nimefeli 4m4 mwaka jana nimepata divisio 4. Naombeni msaada nijiunge na coz gani ili nipate ajira nzuri.
Nikienda kusomea travel agency ni vibaya
Dogo weka kwanza umepata Division 4 ya points ngapi??kuna watu wapo ready kukusaidia, maana ukisema tu unataka kusoma Travel Agency hatuwezi kukupa jibu wakati hatujui kama una vigezo vya kusoma hiyo course au vipi, ndio maana kuna mdau hapo juu akasema weka umepata Division 4 ya points ngapi??
nimepata ya 28
Safi! Hiyo sio mbaya Dogo, kwa mtizamo wangu unaweza kusoma vyuo vya afya kama ulipata pass kwenye masomo ya Sayansi, kwa Mfano kama ulipata D kwenye Physics, Biology na Chemistry au Maths itakusaidia sana. Pia unaweza kusoma course zenye mwelekeo wa Sayansi ya Jamii, ambazo huwa hazitegemei sana sehemu moja katika kupata ajira, kwa mfano unaweza kusoma Certificate ya Community Development na baadae ukaingia Diploma, au unaweza kwenda chuo cha St. John na ukasoma Diploma ya Project Planning and Management au ukasoma Diploma ya Laboratory technician, au Diploma ya Agriculture general.
Hizi kwa mtizamo wangu zinaweza kukusaidia sana kuendelea mbele kwani kuna baadhi ya vyuo bado wanapokea maombi mpaka sasa, hivyo jitahidi uangalie mapema kwani muda unakaribia kwisha. Huu ni ushauri wangu.