Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Tanzania ilirejea katika mfumo wa Vyama vingi vya Siasa mnamo mwaka 1992, toka kipindi hicho tumeshuhudia Chaguzi tatu 1995, 2000, 2005 na mwezi October 2010 tunatarajia kufanya Uchaguzi wa nne utakaoshirikisha Vyama vingi vya Siasa.
Toka Mfumo huo uanzishwe tumeshuhudia juhudi kubwa zikifanywa na Wapinzani japo kwa Uchache wao Bungeni katika kuivua Nguo Serikali na Kuilazimisha wakati mwingine kufanya kile ambacho isingependa kukifanya kwa Hiari yake.
Tumeshuhudia namna Wapinzani walivyoichachafya Serikali ya CCM katika Masuala ya Buzwagi, Meremeta, Mwananchi Gold, Dowans, Richmond na mengine mengi ambayo kabla ya hapo hakuna Mbunge wa CCM aliyekuwa na Ujasiri hata wa Kuyazungumzia hata hakiwa Chumbani na Mke/Mume wake achilia Mbali Bungeni. Ujasiri huu wa Upinzani uliifanya CCM kuwaruhusu ( Nimetumia neno Kuruhusu Makusudi najua litaibua Mjadala) Baadhi ya Makada wake kupiga Kelele aka kupiga Porojo ( Kwa sabau walijua wananchi wanapenda Mavuvuzela) lakini kwenye maamuzi waliishia Kunywea kama Kuku aliyona Mwewe.
Pamoja na Mfumo usio huru wa Uchaguzi na hata wa Media Coverage Wapinzani wameendelea kuamini kwamba siku moja kitaeleweka tu.
Pamoja na Wapinzani kuzunguka kila kijiji kueleza Uoza wa Chama cha Mapinduzi bado wameendelea kupata kura kiduchu katika Chaguzi kuu na hata zile Chaguzi Ndogo.
Pamoja na Watanzania wengi kuenedelea kuwa Maskini Bado wanaendela kuiimbia Nyumbo za Utukufu na kuipa Ushindi CCM
Pamoja na Wajawazito kuendelea kupelekwa Hospitali na Mikokoteni ya kusukumwa na Punda lakini bado wanaendela kuvaa vitenge vya CCM na kuimba nyimbo za Utukufu kwa CCM zilizotungwa na Wanaoshoba wachache akina Hadija Kopa
Pamoja na Wagonjwa kulala chini mahospitali lakini pindi wanaporuhusiwa kutoka Mahospitali huimba Nyimbo za Kuitukuza CCM ambayo ndiyo iliyotengeneza Seriakali inayowalaza chini katika mahospitali
Pamoja na Wanafunzi kukandamizwa na Serikali ya CCM, na pengine hata kupigwa na FFU laiki wao ndio wamekuwa mstari wa mbele kuiimbia na kuitukuza CCM, na wamekuwa msatari wa Mbele kuwaita Wapinzani Mavuvuzela ( very sad indeed)
Pamoja na Wafanyakazi kuendelea kudhulumia toka enzi za Uhuru lakini wamekuwa ni Mawakala wazuri sana katika kukihakikishia chama hiki ushindi wa Kishindo
Pamoja na Wakulima kuibiwa Mbegu zao za Ruzuku bado wamekuwa wakikipa chama hiki Ushindi mnono kila ya Baada ya Miaka Mitano
Nasema najua watu wataniona mimi Hamnazo lakini niko Serious sana kwa 2010 NIKO TAYARI KUFUNGA NA KUOMBA CCM ISHINDE
1: URAIS KWA 100%,
2: UBUNGE KWA 100% NA
3: UDIWANI KWA 100%
Nasema hivyo kwa Sababu
1: Pamoja na Wapinzani wachache kuonyesha japo kukuruka sisi wananchi tumekataa kuwaongeza Bungeni
2: Nadhani tutakapokuwa na 100% may be wananchi wanaweza kuhisi Umuhimu wa Upinzani Imara katika Mfumo wa Kiutawala
3: Na wakiwamiss akina Zitti, Slaa na Wengine May 2015 wanaweza kuamua kuwaingiza kwa Wingi
KWA MARA NYINGINE TENA NASEMA EE MUNGU NAOMBA USAIDIE CCM IPATE 100% Ili uwapumzishe wapiganaji wetu wa Ukweli akina Dr. Slaa ambao waa risk Maisha yao kwa ajili yetu, wamekubali kuwa Upande wa Maskini lakini sisi Maskini tumewakataa, Wamekubali kupiga kelele juu ya Wizi wa Raslimali zetu sisi maskini lakini sisi Maskini tumewaita Wapayukaji na Waliokosa Mwelekeo, Wangeweza kuweka Silaha Chini na Kujiunga wa Wenye Mirija lakini wamekataa na kuamua kukaa nasi
Mungu Uwapumzishe wapiganaji hawa kabla hawajachoka, Labda kama Wakipumzika tutafunguka na Kutambua Umuhimi wao
Nimetoa Ujumbe Machozi yakinilenga lakini ndilo lililopo Moyoni Mwangu
Toka Mfumo huo uanzishwe tumeshuhudia juhudi kubwa zikifanywa na Wapinzani japo kwa Uchache wao Bungeni katika kuivua Nguo Serikali na Kuilazimisha wakati mwingine kufanya kile ambacho isingependa kukifanya kwa Hiari yake.
Tumeshuhudia namna Wapinzani walivyoichachafya Serikali ya CCM katika Masuala ya Buzwagi, Meremeta, Mwananchi Gold, Dowans, Richmond na mengine mengi ambayo kabla ya hapo hakuna Mbunge wa CCM aliyekuwa na Ujasiri hata wa Kuyazungumzia hata hakiwa Chumbani na Mke/Mume wake achilia Mbali Bungeni. Ujasiri huu wa Upinzani uliifanya CCM kuwaruhusu ( Nimetumia neno Kuruhusu Makusudi najua litaibua Mjadala) Baadhi ya Makada wake kupiga Kelele aka kupiga Porojo ( Kwa sabau walijua wananchi wanapenda Mavuvuzela) lakini kwenye maamuzi waliishia Kunywea kama Kuku aliyona Mwewe.
Pamoja na Mfumo usio huru wa Uchaguzi na hata wa Media Coverage Wapinzani wameendelea kuamini kwamba siku moja kitaeleweka tu.
Pamoja na Wapinzani kuzunguka kila kijiji kueleza Uoza wa Chama cha Mapinduzi bado wameendelea kupata kura kiduchu katika Chaguzi kuu na hata zile Chaguzi Ndogo.
Pamoja na Watanzania wengi kuenedelea kuwa Maskini Bado wanaendela kuiimbia Nyumbo za Utukufu na kuipa Ushindi CCM
Pamoja na Wajawazito kuendelea kupelekwa Hospitali na Mikokoteni ya kusukumwa na Punda lakini bado wanaendela kuvaa vitenge vya CCM na kuimba nyimbo za Utukufu kwa CCM zilizotungwa na Wanaoshoba wachache akina Hadija Kopa
Pamoja na Wagonjwa kulala chini mahospitali lakini pindi wanaporuhusiwa kutoka Mahospitali huimba Nyimbo za Kuitukuza CCM ambayo ndiyo iliyotengeneza Seriakali inayowalaza chini katika mahospitali
Pamoja na Wanafunzi kukandamizwa na Serikali ya CCM, na pengine hata kupigwa na FFU laiki wao ndio wamekuwa mstari wa mbele kuiimbia na kuitukuza CCM, na wamekuwa msatari wa Mbele kuwaita Wapinzani Mavuvuzela ( very sad indeed)
Pamoja na Wafanyakazi kuendelea kudhulumia toka enzi za Uhuru lakini wamekuwa ni Mawakala wazuri sana katika kukihakikishia chama hiki ushindi wa Kishindo
Pamoja na Wakulima kuibiwa Mbegu zao za Ruzuku bado wamekuwa wakikipa chama hiki Ushindi mnono kila ya Baada ya Miaka Mitano
Nasema najua watu wataniona mimi Hamnazo lakini niko Serious sana kwa 2010 NIKO TAYARI KUFUNGA NA KUOMBA CCM ISHINDE
1: URAIS KWA 100%,
2: UBUNGE KWA 100% NA
3: UDIWANI KWA 100%
Nasema hivyo kwa Sababu
1: Pamoja na Wapinzani wachache kuonyesha japo kukuruka sisi wananchi tumekataa kuwaongeza Bungeni
2: Nadhani tutakapokuwa na 100% may be wananchi wanaweza kuhisi Umuhimu wa Upinzani Imara katika Mfumo wa Kiutawala
3: Na wakiwamiss akina Zitti, Slaa na Wengine May 2015 wanaweza kuamua kuwaingiza kwa Wingi
KWA MARA NYINGINE TENA NASEMA EE MUNGU NAOMBA USAIDIE CCM IPATE 100% Ili uwapumzishe wapiganaji wetu wa Ukweli akina Dr. Slaa ambao waa risk Maisha yao kwa ajili yetu, wamekubali kuwa Upande wa Maskini lakini sisi Maskini tumewakataa, Wamekubali kupiga kelele juu ya Wizi wa Raslimali zetu sisi maskini lakini sisi Maskini tumewaita Wapayukaji na Waliokosa Mwelekeo, Wangeweza kuweka Silaha Chini na Kujiunga wa Wenye Mirija lakini wamekataa na kuamua kukaa nasi
Mungu Uwapumzishe wapiganaji hawa kabla hawajachoka, Labda kama Wakipumzika tutafunguka na Kutambua Umuhimi wao
Nimetoa Ujumbe Machozi yakinilenga lakini ndilo lililopo Moyoni Mwangu