Naishi na mke wangu vizuri tu siku nyingi, lakini familia yangu ni kubwa kiasi kwamba kila baada ya muda fulani napata mgeni wa kuja kututembelea. Kama ni mwanaume kidogo afadhali hata watasalimiana na atamuhudumia at least kiroho safi, mbaya zaidi ni wa jinsia ya kike. Hata kama anajua kabisa ni ndugu japo wa mbali kidogo anakuwa mzito sana kumuhudumia kwa vikwazo kibao mara oooh naumwa/sijisikii vizuri/n.k. ilihali sura ikionyesha dhahiri kwamba hajafurahia ujio wa huyo mtu.
Sasa nimepata bahati ya kuwapata watoto wawili wa kike wa kaka zangu, kutoka kijijini ili waje kujiendeleza kielimu, mmoja ni mdogo yuko darasa la II na mwingine amemaliza la saba nataka angalau apate kozi za kujiendeleza hapa mjini. Sasa wife ananambia ye ataki kuwaona la sivyo ataondoka, na nnavyoandika hapa, ameamua kuondoka kweli leo hii. Lakini siku mbili baada ya hawa watoto kufika kwangu, na mdogo wake pia ambaye amekuja kusoma chuo naye alifika kwangu na anaishi kwangu na anasoma chuo kwa gharama zangu!
Hivi ni kweli niachie hawa watoto warudi nyumbani ili nikae na mke na shemeji yangu ndani, au nimwachie mke aende sababu njia zote za kujaribu kumwelimisha mke wangu juu ya jukumu na umuhimu wangu kuwasaidia watoto hawa amezikataa, hataki kabisa kuongea juu yao.
Naomba ushauri wenu.
Sasa nimepata bahati ya kuwapata watoto wawili wa kike wa kaka zangu, kutoka kijijini ili waje kujiendeleza kielimu, mmoja ni mdogo yuko darasa la II na mwingine amemaliza la saba nataka angalau apate kozi za kujiendeleza hapa mjini. Sasa wife ananambia ye ataki kuwaona la sivyo ataondoka, na nnavyoandika hapa, ameamua kuondoka kweli leo hii. Lakini siku mbili baada ya hawa watoto kufika kwangu, na mdogo wake pia ambaye amekuja kusoma chuo naye alifika kwangu na anaishi kwangu na anasoma chuo kwa gharama zangu!
Hivi ni kweli niachie hawa watoto warudi nyumbani ili nikae na mke na shemeji yangu ndani, au nimwachie mke aende sababu njia zote za kujaribu kumwelimisha mke wangu juu ya jukumu na umuhimu wangu kuwasaidia watoto hawa amezikataa, hataki kabisa kuongea juu yao.
Naomba ushauri wenu.