nnunu
JF-Expert Member
- Mar 4, 2011
- 654
- 230
Hellow great thinkers,
mi ni kijana wa kitanzania (kiswahili) 23 yrs old niliyegraduate chuo mwaka jana mambo ya Logistics, i thanks God nilibahatika kupata kazi baada tu ya kumaliza chuo july last year kwenye international logistics company, na mshahara ni one million gross,
kama mnavyojua kwa wanaodeal na shipping na telecommunications industry, nikajikuta nikawa busy vibaya mno na kazi, as u know logistics sometimes unatoka saa 4, sometimes you suppose to work at weekends and public holidays( japokuwa napata sana hela za overtime na tax allowances) namshukuru mungu kwa hilo, sema kazi hii imenifanya nikose muda wa social things ambazo zinaweza kunikutanisha na mke wangu mtarajiwa like goin outing, vijiweni, movies, na other social areas, bado still nakaa home kwa wazaz so nikitoka job home, nakaa home sababu panajitosheleza na ninataka kuhama nikimaliza my own house na ni first and last born in family,
kazini natumia usafiri binafsi so kukutana kwenye daladala na woman of my life haiwezekani, enzi za chuo na shule nilikuwa somasoma niliyeogopa mahusiano sababu ya concentration kwenye masomo, kukutana nae kazini ni ngumu sabab nafanya kazi na wageni esp wafaransa, china, ghana na wengineo na sipo tayari kwa hao, ukisema kukutana facebook na social network zingine siamini hilo sababu najua ni maigizo yamejaa humo, nisaidieni wapendwa mawazo jinsi ya kukutana na woman of my life sababu nahamini now nipo tayari kwa hilo emotionally and financially, naomba msaada wa mawazo wana jamii forums wenzangu
.................................................................................................................
KWA KUSOMA MAELEZO YAKO HAPO JUU,
WEWE NI MIONGONI mwa wanaume wasiojiamni kuwa wanaweza
kupendwa wasipokuwa na vitu mkononi mwao, bali wanapendwa kwa vitu walivyonavyo. NI mwanaume usiyejua kutongoza bali unataka kutongozwa na mwanamke. Unapenda utambuliwe na upendwe kwa vitu ulivyonavyo na siyo utambuliwe kwa jinsi ulivyo kama binadamu yeyote mwenye haki ya kutambuliwa na kupendwa.
Na hata ukipata bahati ya kupendwa kwa dhati LAKIN BADO hautaamini kama unapendwa jinsi ulivyo,bali utaamini kuwa unapendwa kwa vitu ulivyonavyo.
Unapenda upendwe,uheshimike,utambulike,uthaminiwe,ujulikane,uhudumiwe kutokana na vitu ulivyonavyo na SIYO KUTOKANA hali ya kuwa wewe ni binadamu na una haki ya kufanyiwa hivyo hata pasipo kuwa na hizo mali zako.
UKIENDELEA KUTOJITAMBUA NA KUJUA THAMANI YAKO YA UANAUME, nina UHAKIKA 100% utapata hasara ya kumpata mwanamke atakayekupenda kwa vitu ulivyonavyo na siyo kukupenda wewe kama mwanaume anayekuhitaji kwa dhati toka ndani ya moyo wako.
Mwanaume anayejua UTHAMANI MKUBWA WA UANAUME WAKE KAMWE HAWEZI,
KUSEMA YOTE HAYO ULIYOYASEMA.
ila HONGERA SANA KWA MAFANIKIO YAKO ULIYOYAPATA KWA HUO MUDA MFUPI ULIONAO...HONGERA SANA ENDELEA KUFANYA KAZI KWA BIDII NA KWA MALENGO ZAIDI.
Pia nashawishika kuamini kuwa muda wa kumpata mwenza haujafika kwako, ukifika tu basi wewe binafsi utapata tu nafasi ya kumtafuta huyo mwenza, haitajalisha upo busy kiasi gani,hata kama utakuwa busy kama pua ya binadamu pindi anapokuwa hai.Ila nakukusisitiza na kukuomba sana JIAMINI /JITAMBUE NA JUA THAMANI YAKO YA UANAUME KWANZA,kwani THAMANI YA MWANAUME NI KUBWA ZAIDI YA HIVYO ULIVYOORODHESHA.....