Wana JF,
Nimefuatilia kampeni za ubunge huko jimboni Arumeru mashariki kupitia vyombo vya habari.Kuna madai kuwa uelewa na uwezo wa mgombea wa CCM Bw. Siyoi Sumari juu ya mambo mbalimbali ya kijamii na kisiasa ya jimboni kwake ni mdogo ukilinganisha na ule wa mgombea wa CHADEMA Bw. Joshua Nassari. Ndiyo maana wakati fulani wapiga debe wa CCM waliwahi kumuombea mgombea wao kura za huruma kwa kusema apewe kura za kushinda ili afutwe machozi.
SWALI.
Je, uandaliwe mdahalo utakaorushwa moja kwa moja na TBC baina ya wagombea hawa wawili tarehe 31-03-2012(siku moja kabla ya kupiga kura) ili wana-Arumeru na sisi pia tujiridhishe na madai haya?
Naomba kuwasilisha.
Nimefuatilia kampeni za ubunge huko jimboni Arumeru mashariki kupitia vyombo vya habari.Kuna madai kuwa uelewa na uwezo wa mgombea wa CCM Bw. Siyoi Sumari juu ya mambo mbalimbali ya kijamii na kisiasa ya jimboni kwake ni mdogo ukilinganisha na ule wa mgombea wa CHADEMA Bw. Joshua Nassari. Ndiyo maana wakati fulani wapiga debe wa CCM waliwahi kumuombea mgombea wao kura za huruma kwa kusema apewe kura za kushinda ili afutwe machozi.
SWALI.
Je, uandaliwe mdahalo utakaorushwa moja kwa moja na TBC baina ya wagombea hawa wawili tarehe 31-03-2012(siku moja kabla ya kupiga kura) ili wana-Arumeru na sisi pia tujiridhishe na madai haya?
Naomba kuwasilisha.