Naomba tumshauri huyu kaka yangu!

Kbd

JF-Expert Member
Oct 9, 2009
1,260
447
Habari za mchana wana MMU! Mchana huu nimeshirikishwa jamba na kaka yangu (tunafanya kazi wote) ili nimshauri na mimi nikaona kabla sijamshauri chochote ngoja nipate mawazo ya wapendwa wangu hapa MMU, maana palipo na wengi hapaharibiki neno.

Alivyonisimulia ni kwamba, yeye enzi za ujana wake karibu miaka 20 imepita akiwa kwenye ndoa aliwahi kutembea na mwanamke nje ya ndoa na kwa bahati yule mdada akapata mimba. Na alivyoona hivyo akamweleza huyu kaka ila huyu kaka alimkatalia kata kata na uhusiano ukaishia hapo. Naomba ifahamike kuwa huyu kaka yuko kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 31 sasa.

Sasa wiki iliyopita huyu kaka kapigiwa simu na baada ya salamu binti akajitambulisha kuwa mi mwanao, ulizaa na fulani miaka hiyo sasa ninakutafuta nikuone. Binti amemaliza form 6 na anafanya kazi na pia anaishi mkoani. Huyu kaka akampigia simu yule mwanamke aliyezaa naye na kumuuliza kulikoni akajibiwa ndio hivyo na nilikwambia ukakataa........sasa mtoto amekuwa akinisumbua kila siku nimwambie baba yake yuko wapi au kama amekufa pia nimwambie...... na mimi nikaona haina maana kumdanya mtoto kwanza ni mkubwa na anamaisha yake hivyo nikaona nimwambie ukweli.

Sasa huyu kaka yangu anajiuliza kwanza akikutana na binti yake atajitetea vipi na pili atamwambia nini mkewe ambaye kweli jambo hilo la mtoto wa nje hataki kusikia kabisa, ila yeye binafsi anatamani kumfahamu mwanae na amtambulishe pia kwa watoto wake na ndugu zake kwa ujumla.

Nasubiri mawazo yenu.
 
huyo mtito ni mkubwa na sioni tatizo la huyu kaka kwenda kumjua mtoto wake mwenyewe...huyu mke atulizane tuu...kama kweli ana nia huyu mtoto anaweza jitokeza ghagla hapi nyumbani ikawa nomaaaaa...so bora amlete mwenyewe tuuu
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
huyo mtito ni mkubwa na sioni tatizo la huyu kaka kwenda kumjua mtoto wake mwenyewe...huyu mke atulizane tuu...kama kweli ana nia huyu mtoto anaweza jitokeza ghagla hapi nyumbani ikawa nomaaaaa...so bora amlete mwenyewe tuuu

Asante, nitamweleza.
 
Hakuna la kumwambia hapo na cha msingi kila kitu kitapatikana atakapokutana na mwanae,anaweza kujipanga kusema hivi na akakuta mtoto nae anampeleka vile.
Ni jambo jema kumjua mtoto wake
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Habari za mchana wana MMU! Mchana huu nimeshirikishwa jamba na kaka yangu (tunafanya kazi wote) ili nimshauri na mimi nikaona kabla sijamshauri chochote ngoja nipate mawazo ya wapendwa wangu hapa MMU, maana palipo na wengi hapaharibiki neno.

Alivyonisimulia ni kwamba, yeye enzi za ujana wake karibu miaka 20 imepita akiwa kwenye ndoa aliwahi kutembea na mwanamke nje ya ndoa na kwa bahati yule mdada akapata mimba. Na alivyoona hivyo akamweleza huyu kaka ila huyu kaka alimkatalia kata kata na uhusiano ukaishia hapo. Naomba ifahamike kuwa huyu kaka yuko kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 31 sasa.

Sasa wiki iliyopita huyu kaka kapigiwa simu na baada ya salamu binti akajitambulisha kuwa mi mwanao, ulizaa na fulani miaka hiyo sasa ninakutafuta nikuone. Binti amemaliza form 6 na anafanya kazi na pia anaishi mkoani. Huyu kaka akampigia simu yule mwanamke aliyezaa naye na kumuuliza kulikoni akajibiwa ndio hivyo na nilikwambia ukakataa........sasa mtoto amekuwa akinisumbua kila siku nimwambie baba yake yuko wapi au kama amekufa pia nimwambie...... na mimi nikaona haina maana kumdanya mtoto kwanza ni mkubwa na anamaisha yake hivyo nikaona nimwambie ukweli.

Sasa huyu kaka yangu anajiuliza kwanza akikutana na binti yake atajitetea vipi na pili atamwambia nini mkewe ambaye kweli jambo hilo la mtoto wa nje hataki kusikia kabisa, ila yeye binafsi anatamani kumfahamu mwanae na amtambulishe pia kwa watoto wake na ndugu zake kwa ujumla.

Nasubiri mawazo yenu.
yupo ktk ndoa kwa miaka 31, hivi umri wake si chini ya miaka 50. maswali anayouliza kwa mtazamo wangu hayafanani na umri wake kwasababu umri wake siyo wakuuliza hayo maswali, sana sana ninamsoma huyu kaka yako ni kama mtu anae kwepa majukumu, kama ambavyo alikwepa miaka 20 iliyopita. mtoto anamiaka 20, ni mtu mzima, na mama wa mtoto alisha mwambia kuwa mtoto alizaliwa kwa baba mwenye mke na ndoa. hapo sitarajii kuwa mtoto atamwuliza baba eti kwanini ulinikana. mtoto ataangalia tu namnagani Baba anaonyesha kujali kwake kwa wakati huu. ikumbukwe kuwa huyu mtoto anatafuta Baba kama mzazi na si kutafuta pesa ( kwani ana kazi tayari).
suala la nini atamweleza mke wake, nalo lipo wazi halina kuficha, ni kuwa miaka 20 iliyopita alitoka nje ya ndoa, hakujua alichokifanya huko, na sasa, amekuja mtoto ambae alimzaa hiyo miaka 20 iliyopita, hakuwa na mawasiliano na mama wala mtoto, bali sasa mtoto amemtafuta. huyo mke atakubali, aidha hata asipokubali hana la kufanya.binti ni mkubwa anajitegemea, huyo mke hata akiwa mkali anajidhalilisha tuu

bado ninaona huyu kaka yako ni mtu mkwepa majukumu, ni mjeuri, mtu wa miaka 31 kwenye ndoa, ni mtu mzima ni mzee, sasa anapouliza aongee nini kwa huyo binti na amwambie niini mke wake, ni uvivu.
 
mwambie amuone mwanae. Pili tabia ya kukataa mimba aache, imagine amekataa mimba ngapi? Mwisho watoto waoane
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Hakuna la kumwambia hapo na cha msingi kila kitu kitapatikana atakapokutana na mwanae,anaweza kujipanga kusema hivi na akakuta mtoto nae anampeleka vile.
Ni jambo jema kumjua mtoto wake

Asante sana my dia, unajua huyu kaka mwenyewe ni kama amepanic sasa anajikuta hata maneno yanampotea. Nitamweleza.
 
yupo ktk ndoa kwa miaka 31, hivi umri wake si chini ya miaka 50. maswali anayouliza kwa mtazamo wangu hayafanani na umri wake kwasababu umri wake siyo wakuuliza hayo maswali, sana sana ninamsoma huyu kaka yako ni kama mtu anae kwepa majukumu, kama ambavyo alikwepa miaka 20 iliyopita. mtoto anamiaka 20, ni mtu mzima, na mama wa mtoto alisha mwambia kuwa mtoto alizaliwa kwa baba mwenye mke na ndoa. hapo sitarajii kuwa mtoto atamwuliza baba eti kwanini ulinikana. mtoto ataangalia tu namnagani Baba anaonyesha kujali kwake kwa wakati huu. ikumbukwe kuwa huyu mtoto anatafuta Baba kama mzazi na si kutafuta pesa ( kwani ana kazi tayari).
suala la nini atamweleza mke wake, nalo lipo wazi halina kuficha, ni kuwa miaka 20 iliyopita alitoka nje ya ndoa, hakujua alichokifanya huko, na sasa, amekuja mtoto ambae alimzaa hiyo miaka 20 iliyopita, hakuwa na mawasiliano na mama wala mtoto, bali sasa mtoto amemtafuta. huyo mke atakubali, aidha hata asipokubali hana la kufanya.binti ni mkubwa anajitegemea, huyo mke hata akiwa mkali anajidhalilisha tuu

bado ninaona huyu kaka yako ni mtu mkwepa majukumu, ni mjeuri, mtu wa miaka 31 kwenye ndoa, ni mtu mzima ni mzee, sasa anapouliza aongee nini kwa huyo binti na amwambie niini mke wake, ni uvivu.

Nashukuru sana Kindimbajuu kwa ushauri wako, nitamweleza aache uvivu na asiendelee kukataa majukumu.
 
mwambie amuone mwanae. Pili tabia ya kukataa mimba aache, imagine amekataa mimba ngapi? Mwisho watoto waoane


Hata mimi hilo la watoto kuoana nimelifikilia, nitafikisha ujumbe wako ndugu yangu. Shukran
 
yupo ktk ndoa kwa miaka 31, hivi umri wake si chini ya miaka 50. maswali anayouliza kwa mtazamo wangu hayafanani na umri wake kwasababu umri wake siyo wakuuliza hayo maswali, sana sana ninamsoma huyu kaka yako ni kama mtu anae kwepa majukumu, kama ambavyo alikwepa miaka 20 iliyopita. mtoto anamiaka 20, ni mtu mzima, na mama wa mtoto alisha mwambia kuwa mtoto alizaliwa kwa baba mwenye mke na ndoa. hapo sitarajii kuwa mtoto atamwuliza baba eti kwanini ulinikana. mtoto ataangalia tu namnagani Baba anaonyesha kujali kwake kwa wakati huu. ikumbukwe kuwa huyu mtoto anatafuta Baba kama mzazi na si kutafuta pesa ( kwani ana kazi tayari).
suala la nini atamweleza mke wake, nalo lipo wazi halina kuficha, ni kuwa miaka 20 iliyopita alitoka nje ya ndoa, hakujua alichokifanya huko, na sasa, amekuja mtoto ambae alimzaa hiyo miaka 20 iliyopita, hakuwa na mawasiliano na mama wala mtoto, bali sasa mtoto amemtafuta. huyo mke atakubali, aidha hata asipokubali hana la kufanya.binti ni mkubwa anajitegemea, huyo mke hata akiwa mkali anajidhalilisha tuu

bado ninaona huyu kaka yako ni mtu mkwepa majukumu, ni mjeuri, mtu wa miaka 31 kwenye ndoa, ni mtu mzima ni mzee, sasa anapouliza aongee nini kwa huyo binti na amwambie niini mke wake, ni uvivu.

Mawazo kama haya ndio yanayohitajika ktk ulimwengu wa great thinkers
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Ndugu yangu hakuna kitu kibaya kama kukataa mtoto,hata iwe vipi so long as ulichojoa kubali matokeo.Sorry to say this,kaka yako ni mpuuzi sana(he is about my age i pressume),miaka yote alichoogopa kumwambia mkewe ni nini hasa,umri huu anakuwa mgeni na wanawake?Sikiliza bana kakako wala asikubabaishe,take charge kbd,chukua namba ya simu kwa kakako,mpigie simu binti,meet her mwambie we ni shangazi yake,the rest is simple kakako atamkuta mwanae dining table nyumbani kwake kisha tuone atafanya nini,gaddamit.Mambo madogo sana haya kila kukicha tunakutana nayo.Msitupe mtoto mtaleta mikosi bure kwenye ukoo wenu.
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Amuone Mwanaye, na yeye ndiye mwenye maamuzi ya mwisho, kama akimkubali mkewe hawezi kukataa tena mtoto mwenyewe ni mkubwa hivyo tatizo ni yeye hajiamini tu. Inakuwaje Mtu unakataa damu yako mwenyewe kwa kisingizio cha ndoa? huo ni ukatili kuliko kuvunjika kwa hiyo ndoa maana yake kama mkeo anakataa damu yako anamaana gani kwako? Ila tutunze uaminifu ktk ndoa maana matukio ya kukosa uaminifu pia huwa yanaumiza sana.
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Amuone Mwanaye, na yeye ndiye mwenye maamuzi ya mwisho, kama akimkubali mkewe hawezi kukataa tena mtoto mwenyewe ni mkubwa hivyo tatizo ni yeye hajiamini tu. Inakuwaje Mtu unakataa damu yako mwenyewe kwa kisingizio cha ndoa? huo ni ukatili kuliko kuvunjika kwa hiyo ndoa maana yake kama mkeo anakataa damu yako anamaana gani kwako? Ila tutunze uaminifu ktk ndoa maana matukio ya kukosa uaminifu pia huwa yanaumiza sana.
well balanced post,thanks.
 
Ndugu yangu hakuna kitu kibaya kama kukataa mtoto,hata iwe vipi so long as ulichojoa kubali matokeo.Sorry to say this,kaka yako ni mpuuzi sana(he is about my age i pressume),miaka yote alichoogopa kumwambia mkewe ni nini hasa,umri huu anakuwa mgeni na wanawake?Sikiliza bana kakako wala asikubabaishe,take charge kbd,chukua namba ya simu kwa kakako,mpigie simu binti,meet her mwambie we ni shangazi yake,the rest is simple kakako atamkuta mwanae dining table nyumbani kwake kisha tuone atafanya nini,gaddamit.Mambo madogo sana haya kila kukicha tunakutana nayo.Msitupe mtoto mtaleta mikosi bure kwenye ukoo wenu.


Mpaka sasa anawasiliana na mwanae kwenye simu tu........yaani amekuwa anauwoga wa ajabu utafikiria ni teenager, anasema akiongea na huyo mwanae anaona kama mate yanamkauka vile hana hata cha kusema sana sana yule binti ndio anakuwa mchangamfu. Na kingine, mkewe si muelewa kivile hivyo anavyodhani yeye akimwambia patakuwa hapatoshi hapo nyumbani.

Asante kwa ushauri, nitamwambia a-man-up na a face responsiblities zake.
 
Amuone Mwanaye, na yeye ndiye mwenye maamuzi ya mwisho, kama akimkubali mkewe hawezi kukataa tena mtoto mwenyewe ni mkubwa hivyo tatizo ni yeye hajiamini tu. Inakuwaje Mtu unakataa damu yako mwenyewe kwa kisingizio cha ndoa? huo ni ukatili kuliko kuvunjika kwa hiyo ndoa maana yake kama mkeo anakataa damu yako anamaana gani kwako? Ila tutunze uaminifu ktk ndoa maana matukio ya kukosa uaminifu pia huwa yanaumiza sana.

Asante sana Likwanda kwa ushauri wako wa busara. Tatizo mpaka sasa ni kwamba huyu kaka hajiamini.......anadhani labda chochote chaweza kutokea kwa binti yake au kwa mkewe. Na mkewe ni mkorofi kwa masuala hayo.....hataki mambo ya watoto wa nje, ndio kinachomtia woga huyu kaka.
 
Kulea alishindwa hata kumuona mtoto anaona kazi?Amtendee huyo binti haki kwa kwenda kumuona maana mpaka amtufute mtu aliyemkataa tangu hata hajazaliwa ni sawa na kujitoa mhanga. . . it takes a lot of strength to do something like that.

Asipoonana nae sasa hivi huyo binti ataumia na huyo kaka yako atajutia uamuzi wake uzee wake wote.Hata kama mkewe sio mwelewa aanze taratibu.Kwanza akamwone mtoto na waendelee kuwasiliana huku akitafuta namna ya kumwambia mkewe.Anaweza akawaambia ndugu zenu wakubwa (baba, mama, wajomba ) kama wapo wamsaidie kuwambia mke.
 
  • Thanks
Reactions: Kbd
Kulea alishindwa hata kumuona mtoto anaona kazi?Amtendee huyo binti haki kwa kwenda kumuona maana mpaka amtufute mtu aliyemkataa tangu hata hajazaliwa ni sawa na kujitoa mhanga. . . it takes a lot of strength to do something like that.

Asipoonana nae sasa hivi huyo binti ataumia na huyo kaka yako atajutia uamuzi wake uzee wake wote.Hata kama mkewe sio mwelewa aanze taratibu.Kwanza akamwone mtoto na waendelee kuwasiliana huku akitafuta namna ya kumwambia mkewe.Anaweza akawaambia ndugu zenu wakubwa (baba, mama, wajomba ) kama wapo wamsaidie kuwambia mke.

Asante sana mpendwa kwa ushauri, nitaufikisha. Yaani kweli kaka zetu hawa wengine ni majanga tui. Huyu kaka ameshaanza kujuta maana ningejua ningejua zimekuwa nyiingi.
 
Mpaka sasa anawasiliana na mwanae kwenye simu tu........yaani amekuwa anauwoga wa ajabu utafikiria ni teenager, anasema akiongea na huyo mwanae anaona kama mate yanamkauka vile hana hata cha kusema sana sana yule binti ndio anakuwa mchangamfu. Na kingine, mkewe si muelewa kivile hivyo anavyodhani yeye akimwambia patakuwa hapatoshi hapo nyumbani.

Asante kwa ushauri, nitamwambia a-man-up na a face responsiblities zake.
Kbd mama sikiliza,huyo wifi yako asikubabaishe,na kwa taarifa yako miaka 30 ndani ya ndoa hawezi mwacha kakako hata iweje,that i can assure you,besides usimwone ni malaika sana ukute naye ashalambwa ndani ya ndoa vile vile.Acheni mambo yenu haya pelekeni mtoto nyumbani,iteni ukoo mumchinjie mtoto mambo yaishe.
Halafu kbd unaanza kuniuzi!
Na log off (source:washawasha).
 
huwa sielewi mtoto anapomtafuta mzazi aliyemkana akiwa mchanga! Kwangu mimi ni hakuna kurudi nyuma, kama alinikataa ndo imetoka mpaka mbinguni. Ni maoni yangu jamani!
 
Jamani hili suala si rahisi kama mnavyotaka kulirahisisha, kumbukeni huyu kaka (sasahivi babu) alimkataa huyu mtoto (sasahivi binti mzima) tangu utotoni (binti analijua hili), binti ameishi na mamake kwa zaidi ya miaka 20 (toka primary-a'level) akijua anaye baba ila hakuwahi kumtafuta, iweje leo amtafute tena kwa spidi hiyo?
baba unao ulazima wa kumjua mwanao lakini si kwa njia rahisi kama ambayo wajumbe wa jf wanaitaka iwe, fikiria miaka 20 hujui chochote (inaonesha ulishamsahau kabisa) huyu mtoto, leo kalelewa, kasomeshwa n.k wajifanya unamtaka haraka! we unadhani mamake anawaza nini, ukoo unawaza nini, na hata mtoto anakuwazia nini (kukuchangamkia si hoja).
kiukweli ulishakosea toka awali, umemkosea mtoto, mamake. familia yake na ukoo wake!
nakushauri usikutane na mwanao hotelini, bar, stendi n.k tuma ujumbe wa watu waende anakoishi binti (kwa mama yake) wakakutane na mama mzazi, familia yake pamoja na binti wakae kikao juu ya namna gani binti anaweza kuwa halali kwako.
kwa taratibu zetu wabantu, lazima pesa (mtindo wa mahari) itolewe kwa wazazi wa mama wa binti, gharama za malezi n.k
kuhusu mkeo wa sasa hapo usiwe na shaka, kwanza hawezi kukudai taraka, anahitaji kueleweshwa na walewale wajumbe walioenda kulee ulikokataa mimba. FANYA HARAKA USIJE CHEZA SIKINDE NA MWANAO PALE DDC KARIAKOO COZ HUMJUI.
 
Back
Top Bottom