Amanikwenu
Senior Member
- Dec 1, 2009
- 187
- 0
Wakuu,
Kati ya shughuli ninazozipenda sana ni kupanda miti. Mwaka huu wa 2010 nina lengo la kupanda miti ya kivuli na matunda (hasa miembe ya asili) isiyopungua 100.
Kama Wana JF naomba tuanzishe kampeni ya kitaifa kwa Wana JF kama timu kupanda miti katika sehemu maalum hapa nchini ambazo tutazichagua hasa zile ambazo ziko sehemu ya vyanzo vya maji. Kampeni hii ihusishe pia shule zetu na taasisi nyingine za elimu.
Napendekeza tuwe na lengo la kupanda angalau miti 1,000 kwa mwaka huu kama Wana JF. Wakipatikana wana JF 50 na kila mmoja akapanda miti 20 tu tutakuwa tumevuka lengo.
Napendekeza ndoto yetu kitaifa iwe ni kuona kila mwanafunzi hapa nchini anapanda angalau mti mmoja kila mwaka.
Nchi yetu kwa sasa ina Wanafunzi katika ngazi mbalimbali za elimu wasiopungua milioni 10.
Naomba kuwasilisha.
Kati ya shughuli ninazozipenda sana ni kupanda miti. Mwaka huu wa 2010 nina lengo la kupanda miti ya kivuli na matunda (hasa miembe ya asili) isiyopungua 100.
Kama Wana JF naomba tuanzishe kampeni ya kitaifa kwa Wana JF kama timu kupanda miti katika sehemu maalum hapa nchini ambazo tutazichagua hasa zile ambazo ziko sehemu ya vyanzo vya maji. Kampeni hii ihusishe pia shule zetu na taasisi nyingine za elimu.
Napendekeza tuwe na lengo la kupanda angalau miti 1,000 kwa mwaka huu kama Wana JF. Wakipatikana wana JF 50 na kila mmoja akapanda miti 20 tu tutakuwa tumevuka lengo.
Napendekeza ndoto yetu kitaifa iwe ni kuona kila mwanafunzi hapa nchini anapanda angalau mti mmoja kila mwaka.
Nchi yetu kwa sasa ina Wanafunzi katika ngazi mbalimbali za elimu wasiopungua milioni 10.
Naomba kuwasilisha.