Naomba Msaada wenu WanaJF: Maumivu Makali wakati wa MP

SaidAlly

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
2,328
2,217
Ndugu wanaJF!

Nahitaji msaada wenu sana kuhusu tatizo la maumivu makali wakati wa hedhi anayopata mpenzi wangu.

Amekua akipata maumivu kwa muda wa karibu miaka 10 sasa, hatujapata mtoto bado na sehemu kubwa ya maoni tunayopewa ni kua atakapopata mtoto basi tatizo hilo litaisha ingawa bado hatujapanga kupata mtoto kwa hivi sasa, je hakuna namna inayoweza kumsaidia? Kwasasa ana umri wa miaka 34 na amekua akitumia tiba mbalimbali na kupata nafuu kwa muda tu, hiyo ikiwemo sindano, vidonge na hata dripu. Sasahivi hali imekua mbaya zaidi kwani ameanza juzi akameza vidonge lakini akazidiwa na maumivu ikabidi jana alazwe hospitali kwa muda akitundikiwa dripu na kupata nafuu kidogo na akapewa vidonge aendelee kumeza lakini jioni hii ya leo hali imekua mbaya zaidi tena na hata hatujui tuende wapi tena kupata msaada.

Nahitaji msaada wenu wanaJF tuondokane na tatizo hili kwani wakati wote unapofika muda wa MP amani huwa inatuishia hapa nyumbani na huzuni hutawala na kwangu mie huwa naumia zaidi kwa kushindwa kumsaidia pale anapozidiwa kwa maumivu.

Natoa shukrani zangu za awali nikiamini ntapata msaada wenu ndugu zangu.

Nawakilisha!
 
duuu! 34yrz bado hajapata mtoto?? Ndo mana anasumbuliwa na maumivu, nawashauri mzae umri umeenda sana jamani.
 
duuu! 34yrz bado hajapata mtoto?? Ndo mana anasumbuliwa na maumivu, nawashauri mzae umri umeenda sana jamani.

Asante kwa ushauri huo pia ingawa nimesema ameanza kupata maumivu toka zamani kama miaka 10 iliyopita yani tangu akiwa na miaka 24.

Ni kweli tunatamani kuzaa lakini maisha ya sasa sio kuzaa tu, kuna kujipanga pia na mambo mengine ambayo nisingependa kuyaweka hapa yanayosababisha tusizae maana hilo kidogo naona kama sio mahala pake. Asante!
 
Kaka,ka mnahis kuzaa inaweza ikawa solution ni vyema mkajaribu,pia umri umeyoyoma hao watoto si watakwita babu!ukishindwa kuzaa nenda hospital bingwa mkapate ushaur na dawa,mfano pale kairuk(mikochen)kuna dada dokta anaitwa clementina anaweza akawasaidia...duh mpe pole wifi.
 
Kaka,ka mnahis kuzaa inaweza ikawa solution ni vyema mkajaribu,pia umri umeyoyoma hao watoto si watakwita babu!ukishindwa kuzaa nenda hospital bingwa mkapate ushaur na dawa,mfano pale kairuk(mikochen)kuna dada dokta anaitwa clementina anaweza akawasaidia...duh mpe pole wifi.

Asante sana kwa ushauri, nadhani sehemu ya kuanzia kesho asubuhi ni hapo Kairuki. Asante!
 
Asante kwa ushauri huo pia ingawa nimesema ameanza kupata maumivu toka zamani kama miaka 10 iliyopita yani tangu akiwa na miaka 24.

Ni kweli tunatamani kuzaa lakini maisha ya sasa sio kuzaa tu, kuna kujipanga pia na mambo mengine ambayo nisingependa kuyaweka hapa yanayosababisha tusizae maana hilo kidogo naona kama sio mahala pake. Asante!
34yrs bado mnajipanga kuhusu kuzaa? kama yeye ni 34 wewe una ngapi sasa!? au kuna tatizo lingine zaidi ya hedhi? ni bora uweke wazi ili upate msaada na ushauri! kwa age hiyo kama bado mnatafuta maisha ndo azae labda atakuwa kwenye 40z
ni maoni yangu tu!
 
34yrs bado mnajipanga kuhusu kuzaa? kama yeye ni 34 wewe una ngapi sasa!? au kuna tatizo lingine zaidi ya hedhi? ni bora uweke wazi ili upate msaada na ushauri! kwa age hiyo kama bado mnatafuta maisha ndo azae labda atakuwa kwenye 40z
ni maoni yangu tu!

Asante kwa maoni yako Mdada!
Hatujipangi kutafuta maisha isipokua ni kwaajili ya kuzaa. Ni kweli umri umekwenda na tunalifahamu hilo lakini kuzaa dada yangu ni maamuzi ya wahusika kwani naamini ni kwei raha ya ndoa ni kuzaa. Hakuna tatizo lingine zaidi ya maumivu wakati wa hedhi sasa labda kama atakua na tatizo linalosababisha hayo maumivu kipindi hicho (ukiacha kuto kuzaa)basi wataalam wanaweza kutusaidia.
Ninachoomba msaada ni Je hakuna tiba katika hilo tofauti na kuzaa?

Asante kwa Maoni.
 
kaka age kubwa yote hyo mtie kitu hyo mnasubili nn nawakati mnazeeka tu achen hzo bana bado tu mu wachumba miaka yote duuuuuuuuu
 
Ndugu wanaJF!

Nahitaji msaada wenu sana kuhusu tatizo la maumivu makali wakati wa hedhi anayopata mpenzi wangu.

Amekua akipata maumivu kwa muda wa karibu miaka 10 sasa, hatujapata mtoto bado na sehemu kubwa ya maoni tunayopewa ni kua atakapopata mtoto basi tatizo hilo litaisha ingawa bado hatujapanga kupata mtoto kwa hivi sasa, je hakuna namna inayoweza kumsaidia?









Kwasasa ana umri wa miaka 34 na amekua akitumia tiba mbalimbali na kupata nafuu kwa muda tu, hiyo ikiwemo sindano, vidonge na hata









dripu. Sasahivi hali imekua mbaya zaidi kwani ameanza juzi akameza vidonge lakini akazidiwa na maumivu ikabidi jana alazwe hospitali kwa muda akitundikiwa dripu na kupata nafuu kidogo na akapewa vidonge aendelee kumeza lakini jioni hii ya leo hali imekua mbaya zaidi tena na hata hatujui tuende wapi tena kupata msaada.

Nahitaji msaada wenu wanaJF tuondokane na tatizo hili kwani wakati wote unapofika muda wa MP amani huwa inatuishia hapa nyumbani na huzuni hutawala na kwangu mie huwa naumia zaidi kwa kushindwa kumsaidia pale anapozidiwa kwa maumivu.

Natoa shukrani zangu za awali nikiamini ntapata msaada wenu ndugu zangu.

Nawakilisha!


Pole sana, mbali na maumivu hayo makali wakati wa hedhi,huwa ana maumivu wakati wakati wa kufanya tendo la ndoa?maumivu wakati wa aja ndogo? anaenda aja ndogo mara kwa mara? maumivu ya mgongo na sehemu ya kuzunguka uke na sehemu ya aja kubwa?

Majibu yako yanaweza kuwa ndio au hapana,lakini maumivu makali ( hasa ya tumbo) si hali ya kawaida,mara nyingi ni dalili ya tatizo ambalo kitaalamu linaitwa ENDOMETRIOSIS.Hali hiyo uweza sababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito.Muone gynercologist aliye karibu na atamfanyia vipimo kama ultrasound na magnetic resonance imaging(MRI).Kama itagundulika tatizo ni hilo nililotaja hapo juu,basi aweza fanyiwa surgery kuondoa hiyo hali

NB.Siyo wote wenye endometriosishuwa wana tatizo la kupata ujauzito lkn asimilia kubwa hawaweza kupata ujauzito
good time brother.
 
Pain during menses ni normal but.. hold let me check my blueprints OB & GY Text book .. nikipata jibu nitarudi kukujibu or i might ask my attending kesho InshaAllah! ...

Ugueni pole bro.
 
Kaka,ka mnahis kuzaa inaweza ikawa solution ni vyema mkajaribu,pia umri umeyoyoma hao watoto si watakwita babu!ukishindwa kuzaa nenda hospital bingwa mkapate ushaur na dawa,mfano pale kairuk(mikochen)kuna dada dokta anaitwa clementina anaweza akawasaidia...duh mpe pole wifi.

Laut!
Asante sana kwa ushauri wako, tumeenda Kairuk na tumempata Dada Clementina, amefanyiwa vipimo na imegundulika ana uvimbe flan kwa ndani japo ni mdogo ila unaendelea kukua, kapatiwa dawa kama hautapotea itabidi afanyiwe operation. Asante kwa msaada wako.
 
Pain during menses ni normal but.. hold let me check my blueprints OB & GY Text book .. nikipata jibu nitarudi kukujibu or i might ask my attending kesho InshaAllah! ...

Ugueni pole bro.

Asante Njiwa!
 
Pole sana, mbali na maumivu hayo makali wakati wa hedhi,huwa ana maumivu wakati wakati wa kufanya tendo la ndoa?maumivu wakati wa aja ndogo? anaenda aja ndogo mara kwa mara? maumivu ya mgongo na sehemu ya kuzunguka uke na sehemu ya aja kubwa?

Majibu yako yanaweza kuwa ndio au hapana,lakini maumivu makali ( hasa ya tumbo) si hali ya kawaida,mara nyingi ni dalili ya tatizo ambalo kitaalamu linaitwa ENDOMETRIOSIS.Hali hiyo uweza sababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito.Muone gynercologist aliye karibu na atamfanyia vipimo kama ultrasound na magnetic resonance imaging(MRI).Kama itagundulika tatizo ni hilo nililotaja hapo juu,basi aweza fanyiwa surgery kuondoa hiyo hali

NB.Siyo wote wenye endometriosishuwa wana tatizo la kupata ujauzito lkn asimilia kubwa hawaweza kupata ujauzito
good time brother.

Mkuu Kiroboto!
Asante kwa maoni yako na ushauri, tumeenda Kairuk(mikochen) na kumuona mtaalam wa mambo hayo, maelezo yake yameendana na mtazamo wako, kesha chukuliwa vipimo na imeonekana ana uvimbe kwa ndani, kapewa dawa kama hautaisha basi atafanyiwa operation.

Nakushukuru kwa kutujali mkuu! Asante sana.
 
Pole sana kwa maumivu.
Sababu kubwa ni kwamba kizazi chake hakiko active yaanai "not energised" Hivyo basi anywe bio water, maji hai yaliyotengenezwa kwa bio disc. Pia asome web hii: Amezcua Bidhaa hii inauzwa online na QNet | Direct Selling - Home. Kwa maelezo zaidi niandikie ama utoe private mail yako na namba ya simu nikupe maelezo nje ya forum hii.
UNIQUE
 
Ndugu wanaJF!

Nahitaji msaada wenu sana kuhusu tatizo la maumivu makali wakati wa hedhi anayopata mpenzi wangu.

Amekua akipata maumivu kwa muda wa karibu miaka 10 sasa, hatujapata mtoto bado na sehemu kubwa ya maoni tunayopewa ni kua atakapopata mtoto basi tatizo hilo litaisha ingawa bado hatujapanga kupata mtoto kwa hivi sasa, je hakuna namna inayoweza kumsaidia? Kwasasa ana umri wa miaka 34 na amekua akitumia tiba mbalimbali na kupata nafuu kwa muda tu, hiyo ikiwemo sindano, vidonge na hata dripu. Sasahivi hali imekua mbaya zaidi kwani ameanza juzi akameza vidonge lakini akazidiwa na maumivu ikabidi jana alazwe hospitali kwa muda akitundikiwa dripu na kupata nafuu kidogo na akapewa vidonge aendelee kumeza lakini jioni hii ya leo hali imekua mbaya zaidi tena na hata hatujui tuende wapi tena kupata msaada.

Nahitaji msaada wenu wanaJF tuondokane na tatizo hili kwani wakati wote unapofika muda wa MP amani huwa inatuishia hapa nyumbani na huzuni hutawala na kwangu mie huwa naumia zaidi kwa kushindwa kumsaidia pale anapozidiwa kwa maumivu.

Natoa shukrani zangu za awali nikiamini ntapata msaada wenu ndugu zangu.

Nawakilisha!

Ask her to visit Precious Clinic at Mawasiliano Tower or call 0659131305
 
Unataka azae akiwa na mingapi ndg vizuri akazaa mwanamke akazaa kabla 35
 
Nina rafiki yangu alikuwa na matatizo ya uvimbe. Na pia alichelewa kidogo kuzaa. Kuna doctor anaitwa Kaisi kama sikosei ni mtaalamu sana. Alimsaidia akamwambia binti nakutoa uvimbe ila nakushauri uzae idadi ya watoto unaowataka haraka kwani chance ya uvimbe kurudi tena ni kubwa na itakuwa ngumu kufanya opereshen now and then.

Kwa hiyo japo mwatafuta maisha nadhani mfikirie seriously issue ya mtoto. Mauvimbe yana tabia ya kuota upya hata baada ya operation.
 
Back
Top Bottom