"Naongea na Riz1": Nusura daladala ikamatwe Arusha

Katika kile kilichoonekana kama ni muendelezo wa wananchi wa Arusha kuikataa serikali, muda mfupi uliopita dereva wa daladala iliyokuwa imesimamishwa na polisi pamoja na gari nyingine eneo la Aicc hosp, ili kupisha msafara wa makamu wa rais ambaye alikuwa anakwenda kupata lunch kibo palace hotel, alijikuta matatani baada ya kuwekwa chini ya ulinzi kwa muda.

Daladala hiyo ilikuwa inapiga wimbo wa bongo fleva unaosema "naongea na Riz1, ongea na mshua" kwa sauti ya juu sana wakati gari zilipokuwa zimesimamishwa. Alifuatwa na askari waliokuwa karibu na kumhoji sababu za kupiga wimbo huo pale na kwa sauti kubwa. Walimlazimisha azime na aseme aliyemtuma.

Hata hivyo alikubali kuzima na kukana kutumwa. Walimwacha baada ya abiria kumtetea kuwa wimbo unatoka kwenye kituo cha redio.

Duh! Kaaazi kwelikweli!?
Hivi hao polisi wanafikiri sawasawa kweli!
 
Tuwekeeni huo wimbo basi ama hata mashairi.JF ni international jamani.

Hhhah Wamechakachuaaaaaaaaa!!!!!!!!

Hizi ripoti asipuuze mshua, hali ya maisha inazidi kuwa mbaya sana. Gharama za hizo semina didimizi zingeweza kununua madawa ya kutosha zahanati zote nchini.

Yale matrekta pale Suma Jkt yatakuja kufa bila kuwafikia wakulima waliolengwa. Ayapeleke kwenye halmashauri za wilaya yakawekwe kwenye vituo vya kukodishia matrekta ili wakulima waweze kuyatumia na gharama zake zitarejea.

Awa tayari kuachana na fikra za kiswahiba za kuteua washikaji, hao ndio wana mwangusha, wengi si safi na hawezi kuwawawajibisha wanapokosea. Ona wale wajakazi wake wa karibu kabisa kama waziri wa elimu, hao wanamiliki shule, wakuu wa Bodi za Zabuni na maafisa masuhuri wa Wizara ndio wanaomiliki makampuni makubwa ya kutoa huduma serikalini.


Mwambie Mshua, kule magogoni tulidhani ndo chuo cha demokrasi, sasa imekuwa ghasi hakuna kitu pale ni mazalia ya waleta udhia katika nchi hii.


Ile aliyowaambia waache uzinzi na ulevi wa kupindukia..ina halalisha ulevi wa kiasi..mwambie Mshua akiwa Dom awe anajaribu kutembelea pale club 84. aone hao jamaa zake wanavyoviumizi vitoto vya wenzao....Spidi ya kwenda Loliondo imeficha mambo mengi sana, kama taifa linaongozwa na wanaoumwa hatima yake ni nini?


Rizi, mwambie Mshua yale maghorofa pale Moro na kule Mbezi beach tumeyaona, hakuna mtazanzania wa kawaida anaweza kufanya kufuru za jinsi hii, kama ni wewe plisi, punguza hiyo kasi Rizi...Sijui lakini kama unakumbuka zile siku ulizotoa za kutaka kuombwa radhi kwa kuchafuliwa,?? tunaona kama zimekwisha na kimya kizito...au ilikuwa stahili ya magamba ...
 
Back
Top Bottom