KIMBURU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2011
- 210
- 189
Nimesikitishwa sana na kauli ya Naibu Wazili wa Elimu kuwa wanafunzi watakaobainika kuwa hawajui kusoma na kuandika na wamefaulu kwenda sekondari, watarudishwa na kisha walimu wa shule walizotoka watawajibishwa.
Pia kuhusu wanafunzi ambao majibu yao yameonekana kufanana sana wamefutiwa matokeo na pia walimu wao watawajibishwa.
Wizara ilitegemea nini kuanzisha mfumo wa majibu ya kuchagua (multiple choice) kwa masomo na maswali yote? Hikujua kuwa mfumo huo unatoa mwanya mkubwa kwa wanafunzi kuigiliziana majibu? na pia haikujua kuwa mfumo huo unawawezesha hata wasiojua kusoma na kuandika kubuni majibu sahihi?
Miaka 50 ya uhuru bado tunaifanyia majiribio Elimu yetu?
Kwa hili naomba Rais KIQUETE awawajibishe watendaji wa wizara hii ambao wameleta mfumo huu usio na mantiki; na sasa wanajikosha kwa kukimbilia kuwaadhibu walimu wasio na makosa.
Pia kuhusu wanafunzi ambao majibu yao yameonekana kufanana sana wamefutiwa matokeo na pia walimu wao watawajibishwa.
Wizara ilitegemea nini kuanzisha mfumo wa majibu ya kuchagua (multiple choice) kwa masomo na maswali yote? Hikujua kuwa mfumo huo unatoa mwanya mkubwa kwa wanafunzi kuigiliziana majibu? na pia haikujua kuwa mfumo huo unawawezesha hata wasiojua kusoma na kuandika kubuni majibu sahihi?
Miaka 50 ya uhuru bado tunaifanyia majiribio Elimu yetu?
Kwa hili naomba Rais KIQUETE awawajibishe watendaji wa wizara hii ambao wameleta mfumo huu usio na mantiki; na sasa wanajikosha kwa kukimbilia kuwaadhibu walimu wasio na makosa.