figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,485
- 54,855
Naomba nifundishwe kupika chai. nahita nijuie kupika kila aina ya chai. iwe ya rangi au maziwa. vilevile nahitaji kujua viungo vinavyo hitajika. ni hayo tu. mia
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Chai ya rangi: Chemsha maji kwa kiasi utakacho. Wkt maji yanachemka, tia viungo [(h)iliki, mdalasini, tangawizi -- angalia maelezo hapa chini]. Acha viungo vichanganyike na maji yachemkayo kwa km dkk 10-15. Sasa unaweza kuweka sukari ukipenda. Tia majani ya chai kidogo na acha yachanganyike na maji yachemkayo kwa km dkk 10 -- usiwache majani yachemkie kwa muda mrefu; chai inaweza kuwa chungu. Chai yako iko tayari kunywewa.
Chai ya maziwa: Ni vema kuanza kwa maji kiasi kidogo, km ktk chai ya rangi. Tia maziwa baada ya viungo kuchemkia ktk maji. Hatua nyingine ni km ktk chai ya rangi hapo juu.
Maelezo Khs Viungo:
(h)iliki - Menya maganda. Weka mbegu ktk kipande cha karatasi/kitambaa safi kisha zitwange.
tangawizi - Mbichi ni bora kuliko ya unga. Isafishe tangawizi, menya maganda kwa wembamba au para kwa kisu. Isage tangawizi ktk kiparuzio (grater). Kiasi cha tangawizi unachoweka ktk maji yachemkayo kinategemea kiasi cha ukali unachokihitaji -- kiasi kikubwa, ukali zaidi. Kumbuka pia, muda mrefu wa kuchemkia tangawizi huchangia kuongeza ukali.
mdalasini - Ni vema kuutwanga kuliko kuuweka mzima mzima. Mdalasini mzima ni bora kuliko wa uliokwishatwangwa -- Ni vema uutwange wewe mwenyewe.
Nasubiri feedback.
kumbe chai naho inautalam wacha nijaribu kumpikia my wife kesho.
jf ni kilakitu nizaidi ya darasa.mia
Chemsha maji yapate moto kisha weka kwenye kikombe halafu chukua majani ya pakti tia ndani ya kikombe chako chenye maji moto, ongeza sukari saizi yako kisha koroga..
Kwisha.....
Nilidhani chips tu...kumbe hata chainaomba nifundishwe kupika chai. nahita nijuie kupika kila aina ya chai. iwe ya rangi au maziwa. vilevile nahitaji kujua viungo vinavyo hitajika. ni hayo tu. mia
Asante kwa elimu, mimi huweka mwanzo nikidhani vitanukia sana, nimejifunzaUsiweke viungo kwenye chai wakati ipo jikoni harufu inapungua, fanya hivi.....
Twanga viungo vyako, inaweza kuwa iliki na mdalasini, vitwange vizuri kisha viweke kwenye chupa ya chai, chai ikichemka weka kwenye chupa funika.... Aseee inanukia hatareee
Hii nitafanyia kazi kuanzia leo!!Twanga viungo vyako, inaweza kuwa iliki na mdalasini, vitwange vizuri kisha viweke kwenye chupa ya chai, chai ikichemka weka kwenye chupa funika.... Aseee inanukia hatareee
Wengine hatutumii majani ya chai, kwahiyo hapo unachemsha maji tu, si ndio?Usiweke viungo kwenye chai wakati ipo jikoni harufu inapungua, fanya hivi.....
Twanga viungo vyako, inaweza kuwa iliki na mdalasini, vitwange vizuri kisha viweke kwenye chupa ya chai, chai ikichemka weka kwenye chupa funika.... Aseee inanukia hatareee
chai haipikwi ina chemshwa kama unataka kuchemsha chai ya rangi:-
Cheers ☕
uzi huu utaimarisha afya yangu nikisikia tu neno chai nahemukwaNaomba nifundishwe kupika chai. nahita nijuie kupika kila aina ya chai. iwe ya rangi au maziwa. vilevile nahitaji kujua viungo vinavyo hitajika. ni hayo tu. mia