Nimeangalia mwenendo wa sisi Watanzania kwa muda mrefu,mwenzenu si uelewi.Mtanzania mmoja akianzisha biashara fulani wengine tutaanzisha hiyo hiyo;Rais au kiongozi yeyote wa ngazi za juu serikalini akisema jambo ambalo hatimaye litatuumiza sisi wenyewe, tutanyanyuka kuandamana na kuliunga mkono;tukiletewa shule za kata ambazo malengo yake halisi ni ku dumaza elimu, tutawapeleka watoto wetu huko bila hata kulalamika,huku tukisifu na kusema shule za kata ni mkombozi wa maskini.Mlolongo wa tabia hizo ni mrefu mno.Lakini hasa kwa nini? Naomba msaada.