Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo, nimelazimika kuacha kutumia gari langu binafsi kwasasa natumia daladala tuu. Nasikia kwamba gari usipoitumia mda mrefu injini huaribika sijabahatika kupata maelezo ya kiufundi inakuwaje, naomba mwenye ujuzi katika hili anipe maelezo ya kisayansi, kwasababu gari yangu naipenda sana sitaki kuiuza nataka niipaki mpaka siku mafuta yatakaposhuka bei. Na kwa wataalamu wa uchumi naombeni mnishauri kama hii subira yangu itawezekana au lah! maana kuna mtu amenikatisha sana tamaa kwamba haiwezekani mafuta kushuka bei.
Serious!!!
Serious!!!