Naongea naye nini?

Babu, mimi nilisema haya nikakumbushwa tena kwa sauti kubwa kabisa kuwa mtoto anaenda Feza, siyo shule tu ya uchochoroni. kule wanasoma watoto wa mabilionea kwa hiyo na mtoto wa Kaunga naye anatakiwa kwenda kama milionea. Well, tupo tofauti. mimi siwezi kujiita ni wa level ya chini, lakini kila ninapompeleka mwanangu shule (boarding) huwa namwuliza matron minimum amount ya kumwachia mtoto as a pocket money, najua matron angeniambia minimum ni 2M nisingeshindwa kutoa, lakini akiniambia ni elfu 20 huwa naacha elfu 20.
Huyu mtoto yupo shule..... atakula, atalala, ataingia darasani............. akiumwa atatibiwa ikishindikana nitapigiwa simu, kwa nini nimwachie laki? ataifanyia nini? si bora hiyo laki nimwekee kwa account yake ataikuta siku atakapoihitaji?
Pamoja na mzazi kumwelewa mtoto, kitu muhimu pia ni kukaa na mtoto wako na kumwelewesha. kama wazazi hatupaswi kudictate mambo, sawa, lakini tunapaswa kukaa na watoto na kuwaambia hali halisi. na huwa wanaelewa wala hawana shida


Kwa hapo tu (Blue)....naomba utegemee kupokea PM yangu muda si mrefu...Ikizingatia tuvyokaangwa huku site...Unaweza kuwa mkombozi bila kutegemea!!

Nakubaliana na wewe, watoto ni waelewa sana endapo tukiwafundisha kuelewa kwa kuwapa sababu ya kitu tunachokiongea....Nashukuru sana kwa michango yako na pia nimefurahi kwamba bado kuna wazazi wanawaona watoto kama watu wazima wa kesho ambao wanatakiwa kuwa reasonable and responsible!!

Nachukia watu wanaowadekeza watoto na kuwaona kama vile wameumbwa kwa precious metals au fragile materials!

Babu DC!!
 
Kwa hapo tu (Blue)....naomba utegemee kupokea PM yangu muda si mrefu...Ikizingatia tuvyokaangwa huku site...Unaweza kuwa mkombozi bila kutegemea!!

Nakubaliana na wewe, watoto ni waelewa sana endapo tukiwafundisha kuelewa kwa kuwapa sababu ya kitu tunachokiongea....Nashukuru sana kwa michango yako na pia nimefurahi kwamba bado kuna wazazi wanawaona watoto kama watu wazima wa kesho ambao wanatakiwa kuwa reasonable and responsible!!

Nachukia watu wanaowadekeza watoto na kuwaona kama vile wameumbwa kwa precious metals au fragile materials!

Babu DC!!
Kitu kikubwa kinanipa msukumo wa kufanya hayo ni fact kwamba sisi ni binadamu......... hatujui kesho kitatokea nini...... Hatuombei mabaya, nakiukweli naomba Mungu sana mabaya yasinikute, lakini Mungu huyo huyo ana mpango na kila binadamu, hatuwezi kubadilisha mipango yake, hakuna aliyewahi kufanya hivyo.
Hebu imagine unawalea wanao kwa mtindo huo, kesho haupo, unamuachaje mwanao? kama kuna vitu nang'ang'ania sana kwa maisha ya wanangu ni kuwawekea akiba, siyo kuwa-spoil. siku ambayo sitakuwepo, hata kama ni miaka 50-60 ijayo, watanikumbuka kwa vitu nilivyowaachia. nimeona watoto wengi wanahangaika sana wazazi wao wanapoishia, au kufilisika...... mtoto anashindwa kwenda shule sababu hawezi kulipa ada.
hata kazi za nyumbani, huwa nahakikisha wanangu wanafanya kazi, kwa kushirikiana na mimi mwenyewe na wadada wa kazi.... hakuna mtu special nyumbani kwangu, kila mtu anafanya kazi kulingana na umri na nguvu zake...... hii ni amri na inatekelezwa.
 
Aisee, kumbe sio mnyamwezi. Nilikuona siku moja unataja mitaa ya Kikungu, Ipole sijui Kanyamsenga nikaconclude utakuwa wa huko.

Au nimekosea wanyamwezi hawana dirt

Bazazi! Amejitahidi kwa msaada wa mwajiri kuitembea Tanzania yangu.
Amefika Sikonge,
Amefika Tabora Mjini,
Amefika Kibondo (siku hizi Kakonko),
Amefika Rufiji (Ikwiriri)
Amefika Morogoro Mjini​
Orodha inaenda na kuenda.

Ni hayo Kaunga!
BAzazi!
 
Last edited by a moderator:
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom