Ado Shaibu
Member
- Jul 3, 2010
- 99
- 108
Wakubwa naomba mnisaidie mantiki ya katiba yetu kuzuia wagombea wasio ridhishwa na matokeo ya urais kupeleka kesi mahakamani ili kupata haki yao.
Title mbona haiendani na swali lenyewe! Anyway, Ibara ya 41 (7) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 inasema kama ifuatavyo: "Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake."Wakubwa naomba mnisaidie mantiki ya katiba yetu kuzuia wagombea wasio ridhishwa na matokeo ya urais kupeleka kesi mahakamani ili kupata haki yao.
Title mbona haiendani na swali lenyewe! Anyway, Ibara ya 41 (7) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 inasema kama ifuatavyo: "Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake."
Mantiki yake ni kulinda Kiti cha Rais maana Kiti hicho ni nyeti sana. Sasa kama Rais anaweza tu kuondolewa kirahisi rahisi hivyo na Mahakama nchi itabaki na amani kweli? Hata hivyo naona kama Rais wa Tanzania karibu yuko juu ya Sheria za nchi, ukiondoa mambo machache yaliyoongelewa kwenye Ibara ya 46A ya Katiba ya Mwaka 1977.
Mpendwa Buchanan, Mhhhh, Pamoja na kulinda kiti hapo hapo amenyongwa mwananchi endapo rais ataamua kuingilia mchakato wa uchaguzi kupitia mkurugenzi wa uchaguzi aliyemchangua mwenyewe. Fikiri kwamba katika nchi kumekuwa na hakika kuwa mgombea x kapata kura milioni 10 na mgombe y kapata kura milioni 8 maana hata kama ni uchaguzi matokeo yako wazi na watu wanakuwa nayo. Wakihesabu wanaona idadi ya hakika ni ngapi, kisha mkurugenzi wa uchaguzi bila haya anatangaza kuwa mgombea y kapata kura 10,000,000 na mgombea x kapata kura 8,000,000; mabo yanaisha kihivyo hivyo tu? Hapa mi nadhani ni tatizo!
Title mbona haiendani na swali lenyewe! Anyway, Ibara ya 41 (7) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 inasema kama ifuatavyo: "Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake."
Mantiki yake ni kulinda Kiti cha Rais maana Kiti hicho ni nyeti sana. Sasa kama Rais anaweza tu kuondolewa kirahisi rahisi hivyo na Mahakama nchi itabaki na amani kweli? Hata hivyo naona kama Rais wa Tanzania karibu yuko juu ya Sheria za nchi, ukiondoa mambo machache yaliyoongelewa kwenye Ibara ya 46A ya Katiba ya Mwaka 1977.
Kwa hiyo unafikiri kuwa mantiki ya Ibara ya 41 (7) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 ni ipi, maana ndio swali la mtoa hoja!
Sasa kama Rais anaweza tu kuondolewa kirahisi rahisi hivyo na Mahakama nchi itabaki na amani kweli? Hata hivyo naona kama Rais wa Tanzania karibu yuko juu ya Sheria za nchi, ukiondoa mambo machache yaliyoongelewa kwenye Ibara ya 46A ya Katiba ya Mwaka 1977.[/COLOR][/B]
Buchanan, kama Rais anaingia madarakani bila ridhaa ya wapiga kura wengi matokeo yake ni chaos. Kumbuka Kenya wananchi wali resist kwa sababu rais alichukuana na jaji mkuu wakaenda viwanja vya Ikulu kwa haraka wakaapa kwa haraka mpaka jamaa akakosea kula kiapo.