BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Nape Nnauye aitambuka Umoja wa Vijana akata rufaa CCM
Na Kizitto Noya | Mwananchi
BAADA ya kimya cha muda, mgombea uenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UV-CCM), Nape Nnauye ameibuka tena baada ya kukata rufaa CCM kupinga maamuzi ya Baraza Kuu la umoja huo ya kumvua uanachama.
Nape alikuwa gumzo kubwa wakati CCM ilipoitisha vikao vyake vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) baada ya kuvuliwa uanachama baraza hilo kutokana na kuilaumu jumuiya hiyo ya vijana ya chama tawala kuingia mkataba usio na maslahi kwa chama wa uwekezaji wa jengo la makao makuu ya UV-CCM.
Baraza hilo, ambalo lilimtia hatiani kwa kusema uongozi, lilisema uamuzi wake ni wa mwisho, huku katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba akieleza kuwa hawezi kukata rufaa "mbinguni na duniani" kabla ya Rais Jakaya Kikwete kuieleza NEC kuwa Nape anaweza kukata rufaa na kuzima mgogoro ulioonekana kuanza kuwa mkubwa.
Akizungumza na Mwananchi jana, Nape alisema kuwa amewasilisha rufaa yake CCM badala ya mwenyekiti wa UV-CCM, akisema kuwa hawezi kuirejesha rufaa hiyo kwenye kikao kilichomwadhibu.
"Ni kweli nimekata rufaa lakini rufaa hiyo nimeiwasilisha kwenye chama na sio UV-CCM kwa kwa kuwa siwezi kuipeleka kesi ya nyani kwa ngedere," alisema mtoto huyo wa mwanasiasa maarufu wa zamani wa CCM, Moses Nnauye.
Nape aligoma kutaja tarehe badala yake alisisitiza kuwa ameipeleka na anaamini itafanyiwa kazi kwa muda muafaka.
"Nisingependa kwenda mbali... elewa tu kwamba nimekata rufaa kwenye chama na sio UVCCM," alisema alipoulizwa aliwasilisha lini rufaa hiyo lakini akaongeza kusema:
"Naamini adhabu itabatilishwa na haki itatendeka."
Akimwaga sera zake wakati wa kuchukua fomu ya kugombea uenyekiti wa UV-CCM, Nape alimwaga shutuma nzito dhidi ya viongozi wa juu wa CCM, akiwemo waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa, mwenyekiti wa umoja huo, Emmanuel Nchimbi na katibu wa jumuiya hiyo kuwa walihusika katika kuingia mkataba ambao hauna maslahi kwa chama.
Nape, ambaye alishindwa na Nchimbi kwenye kinyang'anyiro cha uenyekiti wa UV-CCM, pia alisema mkataba huo wa uwekezaji wa jengo la ofisi za makao makuu ya jumuiya, haukupitishwa na vikao halali vya umoja huo.
Hata hivyo, Nchimbi alijibu tuhuma hizo kuwa mkataba huo ulipitishwa kwenye vikao halali na kwamba una maslahi kwa jumuiya hiyo.
Hata hivyo, Kamati Kuu ya CCM iliunda tume ya watu watatu ambayo imepewa jukumu la kuhakikisha kuwa maslahi ya UV-CCM yanazingatiwa katika mkataba huo baada ya kuliangalia kwa makini suala hilo kwenye kikao chake kilichofanyika Dodoma.
Na Kizitto Noya | Mwananchi
BAADA ya kimya cha muda, mgombea uenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UV-CCM), Nape Nnauye ameibuka tena baada ya kukata rufaa CCM kupinga maamuzi ya Baraza Kuu la umoja huo ya kumvua uanachama.
Nape alikuwa gumzo kubwa wakati CCM ilipoitisha vikao vyake vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) baada ya kuvuliwa uanachama baraza hilo kutokana na kuilaumu jumuiya hiyo ya vijana ya chama tawala kuingia mkataba usio na maslahi kwa chama wa uwekezaji wa jengo la makao makuu ya UV-CCM.
Baraza hilo, ambalo lilimtia hatiani kwa kusema uongozi, lilisema uamuzi wake ni wa mwisho, huku katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba akieleza kuwa hawezi kukata rufaa "mbinguni na duniani" kabla ya Rais Jakaya Kikwete kuieleza NEC kuwa Nape anaweza kukata rufaa na kuzima mgogoro ulioonekana kuanza kuwa mkubwa.
Akizungumza na Mwananchi jana, Nape alisema kuwa amewasilisha rufaa yake CCM badala ya mwenyekiti wa UV-CCM, akisema kuwa hawezi kuirejesha rufaa hiyo kwenye kikao kilichomwadhibu.
"Ni kweli nimekata rufaa lakini rufaa hiyo nimeiwasilisha kwenye chama na sio UV-CCM kwa kwa kuwa siwezi kuipeleka kesi ya nyani kwa ngedere," alisema mtoto huyo wa mwanasiasa maarufu wa zamani wa CCM, Moses Nnauye.
Nape aligoma kutaja tarehe badala yake alisisitiza kuwa ameipeleka na anaamini itafanyiwa kazi kwa muda muafaka.
"Nisingependa kwenda mbali... elewa tu kwamba nimekata rufaa kwenye chama na sio UVCCM," alisema alipoulizwa aliwasilisha lini rufaa hiyo lakini akaongeza kusema:
"Naamini adhabu itabatilishwa na haki itatendeka."
Akimwaga sera zake wakati wa kuchukua fomu ya kugombea uenyekiti wa UV-CCM, Nape alimwaga shutuma nzito dhidi ya viongozi wa juu wa CCM, akiwemo waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa, mwenyekiti wa umoja huo, Emmanuel Nchimbi na katibu wa jumuiya hiyo kuwa walihusika katika kuingia mkataba ambao hauna maslahi kwa chama.
Nape, ambaye alishindwa na Nchimbi kwenye kinyang'anyiro cha uenyekiti wa UV-CCM, pia alisema mkataba huo wa uwekezaji wa jengo la ofisi za makao makuu ya jumuiya, haukupitishwa na vikao halali vya umoja huo.
Hata hivyo, Nchimbi alijibu tuhuma hizo kuwa mkataba huo ulipitishwa kwenye vikao halali na kwamba una maslahi kwa jumuiya hiyo.
Hata hivyo, Kamati Kuu ya CCM iliunda tume ya watu watatu ambayo imepewa jukumu la kuhakikisha kuwa maslahi ya UV-CCM yanazingatiwa katika mkataba huo baada ya kuliangalia kwa makini suala hilo kwenye kikao chake kilichofanyika Dodoma.