Naombeni ushauri; kutoka ualimu kuingia kwenye siasa

Kiba

JF-Expert Member
Mar 23, 2012
459
62
Ni mara yangu ya kwanza kuomba ushauri kabla ya kuomba ushauri pia kwa jamii inayonizunguka.

Ninachomba ushauri ni kuhusu jinsi nitakavyoweza kufikia ndoto yangu ya kuama kutoka katika ualimu na kuamia siasa sana sana udiwani kutokana jinsi nilivyoipata elimu na ugumu wa elimu ulivyo katika eneo nililozalia.

Kutokana na ugumu huu mimi baada ya kupelekwa katika mkoa wa Mwanza nilifika na punde kuamia private lengo ili nirudi katika kata niliyozaliwa as a new hope hadi sasa nawaza ni jinsi gani nitaamua kutoa uamuzi wangu infront of the mass muda huu muafaka kabla ili nianze kujipanga mapema ila nashindwa kujua je nini ushauri wa Watanzania wote juu yangu hila kwakua naamini MUNGU yu juu ya maisha yangu niliamua kuanza na udiwani baada ya hapo MUNGU atapanga.

Hivyo basi naomba wanda jamii ushauri wenu wa njia yeyote maana naamini mawazo ninayohitaji ni ya watanzania wote asanteni sana I waiting for positive response please.
 
Kupanga ni kuchagua, kuliko kulalamika mshshara mdogo ukilinganisha na wana siasa, fanya siasa km wananchi wanakukubali. Lkn siasa ina challenges, baadhi ya wapiga kura watakutegemea uwasomeshee watoto, uwape msaada wa wake zao wanaotaka kujifungua. Kifupi utafanya kazi za individuals zaidi kuliko za community
 
kama huna element za fitina..usiingie kwenye siasa za bongo.. utakufa kwa presha
 
Kupanga ni kuchagua, kuliko kulalamika mshshara mdogo ukilinganisha na wana siasa, fanya siasa km wananchi wanakukubali. Lkn siasa ina challenges, baadhi ya wapiga kura watakutegemea uwasomeshee watoto, uwape msaada wa wake zao wanaotaka kujifungua. Kifupi utafanya kazi za individuals zaidi kuliko za community

asante sana
 
...natamani niseme sawa ingia kwenye siasa, ila ningekushauri kwanza ufanye kautafiti kiasi.
Wakati mwingine waweza kupoteza mwelekeo kabisa kama hutakuwa na sosi nyingine za mapato.
Inawezekana ikawa ni rahisi kama utawaangalia waliofanikiwa tu pasi na kuangalia walioanguka.
Kuna jirani yangu ameuza karibu kila kitu kwa sababu ya siasa.
Wazo zuri ila fanya utafiti wa kutosha hasa kuusu kukubalika kwako huko unakotaka kwenda na mengine pia
 
mbunge analipwa zaidi ya shs million 10...wakati nyie walimu mnalipwa laki 2 yaani nakuunga mkono kabisa ingia kwenye siasa ukale nao pamoja pale dodoma...wahenga wanasema if you cant beat them you might as well join them
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom