Naogopa kupima ukimwi kuliko kitu chochote

Go check n utajua jinsi ya kujipanga upya.......
Ujasiri unaanza hivi

Check ur list ya passenger wako....kuna mgonjwa? Aliyekufa kwa kuumwa na dilili zilishabihiana na unachokidhania na kukiogopa?
Historia yako ya kutembea kwenye mvua ina matukio ya kutembea bila rain coat?

Baada ya hapo unajiuliza hivi: Unapokuwa safarini na ukapotea njia ni bora kuuliza au ni heri kusonga mbele tu bila kujua hatma ya safari yako?..........

Kapime ndugu ni muhimu kujua afya yako ili kuamua jinsi ya kuendelea kuishi
 

....Itabidi uutafute huo ujasiri haraka iwezekanavyo ili ukapime afya yako. Utakosa raha na kuwa na wasiwasi sana lakini huna jinsi inabidi tu ujitutumue na kwenda kujiangalia kama uko salama au umeshadhurika. Siku ile ya AIDS duniani kama sikosei December 1, 2011 nilikuwa naangalia kipindi kimoja walikuwa wanazungumzia kuhusu umuhimu wa kupima na wakasema sasa hivi ni 20 minutes tu tayari umeshajua hali yako. Kila la heri.

Du!20 minutes!Mimi juzi nilienda kupima nikapewa majibu ndani ya kama dk 7 hivi!Au kile kipimo kilikuwa fake nini?
 
nitapata wapi huo ujasiri mimi?na wametangaza hakuna dawa milele

Kupima muhimu sana ili kujua afya yako na kujipanga upya.
Bila shaka kinachokuogopesha kupima ni kuogopa kuja kuambiwa una HIV.Ila kumbuka kama una HIV na hata usipopima utaendelea kuwa nayo hadi utakapokuja kuanza kuugua ndo wakati utahitaji kupimwa ili wajue ugonjwa unaokusumbua,then wakigundua una AIDS inakua too late. Kwa hiyo dawa ni kupima sasa hivi then uishi kadri watakavyokuelekeza,na kama hauna utakua umefanya bonge la re set na kuanza life upya.Hakuna kitu nilichokua naogopa kama kupima,maana barabara nilizopita wewe ni cha mtoto,ila sasa hivi wala hata nikiambiwa nikajitolee damu mie ndo wa kwanza .,
 
kwa uzembe wa madactari wetu wa kibongo, unaweza pima ukawa negativ ukaambiwa positiv. kwikwikwi! kumbe wameshamix blood sample na ya mwingine. kumbuka muhimbili scenario! ila be courageous, okk
 
yani siku iz ni ndani ya dakika3 tu ushapata jibu tena kama unajua kukiangalia kile kipimo unaweza ukawa ushajijua kabla hata ya kuambiwa make siku izi unapima hapohapo unaona damu inavosafiri katika HIV TEST ila ukiona umeanza na kamstari ka kwanza kekundu kwa kile kipimo cha kwanza ujue huna jipya na wa wakirudia tena na determine ikasoma tena vistari viwili ujue uhuuuuuuuuu!!! tayari hapo msubiri mamaa akupe ushauri ili uanze mashudu.. ukijua afya yako is soo good yaani unakuwa na nyodo kwa kila anaye kutaka au unaye mtaka lakini pia ujue si wote wameamukizwa kwa ngono kuna wengine ajali, na mengineyo tofauti na ngono so hata nkimuona mtu anaye ishi na vvu huwa sipelekei kuwa alikuwa mzinzi lahasha huenda first touch yake ndo ika hit the point so usihofu mdau nenda tu .
 
Mbona kupima ki2 rahisi sana!! mi nishapima kama mara 3 hivi!! majibu ndio huwa sichukui.
Hilo ni kosa kubwa kwa nafsi yako. Lakini hujachelewa bado. Jipe moyo wa ujasiri kapime na uchukue majibu yako. Watu wengi wasichokijua ni kuwa yeyote anayefanya hivyo huwa kama amezaliwa upya, kwani majibu yoyote atakayopata yatamweka huru zaidi na kumpa uwezo wa kujua mustakabali wa maisha yake na namna bora ya kuishi kuanzia hapo. Kwa mfano usipokutwa na virusi utapata ahueni ambayo hujawahi kuipata kabla itakayokufanya uwe makini zaidi kwa vitendo vyako ili usijeambukizwa virusi. Na ukipatikana na Virusi itabidi ukubaliane na ukweli kwa kuanza kupima kipimo cha pili ili kujua kiasi cha uambukizo (viral load) ili ujue km unahitaji kuanza kutumia dawa za kurefusha maisha ARVs, na kuchukua tahadhari ili usiweze kuambukizwa aina nyingine ya virusi vya HIV. Kwa kufanya hivyo utakuwa unaishi kwa matumaini.
 
jamani dawa ni kubadili tabia kwa wote wawili sio mmoja ni kazi bure kuishia kupima tu then mwendo mdundo,ni sawasawa na ujitibu malaria halafu unalala bila neti utauguwa tena na tenaaaa, ni hayo tu
Malaria haikubaliki!!Ukimwi----?
 
sasa kama unajitolea kwenda kupima halafu unapewa majibu tofauti jamani inakuwaje hapo????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom