Naomba msaada wa jinsi ya ku-conncect pc mbili kama sina network.

baina

JF-Expert Member
Oct 12, 2010
219
59
Wana jamvi tafadhali naomba mnipokee na shida yangu hii, nina ka office kangu na computer mbili, nataka kuwa nina share mafaili na siko na mtandao, je nawezaje kuziunganisha pc hizi 2 pamoja?, nahitaji kuwa na nini?, na je nikinunua ya tatu nayo naweza kuiunganisha?, natanguliza shukrani.
 
Kama zina wireless unaweza kutengeneza adhock network hii ni temporary na inapotea mtu mmoja aki disconnect. Cheki Set up a computer-to-computer (ad hoc) network

Njia ya muda mrefu zaidi unaweza kuziunganisha na Ethernet cable ambayo ni cross-over sio straight, hii ni kwa PC mbili tu.

Njia ambayo mimi ningekushauri kama zote zina Wifi ni kununua Wireless "Router" yaani hizi Wifi Access Point za kawaida hata bila kuwa na mtandao wa nje PC zote zinakuwa zipo kwenye network moja so zinaweza kuwasiliana. Kama hauna wifi kwenye PC zote au kama unahitaji spidi kubwa sana basi tumia ethernet cables kisha zichomeke kwenye switch (Wifi Access point mara nyingi zina sehemu za switch pia so unaweza kufanya zote kwa pamoja, laptop wireless, desktops wired) au hub (technically slower).
Amazon.com: wireless router
 
Unaposema ''Njia ya muda mrefu zaidi unaweza kuziunganisha na Ethernet cable ambayo ni cross-over sio straight, hii ni kwa PC mbili tu.'' unamaanisha nini? tafadhali nipe taratibu za kufanya haya.
 
Kuna Ethernet cable straight na kuna crossover, tofauti ni katika jinsi waya zilivyopangwa katika zile pini za kuchomekea.

Kama unataka kuunganisha PC mbili directly unahitaji crossover cable, kama una switch au hub katikati basi unahitaji straight cable.

So nenda duka lolote la PC nunua crossover Ethernet cable, chomeka kwenye PC zako kisha fuata maelekezo haya jinsi ya kusetup Windows zionane Connect two computers using a crossover cable

Ila mimi ningekushauri njia ya Wifi Router maana ndo rahisi zaidi na ya muda mrefu maana itachukua PC nyingi. Ili mradi uweke password watu wa nje wasiconnect.

A3L791B05M-YLWS.jpg
 
Pia unaweza fanya hivi....
kwanza unatakiwa udownload hizi software....

  1. Virtual wifi router (works only in windows 7)
  2. Dukto r5

ukishapata hizo software run hiyo virtual wifi router (in windows 7 pc) then itafunguka na kujificha kwenye notification area, iclick hapo kwenye notification area then kwenye share net from chagua no internet sharing, halafu nenda hapo kwenye configure ingiza name na password (min is 8 characters) then click setup hotspot. Ukishasetup nenda kwenye hiyo pc nyingine angalia hapo kwenye wireless utaon hiyo network uliotengeneza inaonekana click connect na ingiza ile password ulioset

baada ya kutengeneza hiyo network install dukto r5 in both computers, then open hizo dukto kwenye hizo computer, zikishafunguka utaoona computer iliyokuwa connected inaonekana hapo click hiyo na hapo utakuta option za ku transfer files, folder na kutuma message.

KUMBUKA: hiyo virtual wifi router inafanya kazi kwenye windows 7 tu

Capture.PNG Capture1.PNG Capture2.PNG Capture3.PNG
 
Simple and clear nenda duka la computer wambie wakupe Ethernet Switch sio mbaya hata ukaanza na 4 Port kama utapata...nyingi zinaanzia 8 Port... waambie wakupe na Patch Cable mbili za Straight Though ....kama computer ni 3 basi chukua cable tatu...hiyo switch kama ni ya 4 Ports ina maana ina uwezo wa kuchukua computer nne ...
 
anataka pc mbili. hivyo tumia waya wa cross over tu kama ilivyosemwa. ni gharama nafuu. chini ya elfu 10
 
Kama zina wireless unaweza kutengeneza adhock network hii ni temporary na inapotea mtu mmoja aki disconnect. Cheki Set up a computer-to-computer (ad hoc) network

Njia ya muda mrefu zaidi unaweza kuziunganisha na Ethernet cable ambayo ni cross-over sio straight, hii ni kwa PC mbili tu.

Njia ambayo mimi ningekushauri kama zote zina Wifi ni kununua Wireless "Router" yaani hizi Wifi Access Point za kawaida hata bila kuwa na mtandao wa nje PC zote zinakuwa zipo kwenye network moja so zinaweza kuwasiliana. Kama hauna wifi kwenye PC zote au kama unahitaji spidi kubwa sana basi tumia ethernet cables kisha zichomeke kwenye switch (Wifi Access point mara nyingi zina sehemu za switch pia so unaweza kufanya zote kwa pamoja, laptop wireless, desktops wired) au hub (technically slower).
Amazon.com: wireless router

Hivi amazon wana ship TZ kweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom