Hivi karibuni kumekuwa na mambo yanayonipa shida kidogo. Utakuta bendi ya muziki inatangaza kuwa itapiga shoo mahali fulani na shoo hiyo itakuwa mpaka majogoo (karibu na asubuhi). Cha kushangaza ni pale wanaposema wakubwa 5,000/= na watoto 1,000/=. Hivi watoto siku hizi wanaruhusiwa shoo za namna hii? Naomba kuelimishwa.