naomba ushauri wenu

mtanzania in exile

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
1,335
1,183
Katika mwaka mmoja tu (june 2011 hadi July 2012) wake za watu watatu wamenifata kunitaka kimapenzi. Ninachotaka kujua ni kwa nini? ni kosa gani nifanyalo kiasi kuwa wake za watu wafikiri nawataka?
Wote nimewakwepa, lakini kinachonishangaza ni kwa nini hasa waache waume zao na kunifuata mimi? Wakati huo huo kuna mwanamke ambae yuko single na ananivutia mno lakini ananipiga chenga mwaka na nusu sasa na anasingizia eti ananihisi mimi ni player, jambo ambalo sio kweli kabisa!
Mmoja kati ya hawa wake za watu amefika hadi kudai kuwa anajua hasa kuwa ninamzimia, na ni woga tu ndio unaonizuia mimi kumfuata, na kwa sababu hiyo ndiyo yeye kaamua ku make the first move. Wote wamedai kuwa ucheshi wangu na tabasamu zangu niwaonapo njiani na sehemu za mikusanyiko ni ishara ya kuwa niko interested. Hilo sio kweli kwani hiyo ni hulka yangu kuwa mcheshi kwa kila nimjuae sio kwao wao tu, tabasamu kwangu ni jambo la kawaida. Daima huwa na dakika chache za kusimama kusalimiana na kuzungumza na niwajuao nikutanapo pahali popote pale.
Hivi ndugu zangu kuwa mcheshi na mchangamfu ni kosa? Huku ugenini ukianza kutokusalimia au kutotaka kujuana na watanzania wenzako ni hatari, kwani mbali ya wao kukuona kuwa unajipenda na kuwadharau wenzako pia nao watakutenga, jambo amablo sio jema hasa ukizingatia kuwa tuko mbali na familia zetu, binaadam mzima leo hujui kesho utaamkaje.
Hebu niambieni nifanyaje ili kuepukana na matatizo haya. Imeanza wake wa watu kuhisi nawataka, isije ikaja kufika waume zao kufikiria nawaibia wake zao.
 
Huyo ni roho inakuandama ya kutembea na wake za watu. Muombe Mungu akuepushe na hilo liroho akupe mchumba ambaye mtaoana.
 
Kama hufanyi makosa unawasi wasi gani.

Huyo anaye kuitwa player ungeomba kamchezo naye basi :violin:
 
Kama hufanyi makosa unawasi wasi gani.

Huyo anaye kuitwa player ungeomba kamchezo naye basi :violin:

Moyo wa binaadamu ni dhaifu, nimekataa watatu and i hope nitakuwa na moyo huo huo kama akitokea mwengine, lakini ningelipenda isiwe hivyo na ndio nikataka kujua ni lipi nifanyalo ambalo limewafanya wake za watu kunitaka.

Sasa wewe unasema nini hapo, nimekwambia aniitae player hanitaki kwa sababu anaamini kuwa mimi ni player na ndio maana hanitaki sasa kamchezo hapo nitapata vipi? vipi mshikaji ushaanza week end nini :A S 465:
 
Moyo wa binaadamu ni dhaifu, nimekataa watatu and i hope nitakuwa na moyo huo huo kama akitokea mwengine, lakini ningelipenda isiwe hivyo na ndio nikataka kujua ni lipi nifanyalo ambalo limewafanya wake za watu kunitaka.

Sasa wewe unasema nini hapo, nimekwambia aniitae player hanitaki kwa sababu anaamini kuwa mimi ni player na ndio maana hanitaki sasa kamchezo hapo nitapata vipi? vipi mshikaji ushaanza week end nini :A S 465:
Mimi nakupa njia za kumpata mana yeye anasema wewe ni player, sa mwambie twende tukacheze mana huwezi kunijua player kama hujacheza na mimi....Akijidai sijui sitaki mwambie nilidhani we ni experiance wa mchezo kuliko mimi ukanifundishe kumbe mimi na wewe wote si wachezaji....Afu utaona kama humpati.

Weekend hapa watatoto wa ki Australians mapaja wazi tu mpaa unalia wasizidi kuzikamua.
 
Katika mwaka mmoja tu (june 2011 hadi July 2012) wake za watu watatu wamenifata kunitaka kimapenzi. Ninachotaka kujua ni kwa nini? ni kosa gani nifanyalo kiasi kuwa wake za watu wafikiri nawataka?
Wote nimewakwepa, lakini kinachonishangaza ni kwa nini hasa waache waume zao na kunifuata mimi? Wakati huo huo kuna mwanamke ambae yuko single na ananivutia mno lakini ananipiga chenga mwaka na nusu sasa na anasingizia eti ananihisi mimi ni player, jambo ambalo sio kweli kabisa!
Mmoja kati ya hawa wake za watu amefika hadi kudai kuwa anajua hasa kuwa ninamzimia, na ni woga tu ndio unaonizuia mimi kumfuata, na kwa sababu hiyo ndiyo yeye kaamua ku make the first move. Wote wamedai kuwa ucheshi wangu na tabasamu zangu niwaonapo njiani na sehemu za mikusanyiko ni ishara ya kuwa niko interested. Hilo sio kweli kwani hiyo ni hulka yangu kuwa mcheshi kwa kila nimjuae sio kwao wao tu, tabasamu kwangu ni jambo la kawaida. Daima huwa na dakika chache za kusimama kusalimiana na kuzungumza na niwajuao nikutanapo pahali popote pale.
Hivi ndugu zangu kuwa mcheshi na mchangamfu ni kosa? Huku ugenini ukianza kutokusalimia au kutotaka kujuana na watanzania wenzako ni hatari, kwani mbali ya wao kukuona kuwa unajipenda na kuwadharau wenzako pia nao watakutenga, jambo amablo sio jema hasa ukizingatia kuwa tuko mbali na familia zetu, binaadam mzima leo hujui kesho utaamkaje.
Hebu niambieni nifanyaje ili kuepukana na matatizo haya. Imeanza wake wa watu kuhisi nawataka, isije ikaja kufika waume zao kufikiria nawaibia wake zao.

Pole kijana na hongera kwa kutupa clue ambazo labda zinaweza kutufanya kujaribu kukusaidia.
- Kwanza huko ugenini uliko inaonyesha jamii yenu Watanzania) mnapenda kutanua. Sijui kitu gani kinakufanyeni hivyo, sijui uhuru wa kuwa mko mbali,au hamu ya kutaka kuchanganyika na wenzako, au labda ni njia ya kupata kipato cha ziada kwa kuhongwa au sababu nyengine zozote. Kwako wewe ni kuwa muangalifu na kujaribu mahusiano ya karibu na wale wachache utakaowaona wana muelekeo wako, yaani wa kutafuta maisha ya sasa na baadae.
-Hulka yako ya kuchangamkia kila mtu inatafsiriwa vibaya na kuonekana kuwa wewe ni mmoja wa hao watanuaji (na ndio maana yule alie na msimamo kama wako pia anakutafsiri kuwa uko katika kundi). Jiangalie na jaribu kuchangamka na watu pale tu inapowajibika, nikikusudia kuepuka michanganyiko isiyo na maana.
Tahadhari: Waswahili wana msemo; "Papo kwa papo kamba hukata jiwe" nikimaanisha kuwa mazowea yatakufanya uingie mtegoni na utaserebuka nao hao wake za watu.
 
kuna watu watafikiri unatania
but mimi naamini ulichokisema
huwa inatokea kwa baadhi ya watu kuwa na mvuto na kundi fulani la jamii
mfano wapo ambao wanatongozwa na ma suger mammy tu sana
wapo wengine gays ndo wanawataka hata kama wao hawashiriki
wapo wanaopendwa na walimu wao tu
kuanzia secondary mpaka chuo mtu anatembea na walimu wake tu
mradi dunia hii haishi vituko...

na hilo la waume zao kuku mind trust me...linakuja....
 
yaani mie haya mambo ya kila kitu imekuwa roho anakuandama jamani?

Hivi ukae mkao wa kutongozwa napo usingizie roho?

Huyo ni roho inakuandama ya kutembea na wake za watu. Muombe Mungu akuepushe na hilo liroho akupe mchumba ambaye mtaoana.
 
labda una mvuto wa kimahaba? Au wanataka kukuchuna? Encelea kuwakataa na kuwa serious zaidi....kama ulikuwa na ukaribu nao punguza.....kama ulijenga mazingira hatarishi acha....
 
Ndugu yangu hayo ni yakawaida cha msingi kua na msimamo mmoja. Kisha tafuta unaempenda nae akupende asiekupenda achana nae. Ukishaoa utulie na mke wako. Huo ndio ushauri wangu
 
Mi ushauri wangu jitahidi kucheza mbali na hao mamanzi wa watu !!
na kama ni suala la uchangamfu basi changamka na wanaume wenzio.Usikute wanakutegea mtego ili wakushike ugoni then wakugonge ****, uku kwetu zipo sanaa hizo.Take care hakuna cha kuzimikiwa wala nini fatilia ushauri aliokupa
THE BOSS utu uzima dawa !!!
 
Pole kijana na hongera kwa kutupa clue ambazo labda zinaweza kutufanya kujaribu kukusaidia.
- Kwanza huko ugenini uliko inaonyesha jamii yenu Watanzania) mnapenda kutanua. Sijui kitu gani kinakufanyeni hivyo, sijui uhuru wa kuwa mko mbali,au hamu ya kutaka kuchanganyika na wenzako, au labda ni njia ya kupata kipato cha ziada kwa kuhongwa au sababu nyengine zozote. Kwako wewe ni kuwa muangalifu na kujaribu mahusiano ya karibu na wale wachache utakaowaona wana muelekeo wako, yaani wa kutafuta maisha ya sasa na baadae.
-Hulka yako ya kuchangamkia kila mtu inatafsiriwa vibaya na kuonekana kuwa wewe ni mmoja wa hao watanuaji (na ndio maana yule alie na msimamo kama wako pia anakutafsiri kuwa uko katika kundi). Jiangalie na jaribu kuchangamka na watu pale tu inapowajibika, nikikusudia kuepuka michanganyiko isiyo na maana.
Tahadhari: Waswahili wana msemo; "Papo kwa papo kamba hukata jiwe" nikimaanisha kuwa mazowea yatakufanya uingie mtegoni na utaserebuka nao hao wake za watu.

ahsante kwa ushauri wako ndugu, lakini napenda nikukosowe kidogo kuhusu hapo uliposema kuwa watu huku nje tunatanuwa sana. Hilo sio kweli na ni mawazo ya wengi wa waliopo nyumbani. Ukweli hutokea baadhi ya siku kukawepo na mikusanyiko ya hapa na pale na sio kila mwisho wa week end, mara nyingi hukuntana kwa sababu kuna jambo iwe harusi, msiba n.k hivyo ndivyo ilivyo pande hizi niliko, sijui kwengine though
 
Mimi nakupa njia za kumpata mana yeye anasema wewe ni player, sa mwambie twende tukacheze mana huwezi kunijua player kama hujacheza na mimi....Akijidai sijui sitaki mwambie nilidhani we ni experiance wa mchezo kuliko mimi ukanifundishe kumbe mimi na wewe wote si wachezaji....Afu utaona kama humpati.

Weekend hapa watatoto wa ki Australians mapaja wazi tu mpaa unalia wasizidi kuzikamua.

kwa maana hiyo unataka nimwambie kuwa nilidhani anapigisha kwa wengine, halafu unafikiri atapendezwa na kauli kama hiyo? No way, nipe ushauri mwengine
 
Kaka kuna ka msemo kanasema, Fanya kila kitu kwa kiasi... Hata kama kuwachangamkia hebu wachangamkie kidogo then endelea na mambo yako na uonyeshe wazi kwamba unachokimaanisha ni salamu tuu na si vinginevyo.. Siajabu wewe unawasabahi huku unatabasamu halafu unawatizama kwa mahaba vifuani .. Sasa hapo unategemea nin?
 
kuna watu watafikiri unatania
but mimi naamini ulichokisema
huwa inatokea kwa baadhi ya watu kuwa na mvuto na kundi fulani la jamii
mfano wapo ambao wanatongozwa na ma suger mammy tu sana
wapo wengine gays ndo wanawataka hata kama wao hawashiriki
wapo wanaopendwa na walimu wao tu
kuanzia secondary mpaka chuo mtu anatembea na walimu wake tu
mradi dunia hii haishi vituko...

na hilo la waume zao kuku mind trust me...linakuja....

Hujakosea nimeshaanza kuhisi machale ya mmoja wao.
 
The only solution ni kuacha kuchekea chekea wake za watu maana kifuatacho waume zao nao wataanza kukuchekea wewe!:evil:
 
The only solution ni kuacha kuchekea chekea wake za watu maana kifuatacho waume zao nao wataanza kukuchekea wewe!:evil:

ucheshi ni tabia yangu, natabasamu kwa yeyote nikutane nae awe mwanamme au mwanamke. kwa nini nibadili tabia njema kwa kuwa tu baadhi ya watu hawaridhiki na walio nao?
 
Back
Top Bottom