ni hapana basi hakuna mfumo wa 50 kwa 50 hapo. Akaanza kuzungumzia mfumo wa uwakilishi 50 kwa 50 katika bunge lakini Mwenyekiti wa Mkutano akamkatanisha na kuruhusu wachangiaji wengine, na kumfanya anyamaze kwa aibu.
Akichangia Mada hiyo, Afisa wa Uchaguzi(CHADEMA), Mama Suzan Kiwanga alieleza kuwa kama serikali ina dhamira ya kutekeleza mfumo wa 50 kwa 50 badala ya kuanzia katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 katika ubunge basi uanzie katika uchaguzi wa mitaa na vijiji unaofanyika mwaka 2009. Hii itawezesha kupata uzoefu kama mfumo huu unatekelezeka. Alisema kwamba ameshangaa katika makubaliano ambayo serikali imesaini na wadau Morogoro mwezi Februari mwaka 2009 kuhusu kanuni za uchaguzi wa 2009, suala la uwakilishi wa 50 kwa 50 wa wanawake halipo. Hivyo, akaitaka CCM na serikali yake kuzingatia suala hilo. Mama Kiwanga akaeleza kuwa kuna ugumu wa wanawake kushinda majimboni kwani yeye mwenyewe aliwahi kuwa mgombea ubunge katika jimbo la Kilombero.
Wanaharakati mbalimbali wamekuwa wakielezea kuwa wanawake wanakosa nafasi ya kugombea na kushinda majimboni. Takwimu zao zinaeleza kuwa katika uchaguzi wa mwaka 2005 takribani wanawake 300 walichukua fomu za ubunge na kuingia katika kura za maoni za CCM pekee lakini kati yao waliopitishwa ni chini ya wagombea 20 kupitia chama hicho. Katika takwimu zao wanaeleza kuwa vyama vidogo vidogo kama NLD ndivyo ambayo vinaongoza kwa kutoa nafasi zaidi kwa wanawake kugombea ubunge kupitia vyama hivyo.
Akitihimisha mada hiyo, Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake hapa nchini(UNIFEM), Mama Salome alisema kwamba amesikia ufafanuzi wa Kiongozi Nape wa jinsi ambavyo CCM imeweka mfumo wa kutekeleza 50 kwa 50. Mkutano huo wa siku mbili, uliohusisha viongozi wakuu wa vyama, wizara, vyombo vya habari na asasi za kiraia ulipitisha maazimio mbalimbali ya jinsi ya kuweka uwiano wa kijinsia katika mifumo ya kisiasa.
ndiyohiyo