mamabaraka
Member
- Oct 18, 2011
- 92
- 14
Niliajiriwa na shirika moja yapata miezi miwili sasa kama mhasibu msaidizi. Tatizo kubwa bosi wangu aliyeniajiri haelewani na mhasibu mkuu wangu. Kisa ni kwamba bosi anapenda kutumia sana pesa mpaka sasa kuna utata kama wafanyakazi wataweza kupata mishahara mwezi June pesa hakuna. Mhasibu akimshauri bosi anakuja juu anasema aachwe atumie pesa anavyotaka yy ndo top. Kingine bosi anaiingilia ofisi ya uhasibu hata kwenye kukusanya mapato ya shirika tena hatoi risiti kwa wateja na hata kuandika majina ya wanaolipa pesa na nyingne hukusanywa na kutumiwa juu kwa juu bila kushirikisha wahasibu. Baada ya kuambiwa ukweli na mhasibu mkuu bosi amekuwa mkali ameichukia ofisi ya uhasibu na hatutambui kama wafanyakazi wake. Mi ndo kwanza nina miezi miwili kazini nimekutana na changamoto hiyo. Kibaya zaidi mhasib akimshaur na kumwambia ofisi ya uhasibu tunashauri hivi bosi huwa ananiita peke yangu na kunisema alitemea niwe upande wakena mi nakuwa hivyo!!!. Naomba ushauri wenu ndugu zangu maana kazi ni ngumu.