Naombeni Ufafanuzi wa kisheria-Jinai

Lizy

JF-Expert Member
Feb 11, 2008
412
289
Habari zetu wana JF;

Naombeni msaada wenu katika suala zima la sheria za jinai.

Ninasikia kwamba sheria huwa zinabadilishwa kutokana na sababu moja ama nyingine. Kwamba kitendo fulani huenda kilikuwa kosa la kisheria kipindi flani, na hukumu yake ilikuwa hivi ama vile. Baada ya mabadiliko ya sheria kutokana na sababu kadha wa kadha, kitendo hicho endapo kitatendwa hakitakuwa kosa tena ama basi kitaendelea kuwa kosa, LAKINI hukumu yake itakuwa hivi ama vile (tofauti na ilivyokuwa mwanzo).

Swali langu; MFANO:
Kwa kipindi flani labda kosa la wizi (wa kawaida) kwa sheria za jinai za kipindi flani hukumu yake ilikuwa Miaka mitano gerezani. Wakati huo, A alitenda kosa la wizi na akahukumiwa kwenda gerezani kutumikia kifungo cha Miaka mitano. A, akiwa gerezani na amekwishatumikia miaka mitatu tayari, hukumu ya sheria hiyo ya wizi ikabadilika, kwamba endapo mtu atapatikana na hatia, hukumu yake itakuwa kifungo cha miaka miwili gerezani.

Swali; Je A ambaye alihukumiwa kwenda jela miaka mitano kipindi hicho, na tayari amekwisha tumikia miaka mitatu gerezani, atakuwa affected kwa namna yoyote na sheria mpya au vile alihukumiwa kabla ya mabadiliko ya sheria itabidi atumikie kifungo chake cha miaka mitano?

Kama jibu ni NDIO kwa swali la kwanza, kwamba atumikie vile alihukumiwa kabla ya badiliko la sheria. Vipi kuhusu kosa la Mauaji ya kukusudia, ambapo B (muuaji) alihukumiwa kifungo cha Kunyongwa mpaka kufa kwa kosa la Mauaji ya kukusudia. Then B akiwa kifungoni kusubiri kunyongwa mpaka kufa, sheria ya Haki za binadamu ikaingilia kati kwamba 'Kila mwanadamu ana haki ya kuishi, na kwamba sheria ya kunyonga mpaka kufa ni batili', kwa pressure kutoka haki za binadamu, Sheria ya kunyongwa mpaka kufa ikafutwa/badilishwa kuwa kifungo cha maisha ama vinginevyo.

Swali; Je, B kama alivyokuwa A kwenye kesi ya wizi hapo juu, ataangukia kwenye sheria mpya au vile alishahukumiwa kunyongwa mpaka kufa kabla ya sheria kufutwa/badilishwa, itabadi akamilishe kifungo chake (anyongwe mpaka kufa)?

Nawashukuru kwa muda wenu, naombeni ufafanuzi tafadhali.

LizY.
 
Kwa kesi ya A:
…Nyama ikishafika Buchani Hairudi tena kuwa Ng'ombe…
…Zege likishakorogwa halirudi kuwa sementi…
…Tunda likidondoka halirudi tena mtini…
…Maneno yakishatamkwa hayarudi tena mdomonii...

....Niliyoyaandika nimeandika (Ponsio Pilato)…

Hitimisho:
Uelewa wangu mdogo, A ataendelea kula mvua zake 5, ila iwapo akitoka nje na kurudia kosa lile basi atahukumiwa kwa miaka 3,

Maelezo ya hapo juu yanajitosheleza kueleza na kutoa jibu la la ufafanuzi kijamii na kisheria!

Kwa kesi ya B:
Katika hilo iwapo shinikizo toka haki za Binadamu litatoka baada ya hukumu litakuwa ni Butu. Sheria itachukua mkondo wake, zuio lilipashwa kupiganiwa kabla ili kuiua sheria kwanza. La, Sheria iliyohukumu ni Halali kutekelezwa kama ilivyo kwani hat kupigania na kudai kuwa ni batili hakusaidii kwani utungwaji, upitishaji na uidhinishaji wa sheria na ubadilishaji au marekebisho yake una utaratibu mahususi ambao pia nao umewekwa kisheria kwa kuzingatiwa.
 
Habari zetu wana JF;

Naombeni msaada wenu katika suala zima la sheria za jinai.

Ninasikia kwamba sheria huwa zinabadilishwa kutokana na sababu moja ama nyingine. Kwamba kitendo fulani huenda kilikuwa kosa la kisheria kipindi flani, na hukumu yake ilikuwa hivi ama vile. Baada ya mabadiliko ya sheria kutokana na sababu kadha wa kadha, kitendo hicho endapo kitatendwa hakitakuwa kosa tena ama basi kitaendelea kuwa kosa, LAKINI hukumu yake itakuwa hivi ama vile (tofauti na ilivyokuwa mwanzo).

Swali langu; MFANO:
Kwa kipindi flani labda kosa la wizi (wa kawaida) kwa sheria za jinai za kipindi flani hukumu yake ilikuwa Miaka mitano gerezani. Wakati huo, A alitenda kosa la wizi na akahukumiwa kwenda gerezani kutumikia kifungo cha Miaka mitano. A, akiwa gerezani na amekwishatumikia miaka mitatu tayari, hukumu ya sheria hiyo ya wizi ikabadilika, kwamba endapo mtu atapatikana na hatia, hukumu yake itakuwa kifungo cha miaka miwili gerezani.

Swali; Je A ambaye alihukumiwa kwenda jela miaka mitano kipindi hicho, na tayari amekwisha tumikia miaka mitatu gerezani, atakuwa affected kwa namna yoyote na sheria mpya au vile alihukumiwa kabla ya mabadiliko ya sheria itabidi atumikie kifungo chake cha miaka mitano?

Kama jibu ni NDIO kwa swali la kwanza, kwamba atumikie vile alihukumiwa kabla ya badiliko la sheria. Vipi kuhusu kosa la Mauaji ya kukusudia, ambapo B (muuaji) alihukumiwa kifungo cha Kunyongwa mpaka kufa kwa kosa la Mauaji ya kukusudia. Then B akiwa kifungoni kusubiri kunyongwa mpaka kufa, sheria ya Haki za binadamu ikaingilia kati kwamba 'Kila mwanadamu ana haki ya kuishi, na kwamba sheria ya kunyonga mpaka kufa ni batili', kwa pressure kutoka haki za binadamu, Sheria ya kunyongwa mpaka kufa ikafutwa/badilishwa kuwa kifungo cha maisha ama vinginevyo.

Swali; Je, B kama alivyokuwa A kwenye kesi ya wizi hapo juu, ataangukia kwenye sheria mpya au vile alishahukumiwa kunyongwa mpaka kufa kabla ya sheria kufutwa/badilishwa, itabadi akamilishe kifungo chake (anyongwe mpaka kufa)?

Nawashukuru kwa muda wenu, naombeni ufafanuzi tafadhali.

LizY.

Lizy, sina majibu kwa maswali ya msingi uliyo uliza, ila nina swali juu ya swali lako... Ni kwamba, je sheria inapotungwa/badilishwa huwa haisemi ni kipindi gani cha nyuma (au cha mbele) inacho cover?
 
Sehemu ya kwanza imejibiwa vema na waliotangulia hapo juu.

Adhabu ya kifo:

Ingawa mie sio mwanasheria,nitajibu vile ninavyofahamu tu.

Tofauti na adhabu nyingine (kama kifungo nk), adhabu ya kifo haiwezi kutekelezwa mpaka Rais atoe ruhusa. Kisheria Rais halazimiki kutoa ruksa hiyo.Infact, anaweza kusamehe (au kubadili adhabu) kama anaona inafaa. Ndio maana mpaka sasa wote waliohukumiwa kunyongwa kipindi cha Ben na sasa JK bado hawajanyongwa! (Mara ya mwisho adhabu ya kifo ilitekelezwa mwaka 1994).

Kwa kifupi, hukumu ya kifo sio lazima itekelezwe (kwa sababu Rais halazimishwi kutoa ruksa ya kunyonga). Hivyo kujibu swali lako, hata kama sheria itabadilika, most likely Rais akatoa uamuzi ambao utaenda sambamba na sheria mpya (say 'kifungo cha maisha').
 
Lizy, sina majibu kwa maswali ya msingi uliyo uliza, ila nina swali juu ya swali lako... Ni kwamba, je sheria inapotungwa/badilishwa huwa haisemi ni kipindi gani cha nyuma (au cha mbele) inacho cover?

Steve, ni nini lkn na wewe jamani, badala ya kunijibu unaniuliza tena maswali mwe!

Ref SMU reply hapo juu. Kama alivyosema, kwa makosa mengineyo tofauti na Mauaji ya kukusudia, mshtakiwa ataendelea kutumikia kifungo chake kwa hukumu iliyokuwa inafunction at the time of her/sentence. Mostly, endapo hukumu ya makosa ya namna kama yake itapunguzwa wakati yeye akiwa kifungoni, anaweza kuponea kwenye the so called "Msamaha wa Rais", though not guaranteed. Sorry for her/him.

Kwa Mauaji ya kukusudia, I agree with SMU. Mahakama yenyewe ilishatoa hukumu by that time kunyongwa ikiwa hukumu, bado ni Rais atatakiwa kuhalalisha kwa kusign utekelezaji. So kwa wale waliokuwa wamehukumiwa hivo (kunyongwa) will automatically fall under the new system (Imprisonment of life sentence) though hukumu yao itaendelea kusomeka Kunyongwa mpaka kufa.

Look, sheria zinatofautiana nchi na nchi.

I wish ningeeleza zaidi ya hayo, ila ndo hivo mwenyewe ni kitu inayonichanganya. Nitajitahidi nikipata DESA somewhere nitaleta, though...

As at now, I stand to be corrected kwa hayo niliyosema.

Thanks.
 
ndugu hebu nikusaidie kidogi
mimi ni mwanasheria, kwanza lazima uelewe kuwa sheria haitumikini kurudi nyuma(RESTROSPECTIVE).mfano.sheria iliyopitishwa ya law school of tanzania inawabana wale wote wahitimu wa kuanzia mwaka 2007,mimi nilishamaliza kabla ya hapo na haikunilazimisha kwwenda law school kwasababu sheria haitendi kwa kurudi nyuma.kwa kujisahidia zaidia fungua google then andika "CAN THE LAW ACT RETROSPECTIVE" Then utapata msaada zaidi ya huu. kumbuka kuwa swali lako hata yesu aliulizwa na wanafunzi wake (nashindwa kunukuu mistari due to incompitancy) ndoa ya zaidi ya wawili,nae aliwajibu kwa ufasaha. wakwmuulize je wale walioishi kwa sheria ya musa (torati) watahukumiwaje? akawajibu "walio wa torati watahukumiwa kwa torati, na walio wa injili watahukumiwa kwa injili" amina
 
kwa swali B: atatumikia kifungo sanasana kama muda wake wa rufaa umepitwa na wakati. atategea zaidi msamaha wa rais,ambao unategemea aina ya kosa.makosa yasiyo na msamaa wa rais ni pamoja na ubakaji(rape),uwizi wa kutumia silaha(armed robbery)nk
 
Back
Top Bottom