Nape amjibu Lowassa kuhusu Ajira...!

Nilichokurupuka ni kipi? au kwasababu nimepingana na hoja ya kuwaita vijana bomu kila siku? Na kisa kasema flani? Lazima umtukane nape na kumwita mbumbumbu ndio siku yako iende?... Serikali imetoa takwimu za hali halisi ya ajira nchini, nikatakiwa kutoa maoni, nilichojibu kuwa serikali iko sahihi, hali ya ajira nchini kwa takwimu sio maneno ya barabarani, na hasa ukilinganisha na nchi hata za Afrika mashariki tu Tanzania ni bora kuliko zingine, umbumbumbu wa Nape uko wapi?


Nadhani ni vizuri pamoja na kutakiwa kutukana kila unapokuta jina la Nape, akili za kuambiwa changanya na zako....

Nakupendea wepesi wako wa kujibu hoja, BIG UP. lakini huwa na ashaka na hoja unavyozijibu, sorry for that
 
Serikali imetoa takwimu za waendesha boda boda kama ajira
 
ebu tusidanganyane...ajira zinapatikana kwa watoto wa vigogo tuu....ebu nendenei BOT mkajionee ni nani wapo huko....kutoa takwimu si kitu chochote.....tuangalieni hali halisi bwaaanaaa.............!

Hahaha! Kwa nini mwende BOT? Nendeni pale Lumumba Mkawakute kina Nnauye na Makamba wa Dunia hii, Nape anajidai kupambana na Ufisadi wakati yeye mwenyewe anaishi kifisadi, anatembelea V8 mjini wakati makatibu wa CCM vijini hawana hata baiskeli,!
 
Tatizo la CCM ndio hilo - unafiki. Lowassa haelewani nao lakini hawezi akatoka huko na akina Nape hawana ubavu wa kumwambia atoke au kumfukuza chamani. Wote wamebakia kupiga domo bila tija yoyote.

Halafu wewe Nape, ukiachana na takwimu feki za serikali, unaweza ukatuambia, kwa kifupi, nini sera ya CCM kuhusu ajira nchini, na kama unadhani sera hiyo inatekelezwa ipasavyo na serikali? Au hamna sera? Au hizo takwimu za Kabaka ndio sera yenyewe?
 
Nilichokurupuka ni kipi? au kwasababu nimepingana na hoja ya kuwaita vijana bomu kila siku? Na kisa kasema flani? Lazima umtukane nape na kumwita mbumbumbu ndio siku yako iende?... Serikali imetoa takwimu za hali halisi ya ajira nchini, nikatakiwa kutoa maoni, nilichojibu kuwa serikali iko sahihi, hali ya ajira nchini kwa takwimu sio maneno ya barabarani, na hasa ukilinganisha na nchi hata za Afrika mashariki tu Tanzania ni bora kuliko zingine, umbumbumbu wa Nape uko wapi?

Nadhani ni vizuri pamoja na kutakiwa kutukana kila unapokuta jina la Nape, akili za kuambiwa changanya na zako....

mbayuayu style 'akili za kuambiwa changanya na zako' (zakuambiwa+ zako)= uongo na wizi na kuikataa kauli yako mara tu mamvi akijitokeza hadharani. nape ndugu yangu siasa za kujikomba zitakuja kukuletea vidonda vya tumbo najua inakuuma kuona watu wanaipeleka kusiko ccm lakini ebu waachie meli yao izame chukua boti la kujiokoa kabla haijazama kabisa najua kutoka moyoni mwako unaona uelekeo wa chama chako waweza kuchukua hatua sasa usingoje kusema' ningejua'
 
Unafiki wa Nape ni upi?

Kama kusimamia msimo wangu kuwa rasilimali za nchi lazima zifaidishe watanzania walio wengi ni unafiki, nina furaha kuitwa mnafiki.....

Kama kwa kusema watu waache ufisadi na ulafi wa madaraka ni unafiki jina hilo linanifaa sana....

Haya mengine ya Arumeru Mashariki, najua ni hasira za kushindwa kutakakowakuta, na najua itakuwa aibu kubwa kwa magwanda, si vibaya mkitanguliza hasira zenu kwangu maana mie ndo punching bag.....

Nape,
Nakubaliana na hoja hii kwamba Lowassa alikuwa wapi siku zote hasa alipokuwa waziri mkuu?nilitegemea angetoa data kwamba ni kwa kiasi gani alichangia katika ongezeko la ajira kwa kusimamia project A,B,C,D na nyinginezo na jinsi ambavyo serikali ilishindwa kusimamia.

Pia kutumia kanisa siyo jukwaa sahihi,kwani nilitarajia angesema hayo kwenye midahalo ya wazi au kwenye press conference ambako watu wangeruhusiwa kuuliza maswali

Kashfa zinazomuandama Lowassa za RICHMOND,zilichangia kukwamisha ujenzi wa viwanda ambavyo vingetoa Ajira

Pia,mradi wa shule za kata bila sera sahihi uliishia kutuzalishia failures kibao mtaani ambao ndiyo janga au bomu linalotarajiwa kulipuka

Kwako Nape,ukiwa kama katibu uenezi wa CCM hustahili kutumia neno magwanda ku-adress chama kingine cha siasa.

Pia takwimu alizotoa waziri wa kazi na ajira,zinaonyesha hali ya kutowajibika kikamilifu au wizara hiyo na serikali nzima ya CCM imeonyesha kuwa haina suluhisho la tatizo la Ajira.

Mashambulizi dhidi ya Lowassa in regardless ya kile alichosema ni kupotoka,tunashambulia mtu badala ya hoja iliyotolewa na kutoa suluhisho thabiti

Kwa,Vijana Tanzania.Tusikubali kutumiwa na wanasiasa,wasitumie matatizo yetu kama mtaji wa kisiasa
 
Unafiki wa Nape ni upi?

Kama kusimamia msimo wangu kuwa rasilimali za nchi lazima zifaidishe watanzania walio wengi ni unafiki, nina furaha kuitwa mnafiki.....

Kama kwa kusema watu waache ufisadi na ulafi wa madaraka ni unafiki jina hilo linanifaa sana....

Haya mengine ya Arumeru Mashariki, najua ni hasira za kushindwa kutakakowakuta, na najua itakuwa aibu kubwa kwa magwanda, si vibaya mkitanguliza hasira zenu kwangu maana mie ndo punching bag.....

Mkuu NAPE HESHIMA YAKO..........
ETI NIMESIKIA MHESHIMIWA EDO ANASEMA YEYE AMEFANYA KAZI NA MZEE MNAUYE KWA MUDA MREFU LAKINI HAJAWAHI KUTAMBULISHWA KAMA WEWE NI MWANA FAMILIA YAKE....... KWA HIYO UNATUMIA JINA HILO KUJINUFAISHA KISIASA....... TAFADHARI TUNAOMBA JIBU!!!!
 
Nilichokurupuka ni kipi? au kwasababu nimepingana na hoja ya kuwaita vijana bomu kila siku? Na kisa kasema flani? Lazima umtukane nape na kumwita mbumbumbu ndio siku yako iende?... Serikali imetoa takwimu za hali halisi ya ajira nchini, nikatakiwa kutoa maoni, nilichojibu kuwa serikali iko sahihi, hali ya ajira nchini kwa takwimu sio maneno ya barabarani, na hasa ukilinganisha na nchi hata za Afrika mashariki tu Tanzania ni bora kuliko zingine, umbumbumbu wa Nape uko wapi?

Nadhani ni vizuri pamoja na kutakiwa kutukana kila unapokuta jina la Nape, akili za kuambiwa changanya na zako....
.........shida yako huwa ni Lowasa sio ufisadi, let my comments be reserved, ni suala la wakati tu.
 
nape ni mbumbumbu,na nadhani si kijana.sisi hatukaki takwimu tunajua vijana wako mtaani hawana ajira na ni wasomi na shahada zao.sio wewe umepewa kazi kwa ajili ya baba yako nauye.naichukia ccm na lazima nirudishe kadi yao.
na hili wizara ya kazi na vijana ifutwe baada ya kuongea ukweli wanapika takwimu.
 
Mkuu Nape kuna wale vijana (watoto) ambao wako kwenye traffic lights DSM. Ukisimamisha gari wanakimbilia kuchafua kioo cha gari (wind screen) then wanafuta ili uwape kamshiko kidogo. je wale CCM haioni kuwa ni nuclear bomb ambalo limeshaanza kuvuja na atahri zake zitaanza soon maana wataanza kutukaba mitaani??

Je CCM inaiambia nini serikali yake kuhusu hawa watoto??? (naamini hata wewe umeshawaona pale morocco ukiwa unaenda barber shop yako pale victoria)
 
[QUOTEa=Nnauye jJr;3546934]Nilichokurupuka ni kipi? au kwasababu nimepingana na hoja ya kuwaita vijana bomu kila siku? Na kisa kasema flani? Lazima umtukane nape na kumwita mbumbumbu ndio siku yako iende?... Serikali imetoa takwimu za hali halisi ya ajira nchini, nikatakiwa kutoa maoni, nilichojibu kuwa serikali iko sahihi, hali ya ajira nchini kwa takwimu sio maneno ya barabarani, na hasa ukilinganisha na nchi hata za Afrika mashariki tu Tanzania ni bora kuliko zingine, umbumbumbu wa Nape uko wapi?

Nadhani ni vizuri pamoja na kutakiwa kutukana kila unapokuta jina la Nape, akili za kuambiwa changanya na zako....[/QUOTE]

wewe nape acha kuchezea akili na maisha yetu!.hapa tz watu hatuna ajira hadi sasa maisha n magumu kila kukicha bcoz of ninyi ccm kushndwa kazi ya kusimamia serikali na rasilimali zilizopo.nape mnaongoza kwa rushwa,kubebana,kutudharau watz,porojo na ubabaishaji wa hali ya juu!.na kama mtaendelea kulifumbia macho hili suala la ajira bomu ni lazma lilipuke!na tena tumewachoka sana ninyi mafisadi ccm na 2015 lazima mtabeba virago vyenu.tunataka ajira sis wananchi na siyo danadana zenu hizo!
 
nnauye amjia juu lowassa

waandishi wetu | mwananchi | march 22, 2012

katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi (ccm), nape nnauye amemtaka waziri mkuu aliyejiuzulu, edward lowassa kueleza jinsi alivyoshughulikia kutatua tatizo la ajira wakati akiwa waziri mkuu.

Kauli hiyo ya nnauye inakuja siku moja baada ya waziri wa kazi na ajira, gaudencia kabaka kueleza kwamba tatizo hilo haliwezi kufafanishwa na bomu na kufafanua kuwa wanaosambaza uvumi huo hawaitendei haki serikali.
“kila siku wanalalamika serikali ya ccm inatengeneza bomu katika suala la ajira, lakini hao wanaolalamika si walikuamo madarakani na walifanya nini.

“unapofika wakati unazungumzia masuala yanayogusa jamii na taifa kwa ujumla unapaswa kuwa na uhakikika na unachokisema sio kupita katika makanisa kuongea kitu ambacho huna uhakika. “amekuwa akitumia njia mbalimbali hususan makanisani kuelezea tatizo la ajira ambalo linaitatiza serikali, lakini mimi nabaki na msimamo ule ule kuwa yeye alipokuwa serikalini (waziri mkuu) alifanya nini kutatua tatizo la ajira,” alihoji tena.

Tucta
katibu mkuu wa chama cha wafanyakazi (tucta), nicolas mgaya alisema suala la ajira bado ni tatizo kwa serikali na kwamba linapaswa kutatuliwa.

Mgaya alisema kuna vijana wengi wanahitimu masomo katika kila fani kwamba kupata kazi ni tatizo ambalo kama litasimamiwa ipasavyo litapungua.

Mgaya alisema serikalini kuna upungufu wa wafanyakazi, lakini inashindwa kuajiri, sasa umefika wakati wa kuziba mapengo hayo na kuwaondoa vijana walioko mitaani bila ajira.

“katika shule za msingi na sekondari kuna upungufu wa walimu, lakini majumbani kwetu kuna vijana waliohitimu masomo ya ualimu hawajaajiriwa sasa hapa serikali inataka kutatua ama inaongeza matatizo,” alihoji mgaya.


my take:
hawa ccm wanataka tuwaelewe vipi kujibizana wenyewe kwa wenyewe?? Hivi majibu haya ya nape yanaonyesha nini katika ushiriki wa lowasa kwenye kampeni arumeru ikiwa ataamua kwenda????

naipenda hii---hii safi sanaaaaaa......waache wachakachuane wenyewe kisha wagambuane wenyewe .....ili tujue magamba ni yapi na mafisadi papa na nyangumi ni yapi?????
 
hahaha! Kwa nini mwende bot? Nendeni pale lumumba mkawakute kina nnauye na makamba wa dunia hii, nape anajidai kupambana na ufisadi wakati yeye mwenyewe anaishi kifisadi, anatembelea v8 mjini wakati makatibu wa ccm vijini hawana hata baiskeli,!

we we thomas nathan isije ikawa unamjibu nape huku rohoni mwako unamfagilia louasa!!!!
 
Mkuu NAPE HESHIMA YAKO..........
ETI NIMESIKIA MHESHIMIWA EDO ANASEMA YEYE AMEFANYA KAZI NA MZEE MNAUYE KWA MUDA MREFU LAKINI HAJAWAHI KUTAMBULISHWA KAMA WEWE NI MWANA FAMILIA YAKE....... KWA HIYO UNATUMIA JINA HILO KUJINUFAISHA KISIASA....... TAFADHARI TUNAOMBA JIBU!!!!
This is hilarious!
 
Mchemba, Nape and Lowassa are the news makers of Tanzania!! Hawa jamaa wakisema kitu Tanzania nzima inahamia kwao! sijui kwa nini??
 
Kutegemea serikali itoe ajira kwa lundo la vijana wanaozagaa mitaani ni unafiki mkubwa sana, na wimbo wa wanasiasa mufilisi. Je ajira mpaka itoke serikalini? Tunalalamikia watoka nje wanaochukua ardhi yetu na kuzalisha mazao lukuki, mpaka wageni wengine kuwa wenyeviti wa vijiji, je kilimo sio ajira? Kwa nchi zilizoendelea ajira ni mpaka ile inayopelekea ulipwe mshahara kwa sababu huwezi pata ardhi nzuri ya kulima au hata kuanzisha biashara yako ya mifugo, kila eneo lina mwenyewe. Hii ni hata pale Kenya. Nilikuwa mpanda Kalemi, kule nimepewa eneo bure, gharama yangu ni kufyeka misitu tu. Vijana wenyewe tunaotaka waajiliwe ni wapi hasa? wanaelimu gani? na ni kwa nini wao hawawezi kujiajili?

Ah, vijana ni bomu, hiyo ni kweli kabisa kwa sababu ni rahisi sana kuwatumia vijana wenye uwezo finyu wa kufikiri kwa matakwa binafsi ya kisiasa wakaandamana nchi nzima kudai ajira, ambazo kwanza hawa uwezo wa kielimu, achilia mbali utashi wa kufanya kazi hizo. Watu wengi sana ni mashuhuda wa usemi usemao 'kama unayataka mali, utayapata shabani, kwa kujibidisha na kuwa makini kwa kile unachofanya.

Mkuu uko sawa serikali haiwezi kutoa ajira kwa vijana wote.. Lakini Serikali inatakiwa kutengeneza mfumo mzuri ambao utawasaidia kuwapa ajira vijana. Umetaja watu wanaotoka nje na kuja kuchukua ardhi hapa.. bt ukumbuke kwamba ardhi hiyo inatolewa katika mazingira ya rushwa.. Tumeona mara ngapi “wawekezaji” wakipewa ardhi na viongozi wa serikali huku wananchi waliokuwapo kwenye ardhi hiyo wakitolewa kwa nguvu..? Kwa maana nyingine wananchi wanazidi kunyang’anywa ajira na Serikali yao wenyewe..! Wataenda wapi hawa wananchi ambao walijiajiri katika ardhi yao lkn sasa wamefukuzwa..? Huo msemo kama unataka mali uende shambani ni shamba gani hilo sasa kama ardhi zinachukuliwa na “wawekezaji” uchwara na nyingine kuhodhiwa na hao hao viongozi wa Serikali..? aliunasema ulipelekwa Kalemi na kupewa eneo bure.. Umecikia wapi cku hizi hapa Tanzania unapelekwa mahali na kupewa eneo bure ili ulime..? ilkuwa enzi hizo na sio sasa Mkuu.. Wapende wasipende Serikali itengeneze mfumo mpana wa kuwawezesha vijana wenye elimu na wasio na elimu waweze kujiajiri wenyewe.. na haswa kwenye sekta ya kilimo..
 
Haya mengine ya Arumeru Mashariki, najua ni hasira zakushindwa kutakakowakuta, na najua itakuwa aibu kubwa kwa magwanda, si vibaya mkitanguliza hasira zenu kwangu maana mie ndo punching bag.....
Ndugu N. N, nadhani sasa tumekuwa taifa la wanajim au maigizo. Umejuwa mmeshinda siku nane kabla? Au kura zimeishapigwa na hesabu yake tayari? Hivi watakaoenda kupiga kura 1 April watakuwa ni wajinga as far as Fools day is concern?
Umenikumbusha, hivi yale tuliyokuwa tukivaa wakati ule wa "chipukizi" yalikuwa yanaitwaje tena? Yale juu kijani, chini nyeusi.
 
Maisha yamebadilika sana Nape, si kwa Tz tu bali ni kwa nchi zote duniani. Watznia wa miaka hii sio wale wa enzi hizo, hapana! Watznia wa leo ni watu ambao wanataka kuona kile walichoahidiwa na viongozi wao kinafanyika, kinatekelezwa na kionekane kiuhalisia sio tu kuja na takwimu ambazo ziko tofauti kabisa na hali halisi ilivyo na ukategemea kwamba wa2 watakuamini kiurahisi, hakuna! Viongozi we2 wanapaswa kubadilika kwa kiasi kikubwa sana! Watznia tunataka vitendo na sio maneno ama takwimu za kupika!

Napeeeeeee!!!!! Poloniu unaijua lakini au unajilengesha upate ofa ya kwenda kulala kitanda cha bure udosini
 
Hivi Nape wale mliowapa muda wa kujivua gamba,tayari wameshajivua gamba? baada ya bw.Rostam
je waliosalia wamejivua?au magamba yao ni magumu sana hayavuliki!! Je huo sio unafiki mnaotufanyia
watanzania juu ya kujivua gamba,halafu mmekuwa kimya mnaendeleza ufisadi?

RA alionewa zaidi kwasababu ni muislam, ndo magamba hao.
 
kimsingi hoja ya NAPE ni ya maana na yenye ukweli inayotokana na mawazo huru ya mtu wa kada yake.,katika namna zote tutakazoamua kutafsiri kauli ya EDO kuwa serikali inajiandalia bomu juu ya issue ya ajira kwa vijana ni wazi tutakuja ku-conclude kuwa ni uzandiki.

Zipo facts katika kulielezea hilo;

1) Ukichukua background ya EDO serikalini kabla na hata baada ya kuwa waziri mkuu, utagundua kuwa alikuwa katika nafasi kubwa za kimaamuzi na ushauri ambapo suala hili kama angelikuwa anataka kulishughulikia basi leo hii kusingelikuwa na tatizo la ajira katika Tanzania. Lakini ni wazi kuwa hakuwa tayari na hakuona umuhimu wa kulishughulikia hili na wala halikuwa miongoni mwa ajenda zinazomkera kama kiongozi ili kusaidia vijana ambao ndio wengi wanalalamika juu ya ukosefu wa ajira.

2) Ukiachilia mbali nafasi zake katika serikali wakati wa nyuma na sasa, bado EDO ni miongoni mwa watanzania matajiri. Anao uwezo wa kuonyesha personal initiative katika hili kama akiamua kuwekeza hapa nchini. Anao uwezo wa kuwekeza katika industry tofauti ambapo ataweza kuchukua idadi kubwa ya vijana kama rasilimali watu ambapo atakuwa amefanya jambo la msingi.

3)Pia kutokana na nafasi aliyonayo katika jamii kutokana na uzoefu wake alionao katika serikali yetu angestahiki kabisa kuwa mshauri kwa yale aliyoyagundua baada ya kuwa nje ya serikali juu ya uboreshaji wa ajira kwani si kweli kuwa juhudi hazifanyiki bali uboreshaji ndio unaohitajika.Lakini kinyume chake naalivyofanya je jamii imtazame katika jicho lipi la Unafiki au la utendaji? kwa mtazamo wangu atajiweka katika kundi la unafiki kwani alikuwemo kwa muda mrefu na hakuling'amua hilo mpaka alipofika nje?

Mkuu,

Maandishi yanaonyesha umeenda shule ila TUMBO linajitahidi kufikiri kuliko kichwa kwa sasa.

EDO kaondoka madarakani 4 (FOUR) years AGO. Kwa muda huo hata kama alikua na mipango lazima imeshafifia au haiwezi kuonekana kwani ongezeko kutoka tu vyuo vikuu ni kubwa mno!.

Suala la ajira kwa vijana ni a TIME BOMB kwa nchi nyingi sana Tanzania is no exception, EDO kuliongelea kakosea nini?

Ukiwa kiongozi uliewahi kuwa madarakani serikalini haipaswi kushutumu/kukosoa/kushauri/kukemea chochote serikalini?

Kuna sehemu gani maalum iliyotengwa ya viongozi wastaafu/waliojiuzulu kusemea matatizo wanayoyaona yapo kwa sasa serikalini?

Asante
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom