Naomba MCHANGO wako....

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,342
29,140
Wakubwa
Nimeamua kuvunja utaratibu wa JF yetu kwa kuleta kitu kigeni kabisa ktk forums yetu.

Ni hivi nategemea kufunga ndoa desemba mwaka huu ambapo pamoja na ubazazi wangu nimekwama kwa binti mmoja wa kipare na desemba 23 ndiyo ndoa yenyewe. na mpaka sasa nimefikia ktk kiwango cha kukusanya michango ya ndugu, jamaa na marafiki. ka kuwa humu nina marafiki wengi nimeamua kuwapostia ujumbe huu kama kuna mtu yeyote ataguswa aweze kushiriki kutoa mchango hata wa maoni ili angalau andiko litimie. Ndoa itakuwa dar es salaam na mnopenda bia mmeula wa chuya maana hakutakuwa na bia ni ya kikanisha haswaaa. Ila amini amini nakuambieni kuwa mwaka huu hautaisha nitakuwa nimefunga ndoa.

Kama mtapenda kuchangia kihali na mali basi wasiliana nami ili uweze kupata details. ila kama kutakuwa na mtu atakayechanga humu naahidi kutoa 50% ya mchango kwa JF.
 
Du hongera kwa kuamia kuuachana ukapera! Jiko lina utamu wake! Naona umekufa kwa mtoto wa Kipare- je unaweza kutupa sababu- au kupenda tu?
Ni hayo tu Mkuu!
 
zaidi ya kupenda.
huyu binti amenikuta nikiwa katikati ya jukwaa la ufuska, nilikuwa shikikiki na aliweka stratergy ya kunibadilisha na mapaka nikabadilika na kuwa mtu. hivi sasa natembea kifua mbele kwamba ubazazi nimeacha na akina brazameni najua hawatoacha mpaka wachongwe na madem hodari kama huyu.
pia sababu kubwa ni kuwa tabia yake imenivutia na kwa kuwa tunaheshimiana na kujaliana. kikubwa zaidi tunasikizana. Hivyo ilinichukua miaka minne kufikia uamuzi huu.
Kwa hiyo nimemwomba tufunge ndoa si kwa sababu ya mapenzi tu, bali zaidi ya hapo. (nawazimikia sana mabinti wa kiafrika).

Mzalendo unatoa ahadi ya kiasi gani ktk mchango wako?

Yeyote ajisikiaye kuchanga atume ujumbe ktk pm yangu
 
Duh! mkuu umeamua kweli kutoka chamani kwetu? hapa hatoki mtu....sasa mkuu hiyo harusi haina mvinyo itapanda kweli kwa akina sisi?
 
December ndio hiyo imefashifika tuambie harusi itafanyika wapi, na pia kama unataka mchango wetu please fikiria mara mbili suala la kuweka mvinyo cos bila ya mvinyo wakina sisi hatuwezi kuchangamka.
 
zaidi ya kupenda.
huyu binti amenikuta nikiwa katikati ya jukwaa la ufuska, nilikuwa shikikiki na aliweka stratergy ya kunibadilisha na mapaka nikabadilika na kuwa mtu. hivi sasa natembea kifua mbele kwamba ubazazi nimeacha na akina brazameni najua hawatoacha mpaka wachongwe na madem hodari kama huyu.
pia sababu kubwa ni kuwa tabia yake imenivutia na kwa kuwa tunaheshimiana na kujaliana. kikubwa zaidi tunasikizana. Hivyo ilinichukua miaka minne kufikia uamuzi huu.
Kwa hiyo nimemwomba tufunge ndoa si kwa sababu ya mapenzi tu, bali zaidi ya hapo. (nawazimikia sana mabinti wa kiafrika).
msanii hongera sana tena nakaribu kwenye chama. Nimependa sana jitihada za huyo dada, thats what women were created for, to shape and help men be the best they can be. Mungu akujalie uwe na amani na furaha kila siku na kumbuka hakuna institution nzuri duniani kama familia, trust me just play your cards rite and you'll never regret. Huu ndio mchango wangu wa mawazo.
 
..duh!hii imekaa ki-msanii haswa!

..kwahiyo,inotherwords unatushauri tuichangie jf sio!

..msg delivered!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom