Naomba ushauri wenu kazi yangu ipo matatani.

mamabaraka

Member
Oct 18, 2011
92
14
Niliajiriwa na shirika moja yapata miezi miwili sasa kama mhasibu msaidizi. Tatizo kubwa bosi wangu aliyeniajiri haelewani na mhasibu mkuu wangu. Kisa ni kwamba bosi anapenda kutumia sana pesa mpaka sasa kuna utata kama wafanyakazi wataweza kupata mishahara mwezi June pesa hakuna. Mhasibu akimshauri bosi anakuja juu anasema aachwe atumie pesa anavyotaka yy ndo top. Kingine bosi anaiingilia ofisi ya uhasibu hata kwenye kukusanya mapato ya shirika tena hatoi risiti kwa wateja na hata kuandika majina ya wanaolipa pesa na nyingne hukusanywa na kutumiwa juu kwa juu bila kushirikisha wahasibu. Baada ya kuambiwa ukweli na mhasibu mkuu bosi amekuwa mkali ameichukia ofisi ya uhasibu na hatutambui kama wafanyakazi wake. Mi ndo kwanza nina miezi miwili kazini nimekutana na changamoto hiyo. Kibaya zaidi mhasib akimshaur na kumwambia ofisi ya uhasibu tunashauri hivi bosi huwa ananiita peke yangu na kunisema alitemea niwe upande wakena mi nakuwa hivyo!!!. Naomba ushauri wenu ndugu zangu maana kazi ni ngumu.
 
sasa hapa si ndo pa kulalamika jamani au umesahau miwani?Piga kazi ndugu huo ni upepo tu utapita.
 
Niliajiriwa na shirika moja yapata miezi miwili sasa kama mhasibu msaidizi. Tatizo kubwa bosi wangu aliyeniajiri haelewani na mhasibu mkuu wangu. Kisa ni kwamba bosi anapenda kutumia sana pesa mpaka sasa kuna utata kama wafanyakazi wataweza kupata mishahara mwezi June pesa hakuna. Mhasibu akimshauri bosi anakuja juu anasema aachwe atumie pesa anavyotaka yy ndo top. Kingine bosi anaiingilia ofisi ya uhasibu hata kwenye kukusanya mapato ya shirika tena hatoi risiti kwa wateja na hata kuandika majina ya wanaolipa pesa na nyingne hukusanywa na kutumiwa juu kwa juu bila kushirikisha wahasibu. Baada ya kuambiwa ukweli na mhasibu mkuu bosi amekuwa mkali ameichukia ofisi ya uhasibu na hatutambui kama wafanyakazi wake. Mi ndo kwanza nina miezi miwili kazini nimekutana na changamoto hiyo. Kibaya zaidi mhasib akimshaur na kumwambia ofisi ya uhasibu tunashauri hivi bosi huwa ananiita peke yangu na kunisema alitemea niwe upande wakena mi nakuwa hivyo!!!. Naomba ushauri wenu ndugu zangu maana kazi ni ngumu.

Pole! But hapo waweza fanya moja kati ya haya: 1.kama ulisaka kazi kwa muda mrefu hatimaye ukafanikiwa katika hilo shirika nawe unategemea hapo na huna mahala pengine pa kuongeza kipato,msapoti bosi ikiwa yeye ndo mtoaji wa mishahara ili maisha yaende but ukijua kwamba it is illegal. 2.kama shirika lazima huyo bosi zipo ngazi kumzidi,kuwa mzalendo, mchome(kama mbwai mbwai) kwan kwa kubaki kimya itaonekana nyie na bosi lenu moja na mwisho wa siku mtahusika wote kuja kutoa hesabu za zilizoliwa na bosi peke yake.kwa kufanya hivyo utakuwa umetenda haki na kutetea maslahi ya shirika hata Mungu anakuona na hatakuacha upoteze kazi kwa kutenda haki na hata hapo pakichafuka utapata pengine.
 
sasa hapa si ndo pa kulalamika jamani au umesahau miwani?Piga kazi ndugu huo ni upepo tu utapita.

Upepo utapita wakati huenda inapatikana kidogo kuliko matumizi na shirika likifilisika wao ndo watakuwa responsible hela zimeenda wapi. Ilopo angalia njia thabiti ya kujinasua maana hilo litakuwa dhoruba
 
Pole! But hapo waweza fanya moja kati ya haya: 1.kama ulisaka kazi kwa muda mrefu hatimaye ukafanikiwa katika hilo shirika nawe unategemea hapo na huna mahala pengine pa kuongeza kipato,msapoti bosi ikiwa yeye ndo mtoaji wa mishahara ili maisha yaende but ukijua kwamba it is illegal. 2.kama shirika lazima huyo bosi zipo ngazi kumzidi,kuwa mzalendo, mchome(kama mbwai mbwai) kwan kwa kubaki kimya itaonekana nyie na bosi lenu moja na mwisho wa siku mtahusika wote kuja kutoa hesabu za zilizoliwa na bosi peke yake.kwa kufanya hivyo utakuwa umetenda haki na kutetea maslahi ya shirika hata Mungu anakuona na hatakuacha upoteze kazi kwa kutenda haki na hata hapo pakichafuka utapata pengine.

Sioni kama kuna haja ya kuwa upande wa boss wakati hela hatumii nae pia shirika likifilisika ajira bado itakosekana pia kwako mhasibu msaidizi ilopo mwaga uguli kwani boss yeye keshamwaga mboga, means u have to repot to the high level
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom