LD
JF-Expert Member
- Aug 19, 2010
- 3,014
- 574
Habari za siku nyiki wapendwa kaka na dada, nimejitokeza kwenu, kuomba ushauri na uzoefu wenu katika hali kama hii nayoisikia sasa. Sio lazima nikisema mimi iwe ndio mimi kabisa eeh. Yawezekana namwakilisha mtu ila najiita mimi. Manake wapwa hamchelewi kuunganisha dots hapa.
Mwenzenu kulikuwa na kaka mmoja, alikuaga rafiki yangu wa barua enzi zile primary na sekondari. Si haba tuliwasiliana hadi form six, wakati yeye akiwa anasoma shule tofauti kabisa na mimi. Baada ya kumaliza Form six akaenda kusoma chuo Nje ya nchi. Huko Ughaibuni.
Sasa mie si nikabaki bongo, nikajua ndio nitolee tena, sasa we majuu na mie bongo wapi na wapi. Mmmmh nikamsahau kabisa, nadhani na yeye akanishau kabisa. Nikachukulia kama ilikuwa ni utoto tu wakati huo. Uzuri au ubaya urafiki wetu haukufika mbali sana. Uliishia kwenye karatasi, kuandika kwa kalamu ya kunukia na kupulizia marashi
Sasa maisha yakaendelea hivyo, nikawa nimeingia kwenye mtandao mmoja wa kijamii, nikamuona, lakini kwa kuwa nilijua yuko majuu, mie nikaogopa hata kumwandikia. Mmmh mi nikawa nipo na jina lingine, sio jina langu halisi lililozoeleka, kwa hivyo isingekuwa rahisi kunitambua.
Mmmh siku moja nikakutana na marafiki wengine ambao tulikuwa tunasoma pamoja na huyo kaka, tukapiga stori za hapa na pale, tukikumbukia enzi za maisha ya sekondari. Mmh si tukajikuta tunamuongelea na huyu kaka. Basi yale maongezi yakapelea mimi kuamua kumwandikia yule rafiki na kujimbulisha kwake.
Uuuuh, ikawa kama sikukuu, hakuamini, loooh, kumbe alisharudi bongo na anafanya kazi hapa. He! tukapeana namba za simu. Duh roho si ikaanza kunipasuka! Duh tunachat tunapiga stori za zamani na sasa, looh moyo unanipasuka. Nikitoka ofisini nikifika nyumbani, naanza kuandika tena sms tunachat...loooh nikaanza kujistukia.
Mbona moyo unanipasuka hivi? Yani huyu kaka ndio ananipasua moyo kiasi hiki, situlii, nataka kumsikia tu, hata akiandika sms. Duh asubuhi natamani ifike niingie online nimuone.
Jamani hii hali imewahi kukuta? Na je ukiwa kama binti au kaka ulifanya je? Manake sasa najiona nitaanza kumshobokea halafu niumie. Mmmmh nikifungukaa mazima kwake itakuwa je? Duh ataniona je kwanza?
Anasomeka yuko single na mimi niko single kwa maana kwamba hata kama ana mtu sio ndio kashafanya maamuzi .........dah dah Moyo una kihere here huu. NA SIJUI yeye kama moyo wake una kihere here na mimi kiasi hiki nilicho nacho mimi. Au niendelee tu kukomaa kuwa mgumuuuuuuuuu afu anabadilika anakuwa kaka, au ananipotea tena kabisa.
Manake kwa jinsi moyo unavyonipasuka ni kwamba naweza funguka wajameni, halafu nikifunguka baadaye kitatokea nini? Si nitakuja kulia mie?
Hebu mshaurini dada yenu.
Mwenzenu kulikuwa na kaka mmoja, alikuaga rafiki yangu wa barua enzi zile primary na sekondari. Si haba tuliwasiliana hadi form six, wakati yeye akiwa anasoma shule tofauti kabisa na mimi. Baada ya kumaliza Form six akaenda kusoma chuo Nje ya nchi. Huko Ughaibuni.
Sasa mie si nikabaki bongo, nikajua ndio nitolee tena, sasa we majuu na mie bongo wapi na wapi. Mmmmh nikamsahau kabisa, nadhani na yeye akanishau kabisa. Nikachukulia kama ilikuwa ni utoto tu wakati huo. Uzuri au ubaya urafiki wetu haukufika mbali sana. Uliishia kwenye karatasi, kuandika kwa kalamu ya kunukia na kupulizia marashi
Sasa maisha yakaendelea hivyo, nikawa nimeingia kwenye mtandao mmoja wa kijamii, nikamuona, lakini kwa kuwa nilijua yuko majuu, mie nikaogopa hata kumwandikia. Mmmh mi nikawa nipo na jina lingine, sio jina langu halisi lililozoeleka, kwa hivyo isingekuwa rahisi kunitambua.
Mmmh siku moja nikakutana na marafiki wengine ambao tulikuwa tunasoma pamoja na huyo kaka, tukapiga stori za hapa na pale, tukikumbukia enzi za maisha ya sekondari. Mmh si tukajikuta tunamuongelea na huyu kaka. Basi yale maongezi yakapelea mimi kuamua kumwandikia yule rafiki na kujimbulisha kwake.
Uuuuh, ikawa kama sikukuu, hakuamini, loooh, kumbe alisharudi bongo na anafanya kazi hapa. He! tukapeana namba za simu. Duh roho si ikaanza kunipasuka! Duh tunachat tunapiga stori za zamani na sasa, looh moyo unanipasuka. Nikitoka ofisini nikifika nyumbani, naanza kuandika tena sms tunachat...loooh nikaanza kujistukia.
Mbona moyo unanipasuka hivi? Yani huyu kaka ndio ananipasua moyo kiasi hiki, situlii, nataka kumsikia tu, hata akiandika sms. Duh asubuhi natamani ifike niingie online nimuone.
Jamani hii hali imewahi kukuta? Na je ukiwa kama binti au kaka ulifanya je? Manake sasa najiona nitaanza kumshobokea halafu niumie. Mmmmh nikifungukaa mazima kwake itakuwa je? Duh ataniona je kwanza?
Anasomeka yuko single na mimi niko single kwa maana kwamba hata kama ana mtu sio ndio kashafanya maamuzi .........dah dah Moyo una kihere here huu. NA SIJUI yeye kama moyo wake una kihere here na mimi kiasi hiki nilicho nacho mimi. Au niendelee tu kukomaa kuwa mgumuuuuuuuuu afu anabadilika anakuwa kaka, au ananipotea tena kabisa.
Manake kwa jinsi moyo unavyonipasuka ni kwamba naweza funguka wajameni, halafu nikifunguka baadaye kitatokea nini? Si nitakuja kulia mie?
Hebu mshaurini dada yenu.