Naomba ufafanuzi juu ya JK na mgogoro-Kenya

Freetown

JF-Expert Member
Apr 6, 2008
883
73
Nilisoma maoni ya wana jf walioweza kupata nafasi ya kuandika kuhusu jk kuwa ndiye aliyetatua mgogoro wa uchaguzi wa Kenya, sikuweza kusema lolote kwa wakati huo, japo nimechelewa naomba kutoa dukuduku langu.
1. Ninachojua ni kwamba pamoja na wote walioenda toka USA, Rais wa Ghana, Mkapa, na wengineo aliyewezesha hayo ni Koffi Anan, alikaa Nairobi siku 42.
2. Kikwete alikwenda kama shuhuda kwa kuwa ni mwenyekiti wa AU na si vinginevyo.
3. Ingelikuwa ni JK ndiye aliyetatua matatizo yao, mbona hawakumuita tena wakati mzozo ulipotaka kuibuka upya juu ya kugawana madaraka?? Badala yake waliomba Anan aingilie kati tena kwa kuwa ndiye wanayemjua kuwa alitatua mgogoro wa mwanzo.
4. JK alikaa mda gani??? Nairobi mpaka apewe credibility ya kuwa ndiye aliyekuwa mfumbuzi wa ule mgogoro???.KIKAO CHA CCM BUTIAMA NI SHAIDI
5. Alipoombwa atatue mzozo wa ccm na cuf mnakumbuka alijibu nini na amefanya nini katika hilo?????.
6. viongozi wetu wanapenda sifa. Angesifiwa zaidi angewajibu waandishi wa habari kuwa alienda kule kama shaidi na siyo mpatanishi kwa kuwa in mwenyekiti wa AU.
7. Wakati anakwenda Nairobi tarehe ya kusign mwafaka ilikuwa ishatajwa nay Yeye kualikwa.
8. NAOMBA KAMA KUNA MWENYE HOJA ZAIDI JUU YA HILI. LENGO NI KUJENGA SIYO KUBOMOA
 
Back
Top Bottom