Naniasiyekumbuka hili??

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,596
Mwananchi wewe unajisikiaje pale nchi yako inakosa eneo maalumu kwa ajili ya Viongozi!!
Kwa sababu ya ufisadi na tamaa zao kuuza nyumba za serikali ambazo baba zetu waliziheshimu kwa miongo kadhaa leo hii zinaizwa kwa mkopo wa shilingi milioni 6-30!??Je kweli viongozi wetu wanenda kukaa kijitonyama nihaki wakati Oysterbay ilikuwepo leo limegeuzwa capital state!!!??Hapana tunataka zirudi serikalini Nikibahatika serikali yangu ikachukua madaraka tutaandamana hadi kwa rais wangu kumwomba zirudishwe serikalini!
Wewe mwana jamii unalionaje hili??
 
Naumia sana!!nipitapo maeneo ya oysterbay na kuona nyumba za mawaziri viongozi waandamizi zimekuwa apartments!!
 
Kwa taarifa yako, ni ahadi kama hizo za kurejesha nyumba za serikali, kufikisha mafisadi ikiwa ni pamoja na mama mkuu mahakamani ndizo zimefanya muungwana na washkaji zake kuanza kukazania wimbo wa "mtu" anayetaka kuingia ikulu hata kwa kumwaga damu na kukanyaga maiti za wa-TZ kama ngazi. Inatisha! Wakati mwingine kauli za kuwarudi wakosaji zinawafanya walioko madarakani kuanza kuungana na kujiandaa kwa maafa. Kuna wakati nilifikiri ingekuwa vyema Dr. Slaa asiwe specific na matishio yoyote bali ayaweke kwenye mkakati wake wa kuongoza nchi. Kauli ya Shimbo si bure. CCM hawako tayari kupoteza maslahi waliyojikusanyia.
 
Back
Top Bottom