Naomba mawazo juu ya project ya kufanya

Enny

JF-Expert Member
May 26, 2009
962
130
Habari za kazi wanajamii. Naomba msaada wenu katika jambo hili.

Nilikuwa nafanya kazi katika mgodi wa North Mara na sasa nimepunguzwa kazi, katika pesa nilizolipwa, na mafao yangu ya nssf pamoja na hela niliokuwa nimeweka Benki nina kama milioni 20,000,000.

Nafikiria biashara ya kuanza ili niweze kuendesha maisha yangu na familia kwa ujumla.

Mchango wenu ni muhimu na una maana kubwa katika suala hili.

Ahsateni.
 
fuga kuku na ng'ombe wa maziwa but uwe wa kisasa,i mean with modern technology.Au fanya biashara yoyote ya vyakula vyakula inalipa.
ONYO:usijiingize kwenye biashara za magari magari-INAFILISI hukawii KUFULIA.
 
Tafuta ndugu, ndugu wa kweli akushauri. Millioni ishirini siyo nyingi mana ukizitumia tumia utajikuta hata bishara yenyewe hutaianza. Labda uchukue millioni kumi uiweke kwnye fixed account ili kuhakikisha umeificha pahala na hiyo millioni kumi nyingine ufungue biashara.
 
Nashukuru kwa ushauri wenu, niliuwa nahitaji more business ideas ili niweze kuchagua
wazo lanu lilikuwa ni aanzishe biashara ya vifaa vya ujenzi
 
Nashukuru kwa ushauri wenu, niliuwa nahitaji more business ideas ili niweze kuchagua
wazo lanu lilikuwa ni aanzishe biashara ya vifaa vya ujenzi
Ili upate ushauri vizuri tuambie unataka kufanya biashara sehemu gani ya Tanzania?, Dodoma, Dar?
Kwakuwa kila mahali kuna tofauti yake?
 
Nijambo zuri kufikiria Biashara lakini kutaka ushauri hapa unaweza kupata ushauri usio mzuri.
Ushauri wangu kwako ni kuandaa mpango kazi ambao watu unaowaamini wataupitia na kuukosoa au kukushauri kulingana na mpango kazi .
 
Tafuta ndugu, ndugu wa kweli akushauri. Millioni ishirini siyo nyingi mana ukizitumia tumia utajikuta hata bishara yenyewe hutaianza. Labda uchukue millioni kumi uiweke kwnye fixed account ili kuhakikisha umeificha pahala na hiyo millioni kumi nyingine ufungue biashara.

Hizi biashara za kufuga, au kununua na kuuza sio wote wanafanikia. Ukishaweka hiyo 10m kwenye fixed deposit, angalia kama unaweza kujiajiri mwenyewe as a consultant hii itategemea na background yako. Kama ni mhasibu je una CPA, kama ni IT tanua network yako kuanzia na classmates zako ambao wanaweza kukuunganisha.
 
Habari za kazi wanajamii. Naomba msaada wenu katika jambo hili.

Nilikuwa nafanya kazi katika mgodi wa North Mara na sasa nimepunguzwa kazi, katika pesa nilizolipwa, na mafao yangu ya nssf pamoja na hela niliokuwa nimeweka Benki nina kama milioni 20,000,000.

Nafikiria biashara ya kuanza ili niweze kuendesha maisha yangu na familia kwa ujumla.

Mchango wenu ni muhimu na una maana kubwa katika suala hili.

Ahsateni.


Hi Enny,

Kwanza nashukuru kwa ujasiri wako wa kutaka kupata proffessional advice ya nini cha kufanya na utakifanya vipi(wengi wetu sisi watanzania tunadharau, hivyo hongera sana).

Pili nikukaribishe kwetu GMBD Consult Ltd (for details www.gmconsultz.com)
utakutana na team ya washuari kulingana na biashara unayotaka kufanya. Vile vile tunaanada michanganuo ya biashara(business plan) ya jinsi ya kuifanya hiyo biashara yako. wasiliana nasi kwa simu number 0715 737302 au 0784 737302 pia barua pepe info@gmconsultz.com kwa maelezo zaidi ama tuandikie barua Mkurugenzi, GMBD Consult Ltd, P.o.Box 62279 Dsm
 
Tafadhali sana omba mchakato wa kibiashara toka kwa wataalamu-lakini mimi ningekushauri kufanya biashara ya kuuza nafaka-inatoa sana.na bidhaa ambayo kila mmoja wetu anaitumia sana.
 
There is no risk investment but only risk investor and you are one of them. The first indicator of the risk investor is having money and not knowing what to do with them, you will surely find people who know what to do with your money.

In this world only two things can be invested money and time. If you invest money before investing time, you will surely lose all the money you have.

Please invest the time you have by reading books on the any investment you want to do and love to do because in any investment there are people who succeed and fail the only different is you will guarantee failure if you dont invest time in the investment you want to do.

The only insurance you have in any investment you want to pursue is to invest time first before investing the money, being rich is predictable and not luck, it is pluck. Every person can have monet at any time t, but the people who succeed must and must invest in time before putting that seed down (money). You should know what to sow and at what time and who should help you, what to avoid and who should partner in the journey you ought to begin. If you do that I surely will see you, yes you at the top.
 
Hi Enny,

Kwanza nashukuru kwa ujasiri wako wa kutaka kupata proffessional advice ya nini cha kufanya na utakifanya vipi(wengi wetu sisi watanzania tunadharau, hivyo hongera sana).

Pili nikukaribishe kwetu GMBD Consult Ltd (for details www.gmconsultz.com)
utakutana na team ya washuari kulingana na biashara unayotaka kufanya. Vile vile tunaanada michanganuo ya biashara(business plan) ya jinsi ya kuifanya hiyo biashara yako. wasiliana nasi kwa simu number 0715 737302 au 0784 737302 pia barua pepe info@gmconsultz.com kwa maelezo zaidi ama tuandikie barua Mkurugenzi, GMBD Consult Ltd, P.o.Box 62279 Dsm
Ahsante sana. nitakutafuta
 
Hi Enny,
Kazi kusimama ni kawaida siku hizi hasa baada ya privatisation, wengi tumeishasimama na kuanza hata zaidi ya mara 3. Chamuhimu ni kujua kwenda na wakati hasa contract au kampuni yako. Contract inapoanza na wewe weka malengo kuwa kwa kipindi hiki nitafanya nini, kujenga, shamba, gari au nitasoma nipate CV nzuri zaidi au kama watoto nitampeleka chuo kizuri aanze kujitegemea. Chapili tafuta ajira mpya (potential employers) ukiwa kazini tafuta contacts za waajiri wengine kupitia watu unaowahudumia, wageni, colleagues at college, school, at home or your working place Tatu jifunze kujiajiri mwenyewe kwa kufanya biashara ndo kama anavyosema hapo juu tumia ujuzi wako kujiajiri (mfano consultancy, kufundisha) au fanya tu biashara kama ufugaji, kilimo, duka nk.
naomba tu nikushauri ktk chochote utakachofanya jaribu kwanza kuwekeza kwenye fixed asset kama huna nyumba, shamba au kiwanja kabisa bora ununue hata cha bei ndogo ndo ufanye hizo biashara nyingine. Maana bongo hii hukawii kufilisika biashara kama hujawahi kuzifanya kabisa na huna uhakika wa kupata kazi karibuni, bora uwe ndani ya nyumba yako au uwe na kiwanja cha kwenda hali ikiwa ngumu.
Lakini zaidi nadhani urudi kutafuta kazi hata za muda mfupi (biashara ni nzuri kujifunzia ukiwa na ajira unaweza take risk ya kuinvest hata kiasi kikubwa mradi unajua kuna backup).
nakutakia mafanikio mema
 
biashara zipo nyingi, ila lazima uwe na biashara ambayo unailenga ndio tushauri kuanzia hapo. ni wewe mwenyewe unayeamua kujitoa hivyo hata mtu akikwambia kauze nafaka ilhali hupendi hakikka hutafanikiwa kwani ubunifu hautakuwepo. kujiajiri ni silaha kubwa sana kama una ujasiri na unaweza jiajiri. hofu ya kukosa hela ndio inakwaza wengi kujiajiri ila inalipa.

Fixed deposit sikushauri, in the long run utakuwa unapoteza hasa kwa kuzingatia mfumuko wa bei hapa kwetu, we tumia hiyo pesa kujiajiri na ondoa woga
 
Hi Enny,
Kazi kusimama ni kawaida siku hizi hasa baada ya privatisation, wengi tumeishasimama na kuanza hata zaidi ya mara 3. Chamuhimu ni kujua kwenda na wakati hasa contract au kampuni yako. Contract inapoanza na wewe weka malengo kuwa kwa kipindi hiki nitafanya nini, kujenga, shamba, gari au nitasoma nipate CV nzuri zaidi au kama watoto nitampeleka chuo kizuri aanze kujitegemea. Chapili tafuta ajira mpya (potential employers) ukiwa kazini tafuta contacts za waajiri wengine kupitia watu unaowahudumia, wageni, colleagues at college, school, at home or your working place Tatu jifunze kujiajiri mwenyewe kwa kufanya biashara ndo kama anavyosema hapo juu tumia ujuzi wako kujiajiri (mfano consultancy, kufundisha) au fanya tu biashara kama ufugaji, kilimo, duka nk.
naomba tu nikushauri ktk chochote utakachofanya jaribu kwanza kuwekeza kwenye fixed asset kama huna nyumba, shamba au kiwanja kabisa bora ununue hata cha bei ndogo ndo ufanye hizo biashara nyingine. Maana bongo hii hukawii kufilisika biashara kama hujawahi kuzifanya kabisa na huna uhakika wa kupata kazi karibuni, bora uwe ndani ya nyumba yako au uwe na kiwanja cha kwenda hali ikiwa ngumu.
Lakini zaidi nadhani urudi kutafuta kazi hata za muda mfupi (biashara ni nzuri kujifunzia ukiwa na ajira unaweza take risk ya kuinvest hata kiasi kikubwa mradi unajua kuna backup).
nakutakia mafanikio mema
Nashukuru sana kwa ushauri wako. nitaufanyia kazi.
 
There is no risk investment but only risk investor and you are one of them. The first indicator of the risk investor is having money and not knowing what to do with them, you will surely find people who know what to do with your money.

In this world only two things can be invested money and time. If you invest money before investing money, you will surely lose all the money you have.

Please invest the time you have by reading books on the any investment you want to do and love to do because in any investment there are people who succeed and fail the only different is you will guarantee failure if you dont invest time in the investment you want to do.

The only insurance you have in any investment you want to pursue is to invest time first before investing the money, being rich is predictable and not luck, it is pluck. Every person can have monet at any time t, but the people who succeed must and must invest in time before putting that seed down (money). You should know what to sow and at what time and who should help you, what to avoid and who should partner in the journey you ought to begin. If you do that I surely will see you, yes you at the top.
Thank you for your advice
 
Ongeza mtaji. Mil 20 za madafu is a peanut mazee. I honestly say so.

Usimkatishe tamaa mwenzako, even with 20 m unaweza kufanya biashara ya kueleweka mradi uwe na malengo. Problem ni kama hiyo saving ya Enny ndo anategemea kwa kila kitu kwa sasa. Biashara ya chakula inalipa na unaweza kuanza kwa amount hiyo.
 
Back
Top Bottom