gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,673
Wana jf naombeni ushauri jamani, kama nilivyowaambia jana kuwa nimejifungua jana mtoto wa kiume kwenye thre yangu, nashukuru sana kwa wote walionitumia salam za pongezi , nasema tu mbarikiwe sana. sasa leo nakuja na ishu hii naomba ushauri jamani.
leo mchana nitakuwa nitaruhusiwa kurudi nyumbani kwania hali yangu na mtoto ni nzuri kabisa, ila napata utata sijui nikifika nyumbani wanangu wengine nitafanyaje.
ninao watoto wawili tayari na huyu ni wa tatu sasa nilishazoea sana kulala pamoja na wanangu, na huwez kuamini jinsi ambavyo wako karibu na mimi sasa leo hii naenda na kichanga na kulala nao siwez tena,je nitawatoaje chumbani kwangu ili wasione kuwa nimewabagua? swali la pili nifanyeje ili hawa wakubwa manake wanauwezo wa kugundua mambo kwa sasa wasione kama nampendelea huyu mdogo? nauliza kwani jana baba yao alinunua zawadi za mtoto mdogo walimfurahia sana kwani walijua ni za kwao, sasa walipoambiwa kuwa ni za mtoto mpya anakuja na mama kesho(leo) walikwazika sana wakasema mbona wao hawapendwi tena kama huyu mpya. na walidiriki kusema sisi tutampiga huyu labda mama asimlete. jamani nimejikuta nakosa raha sana sijui tulikosea wapi na kwasasa turekebishe vipi.
call me mama triple'G'
leo mchana nitakuwa nitaruhusiwa kurudi nyumbani kwania hali yangu na mtoto ni nzuri kabisa, ila napata utata sijui nikifika nyumbani wanangu wengine nitafanyaje.
ninao watoto wawili tayari na huyu ni wa tatu sasa nilishazoea sana kulala pamoja na wanangu, na huwez kuamini jinsi ambavyo wako karibu na mimi sasa leo hii naenda na kichanga na kulala nao siwez tena,je nitawatoaje chumbani kwangu ili wasione kuwa nimewabagua? swali la pili nifanyeje ili hawa wakubwa manake wanauwezo wa kugundua mambo kwa sasa wasione kama nampendelea huyu mdogo? nauliza kwani jana baba yao alinunua zawadi za mtoto mdogo walimfurahia sana kwani walijua ni za kwao, sasa walipoambiwa kuwa ni za mtoto mpya anakuja na mama kesho(leo) walikwazika sana wakasema mbona wao hawapendwi tena kama huyu mpya. na walidiriki kusema sisi tutampiga huyu labda mama asimlete. jamani nimejikuta nakosa raha sana sijui tulikosea wapi na kwasasa turekebishe vipi.
call me mama triple'G'